Utangulizi wa Sehemu ya 10
Yehova ni Mfalme juu ya kila kitu. Sikuzote amekuwa na mamlaka juu ya kila kitu, naye ataendelea kuwa na mamlaka. Kwa mfano, Yeremia alipotupwa ndani ya shimo, Yehova alimwokoa ili asife. Alimwokoa Shadraki, Meshaki, na Abednego kutoka katika tanuru la moto na akamwokoa Danieli kutoka katika vinywa vya simba. Yehova alimlinda Esta ili aokoe taifa lake lote. Hataruhusu uovu uendelee milele. Unabii kuhusu ile sanamu kubwa na mti mkubwa unatoa uhakikisho kwamba hivi karibuni Ufalme wa Yehova utaondoa uovu wote na kutawala dunia.