Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 6/15 uku. 24
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Habari Zinazolingana
  • Kuvuka Bahari Nyekundu (ya Shamu)
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • ‘Yah Ndiye Wokovu Wangu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Muujiza Katika Bahari Nyekundu
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 6/15 uku. 24

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Je! Farao wa Kutoka alikufa wakati jeshi la Misri lilipoharibiwa katika Bahari Nyekundu?

Ndiyo, alikufa, ingawa kitabu cha Kutoka hakisemi uhakika huo moja kwa moja. Kinasema:

“Wale Wamisri wakawafuatia [Waisraeli], wakaingia ndani kati ya bahari, farasi zote za Farao, na magari yake, na wapanda farasi wake.. .. [Yehova] akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao. Musa akaunyosha mkono wake . . . Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.”​—Kutoka 14:23-28.

Masimulizi hayo yanataja wapanda farasi na majeshi, lakini hayasemi waziwazi kama Farao alikufa. Wala wimbo wa ushindi wa Waisraeli, ambao katika huo walisema: “Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini maakida yake wateule wamezama katika Bahari ya Shamu.”​—Kutoka 15:4.

Lakini, Zaburi 136:1-15 inaonyesha kwamba Farao aliangamia. Hapo tunasoma watu wakimtolea shukrani ‘Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao, na Yeye aliyewatoa Waisraeli katikati yao kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa, yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, akawavusha Israeli katikati yake, na akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu.

Kwa hiyo kitabu cha Zaburi kinakamilisha Kutoka na kuonyesha kwamba Farao mwenye kimbelembele, aliyewaonea Waisraeli, alikufa ndani ya Bahari ya Shamu (Nyekundu).

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki