Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 48 uku. 116-uku. 117 fu. 1
  • Mwana wa Mjane Afanywa Kuwa Hai Tena

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwana wa Mjane Afanywa Kuwa Hai Tena
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mjane wa Sarefathi Alithawabishwa kwa Sababu ya Imani Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je! Wewe Una Imani Kama Ile ya Eliya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Igeni Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 48 uku. 116-uku. 117 fu. 1
Eliya anamwita mjane anayekusanya kuni

SOMO LA 48

Mwana wa Mjane Afanywa Kuwa Hai Tena

Mtungi wa unga na mtungi wa mafuta

Wakati wa ukame, Yehova alimwambia Eliya hivi: ‘Nenda Sarefathi. Mjane fulani huko atakupa chakula.’ Akiwa kwenye malango ya jiji, Eliya alikutana na mjane maskini akikusanya kuni. Akamwomba kikombe cha maji. Alipokuwa akienda kuyaleta, Eliya akamwita na kumwambia: ‘Tafadhali niletee kipande cha mkate.’ Lakini mjane huyo akamwambia: ‘Sina mkate wowote wa kukupa. Nina unga na mafuta yanayotosha kutayarisha chakula kidogo tu kwa ajili yangu na mwanangu.’ Eliya akamwambia: ‘Yehova ameahidi kwamba ukinitayarishia mkate, unga wako na mafuta yako hayatakwisha hadi mvua zitakaporudi.’

Kwa hiyo, yule mjane akarudi nyumbani na kutayarisha mkate kwa ajili ya nabii wa Yehova. Kama tu Yehova alivyoahidi, yule mjane na mwana wake walikuwa na chakula kipindi chote cha ukame. Mitungi yake ya unga na mafuta haikupungua.

Kisha jambo fulani baya likatukia. Mvulana wa yule mjane akawa mgonjwa sana hivi kwamba akafa. Yule mjane akamsihi Eliya amsaidie. Eliya akamchukua yule mvulana na kumbeba hadi kwenye chumba cha darini. Akamlaza juu ya kitanda na kusali: ‘Yehova, tafadhali mfanye mvulana huyu awe hai tena.’ Ikiwa Yehova angefanya hivyo, je, unajua kwa nini hilo lingekuwa jambo la ajabu? Kwa sababu tunajua kwamba, kabla ya hapo hakuna mtu aliyewahi kurudishwa kuwa hai. Na huyo mjane na mwana wake hata hawakuwa Waisraeli.

Lakini mvulana huyo akawa hai tena naye akaanza kupumua! Eliya akamwambia mjane huyo: ‘Ona! Mwana wako yuko hai.’ Akashangilia sana na kumwambia Eliya hivi: ‘Kwa kweli wewe ni mtu wa Mungu. Ninajua hilo kwa sababu unasema tu kile ambacho Yehova anakuambia useme.’

Eliya akimpa mjane mtoto wake aliyefufuliwa

“Waangalieni kunguru: Hawapandi mbegu wala hawavuni; hawana bohari wala ghala; lakini Mungu huwalisha. Je, ninyi si wenye thamani kuliko ndege?”​—Luka 12:24

Maswali: Mjane wa Sarefathi alionyeshaje kwamba anamtegemea Yehova? Tunajuaje kwamba Eliya alikuwa nabii wa kweli wa Mungu?

1 Wafalme 17:8-24; Luka 4:25, 26

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki