Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 22 uku. 56-uku. 57 fu. 3
  • Muujiza Katika Bahari Nyekundu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Muujiza Katika Bahari Nyekundu
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Kuvuka Bahari Nyekundu (ya Shamu)
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • ‘Yah Ndiye Wokovu Wangu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • “Simameni Imara Muuone Wokovu wa Yehova”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 22 uku. 56-uku. 57 fu. 3
Farao na jeshi lake

SOMO LA 22

Muujiza Katika Bahari Nyekundu

Muda mfupi tu baada ya kusikia kwamba Waisraeli wameondoka Misri, Farao alibadili mawazo yake kuhusu kuwaruhusu waondoke. Aliwaamuru hivi mashujaa wake wa vita: ‘Tayarisheni magari ya vita ili tuwafuate! Hatukupaswa kuwaruhusu waondoke.’ Farao na wanaume wake wakaanza kuwafuata Waisraeli.

Yehova alikuwa akiwaongoza watu wake kupitia wingu wakati wa mchana na nguzo ya moto wakati wa usiku. Aliwaongoza hadi kufikia Bahari Nyekundu, na kuwaambia wapige kambi.

Kisha Waisraeli wakaona Farao na jeshi lake wakiwafuatilia. Walijikuta wakiwa wamenaswa kati ya bahari na jeshi la Wamisri. Wakaanza kumlilia Musa na kusema, ‘Tutakufa! Ni bora ungetuacha Misri.’ Lakini Musa akawaambia: ‘Msiogope. Simameni imara muuone wokovu wa Yehova.’ Kwa kweli Musa alimtumaini Yehova, sivyo?

Yehova akawaambia Waisraeli wavunje kambi. Usiku huo, Yehova akalihamisha wingu na kuliweka katikati ya Wamisri na Waisraeli. Kukawa na giza upande wa Wamisri, lakini upande wa Waisraeli kukawa na mwangaza.

Yehova akamwambia Musa aunyooshe mkono wake juu ya bahari. Kisha Yehova akafanya upepo wenye nguvu uvume usiku kucha. Bahari ikagawanyika na kukawa na njia katikati yake. Idadi kubwa ya Waisraeli wakapita katikati ya bahari juu ya nchi kavu, huku maji yakiwa kama ukuta kando yao nao wakaelekea upande wa pili wa bahari.

Waisraeli walipita katikati ya bahari juu ya nchi kavu, huku maji yakiwa kama ukuta kando yao

Jeshi la Farao likawafuata Waisraeli ndani ya bonde la bahari. Kisha Yehova akavuruga jeshi hilo. Magurudumu ya magari yao ya vita yakaanza kutoka. Wanajeshi hao wakapiga kelele na kusema: ‘Tuondoke hapa, kwa kuwa Yehova anawapigania Waisraeli!’

Yehova akamwambia Musa: ‘Nyoosha mkono wako juu ya bahari.’ Ghafla kuta za maji zikaangukia jeshi la Wamisri. Farao na wanaume wake wote wakafa. Hakuna hata mmoja aliyeokoka.

Ng’ambo ile nyingine ya bahari, umati mkubwa ulikuwa ukimsifu Mungu kwa kuimba hivi: “Mwimbieni Yehova, kwa maana amekwezwa sana. Farasi na mpandaji wake amewavurumisha baharini.” Watu walipokuwa wakiimba, wanawake walikuwa wakicheza dansi wakiwa na matari. Kila mtu alikuwa na furaha kwa sababu sasa walikuwa huru kabisa.

“Ili tuwe hodari na kusema: ‘Yehova ni msaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu atanifanya nini?’”​—Waebrania 13:6

Maswali: Ni nini kilichotokea kwenye Bahari Nyekundu? Yehova aliwaokoaje Waisraeli?

Kutoka 13:21–15:21; Nehemia 9:9-11; Zaburi 106:9-12; 136:11-15; Waebrania 11:29

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki