Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 57 uku. 138-uku. 139 fu. 1
  • Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yeremia hakuacha kuongea na watu kuhusu Yehova
    Wafundishe Watoto Wako
  • “Siwezi Kunyamaza Kimya”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • Utachagua Marafiki wa Aina Gani?
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Nimeyatia Maneno Yangu Katika Kinywa Chako”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 57 uku. 138-uku. 139 fu. 1
Yeremia akivunja chupa ya udongo mbele ya wazee

SOMO LA 57

Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri

Yehova alimchagua Yeremia awe nabii wa watu wa Yuda. Alimwambia awahubirie watu hao na kuwaonya waache kufanya mambo mabaya. Yeremia alisema hivi: ‘Lakini Yehova, mimi ni mvulana tu. Sijui jinsi ya kuzungumza na watu.’ Yehova akamwambia hivi: ‘Usiogope. Nitakuambia kile utakachosema. Nitakusaidia.’

Yehova akamwambia Yeremia akusanye wanaume wazee, avunje chupa ya udongo mbele yao, na kusema: ‘Hivi ndivyo Yerusalemu litakavyovunjwa.’ Yeremia alipofanya kama Yehova alivyomwagiza, wazee hao wakakasirika sana. Kuhani anayeitwa Pashuri akampiga Yeremia na kumweka katika mikatale. Yeremia hangeweza kusonga usiku kucha. Pashuri alipomwachilia asubuhi iliyofuata, Yeremia alisema hivi: ‘Siwezi kuvumilia tena. Nitaacha kuhubiri.’ Lakini, je, aliacha kuhubiri? Hapana. Yeremia alipotafakari kuhusu jambo hilo, alisema hivi: ‘Ujumbe wa Yehova ulikuwa kama moto unaowaka ambao umefungiwa ndani yangu. Siwezi kuacha kuhubiri.’ Yeremia aliendelea kuwaonya watu hao.

Miaka kadhaa ilipita, na kukawa na mfalme mwingine nchini Yuda. Makuhani na manabii wa uwongo waliuchukia ujumbe wa Yeremia. Waliwaambia wakuu hivi: ‘Mtu huyu anastahili kufa.’ Yeremia akasema hivi: ‘Mkiniua, mtamwua mtu asiye na hatia. Maneno ninayosema si yangu, ni ya Yehova.’ Wakuu waliposikia maneno hayo, wakasema hivi: ‘Mtu huyu hastahili kufa.’

Yeremia aliendelea kuhubiri, na wakuu wakakasirika sana. Wakamwambia mfalme amuue Yeremia. Mfalme Sedekia akawaambia kwamba wanaweza kumfanyia Yeremia chochote walichotaka. Wakamchukua na kumtupa ndani ya tangi refu lenye matope, wakitumaini kwamba angefia humo. Yeremia akaanza kuzama ndani ya matope.

Ebed-meleki na wanaume walio pamoja naye wakimtoa Yeremia ndani ya tangi

Kisha ofisa mmoja wa makao ya mfalme aliyeitwa Ebed-meleki akamwambia mfalme hivi: ‘Wakuu wamemtupa Yeremia ndani ya tangi! Tukimwacha humo, atakufa.’ Sedekia akamwamuru Ebed-meleki achukue wanaume 30 na kumtoa Yeremia katika tangi hilo. Je, hatupaswi kumwiga Yeremia ambaye hakuruhusu kitu chochote kimzuie kuhubiri?

“Mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu, lakini yule atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.”​—Mathayo 10:22

Maswali: Kwa nini Yeremia alimtii Yehova hata alipokuwa mvulana mdogo? Ni nani waliomzuia Yeremia kuhubiri?

Yeremia 1:1-19; 19:1-11; 20:1-13; 25:8-11; 26:7-16; 38:1-13

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki