Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 50 uku. 120-uku. 121 fu. 5
  • Yehova Amlinda Yehoshafati

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Amlinda Yehoshafati
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yehoshafati Anamtumaini Yehova
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • “Vita Si Yenu Bali Ni ya Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Uwe na Bidii kwa Ajili ya Nyumba ya Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Hukumu Yatekelezwa Katika Bonde la Kukata Maneno
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 50 uku. 120-uku. 121 fu. 5
Mfalme Yehoshafati na waimbaji Walawi wakiliongoza jeshi kutoka Yerusalemu

SOMO LA 50

Yehova Amlinda Yehoshafati

Yehoshafati, mfalme wa Yuda, alibomoa madhabahu na sanamu za Baali katika nchi yote. Alitaka watu wazijue sheria za Yehova. Kwa hiyo, akawatuma wakuu na Walawi katika nchi yote ya Yuda ili wawafundishe watu sheria za Yehova.

Mataifa yaliyokuwa karibu yaliogopa kushambulia Yuda kwa kuwa yalijua Yehova yuko pamoja na watu wake. Hata walimletea Mfalme Yehoshafati zawadi. Lakini Wamoabu, Waamoni, na wale walioishi kwenye eneo la Seiri wakaja kushambulia Yuda. Yehoshafati alijua kwamba alihitaji msaada wa Yehova. Akawakusanya pamoja wanaume, wanawake, na watoto wote Yerusalemu. Akiwa mbele yao, Yehoshafati akasali hivi: ‘Yehova, bila wewe, hatuwezi kushinda. Tafadhali tuambie tunalopaswa kufanya.’

Yehova akajibu sala hiyo akisema: ‘Msiogope. Nitawasaidia. Simameni mahali penu, simameni tuli, nanyi mtaona jinsi nitakavyowaokoa.’ Yehova aliwaokoaje?

Siku iliyofuata, Yehoshafati akachagua waimbaji na kuwaambia waende mbele ya jeshi. Walitembea kutoka Yerusalemu hadi kwenye uwanja wa vita katika eneo linaloitwa Tekoa.

Waimbaji walipokuwa wakimsifu Yehova kwa sauti kubwa za shangwe, Yehova aliwapigania watu wake. Aliwafanya Waamoni na Wamoabu wachanganyikiwe sana hivi kwamba wakaanza kupigana wenyewe kwa wenyewe, na hakuna hata mmoja wao aliyeokoka. Lakini Yehova akawalinda watu wa Yuda, wanajeshi, na makuhani. Watu wote katika nchi zilizowazunguka walisikia kuhusu jambo ambalo Yehova alikuwa amefanya, nao wakajua kwamba bado Yehova anawalinda watu wake. Yehova anawaokoaje watu wake? Katika njia nyingi. Hahitaji msaada wa wanadamu ili kufanya hivyo.

“Hamtahitaji kupigana vita hivi. Simameni mahali penu, simameni tuli, muuone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu.”​—2 Mambo ya Nyakati 20:17

Maswali: Yehoshafati alikuwa mfalme wa aina gani? Yehova alilindaje taifa la Yuda?

2 Mambo ya Nyakati 17:1-19; 20:1-30

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki