Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 91 uku. 212-uku. 213 fu. 1
  • Yesu Afufuliwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Afufuliwa
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Amkumbuka Mwana Wake
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Kaburi Tupu
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Yesu Yuko Hai
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Kaburi Tupu​—Yesu Yuko Hai!
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 91 uku. 212-uku. 213 fu. 1
Wanawake wanashangaa kuona kaburi la Yesu likiwa tupu

SOMO LA 91

Yesu Afufuliwa

Baada ya Yesu kufa, mwanamume fulani tajiri, aliyeitwa Yosefu, alimwomba Pilato amruhusu autoe mwili wa Yesu kutoka mtini. Yosefu akaufunga mwili wa Yesu kwa kitani bora na kuupaka manukato na kisha kuulaza ndani ya kaburi jipya. Pia akaviringisha jiwe kubwa kwenye mwingilio. Wakuu wa makuhani wakamwambia hivi Pilato: ‘Tunahofia kwamba baadhi ya wanafunzi wa Yesu watachukua mwili wake na baadaye watasema kwamba amefufuliwa.’ Hivyo Pilato akawaambia: ‘Funikeni mwingilio wa kaburi na mweke walinzi.’

Siku tatu baadaye, asubuhi na mapema, baadhi ya wanawake wakaenda kwenye kaburi na kupata kwamba jiwe lilikuwa limeondolewa. Ndani ya kaburi kulikuwa na malaika aliyewaambia hivi wanawake hao: ‘Msiogope. Yesu amefufuliwa. Nendeni mkawaambie wanafunzi wake wakakutane naye huko Galilaya.’

Maria Magdalene akaondoka haraka kwenda kuwatafuta Petro na Yohana. Akawaambia hivi: ‘Mtu fulani ameuchukua mwili wa Yesu!’ Petro na Yohana wakakimbia kwenda kaburini. Walipoona kwamba kaburi lilikuwa tupu, wakarudi nyumbani.

Maria aliporudi kaburini, aliona malaika wawili ndani na kuwaambia hivi: ‘Sijui walipompeleka Bwana wangu.’ Kisha akamwona mwanamume fulani, na akifikiri kwamba alikuwa mtunza-bustani, akasema: ‘Bwana, tafadhali niambie ulipomlaza.’ Lakini mwanamume huyo aliposema, “Maria!” akatambua kwamba alikuwa Yesu. Akalia na kusema: “Mwalimu!” na kumng’ang’ania. Yesu akamwambia hivi: ‘Nenda kwa ndugu zangu nawe uwaambie kwamba umeniona.’ Mara moja, Maria akakimbia kwa wanafunzi na kuwaambia kwamba amemwona Yesu.

Baadaye siku hiyo, wanafunzi wawili walikuwa wakitembea kutoka Yerusalemu kwenda Emau. Mwanamume fulani akajiunga nao na kuwauliza walikuwa wakizungumza kuhusu nini. Wakasema: ‘Je, hujasikia? Siku tatu zilizopita wakuu wa makuhani walimuua Yesu. Sasa wanawake fulani wanasema kwamba yuko hai!’ Mwanamume huyo akauliza hivi: ‘Je, hamuwaamini manabii? Walisema kwamba Kristo atakufa na kufufuliwa.’ Na akaendelea kuwaeleza maana ya Maandiko. Walipofika Emau, wanafunzi wakamwomba ajiunge nao. Wakati wa mlo wa jioni baada ya kusali kwa ajili ya mkate, wakatambua kwamba alikuwa Yesu. Kisha akatoweka.

Wanafunzi hao wawili wakafanya haraka kwenda Yerusalemu kwenye nyumba ambayo mitume walikuwa wamekutanika na wakawaambia kilichotokea. Walipokuwa kwenye nyumba hiyo, Yesu akatokea mbele yao wote. Mwanzoni mitume hawakuamini kwamba alikuwa Yesu. Kisha akasema hivi: ‘Tazameni mikono yangu; niguseni. Iliandikwa kwamba Kristo angefufuka kutoka kwa wafu.’

“Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna mtu anayekuja kwa Baba bila kupitia kwangu.”​—Yohana 14:6

Maswali: Ni nini kilichotokea wanawake walipoenda kwenye kaburi la Yesu? Ni nini kilichotokea katika barabara ya kwenda Emau?

Mathayo 27:57–28:10; Marko 15:42–16:8; Luka 23:50–24:43; Yohana 19:38–20:23

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki