Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 70 uku. 166-uku. 167 fu. 2
  • Malaika Watangaza Kuzaliwa kwa Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Malaika Watangaza Kuzaliwa kwa Yesu
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alizaliwa Wapi na Wakati Gani?
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kuzaliwa kwa Yesu—Wapi na Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Yesu Anazaliwa Katika Boma la Ng’ombe
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Kuzaliwa kwa Yesu—Wapi na Wakati Gani?
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 70 uku. 166-uku. 167 fu. 2
Malaika wanawatangazia wachungaji kuhusu kuzaliwa kwa Yesu

SOMO LA 70

Malaika Watangaza Kuzaliwa kwa Yesu

Mtawala wa Milki ya Roma, Kaisari Augusto, alitoa amri kwamba Wayahudi wote warudi kwenye majiji yao ili wakaandikishwe. Kwa hiyo, Yosefu na Maria wakasafiri kwenda Bethlehemu, ambako familia ya Yosefu ilitokea. Kwa wakati huo, Maria alikuwa karibu kuzaa.

Walipofika Bethlehemu, mahali pekee walipopata ili kupumzika palikuwa zizini. Hapo ndipo Maria alipomzaa Yesu mwana wake. Akamfunga kwa vitambaa na kumlaza kwa wororo katika hori.

Karibu na Bethlehemu, wachungaji fulani walikuwa nje wakati wa usiku, wakichunga makundi yao ya mifugo. Ghafla, malaika akasimama kando yao na utukufu wa Yehova ukamulika pande zote. Wachungaji hao wakaogopa, lakini malaika akawaambia hivi: ‘Msiogope, nina habari zenye kusisimua. Leo, Masihi amezaliwa Bethlehemu.’ Wakati huohuo, malaika wengi wakatokea katika mbingu, wakisema: ‘Utukufu juu kwa Mungu, na amani juu ya dunia.’ Kisha malaika hao wakatoweka. Wachungaji hao walitendaje?

Wachungaji hao wakaambiana hivi: ‘Twendeni moja kwa moja hadi Bethlehemu.’ Nao wakaenda haraka na kuwakuta Yosefu na Maria katika hori wakiwa na mtoto wao mchanga.

Wote waliosikia juu ya mambo ambayo malaika aliwaambia wachungaji hao walistaajabu. Maria alifikiria sana kuhusu maneno ya yule malaika na hakuyasahau kamwe. Basi wachungaji wakarudi kwenye makundi yao ya mifugo, wakimshukuru Yehova kwa ajili ya mambo yote waliyosikia na kuona.

“Nilitoka kwa Mungu nami nipo hapa. Sikuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, bali Yeye ndiye aliyenituma.”—Yohana 8:42

Maswali: Malaika walitangaza jinsi gani kuzaliwa kwa Yesu? Wachungaji walimpata nani huko Bethlehemu?

Luka 2:1-20; Isaya 9:6

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki