Utangulizi wa Sehemu ya 12
Yesu aliwafundisha watu kuhusu Ufalme wa mbinguni. Pia aliwafundisha kusali jina la Mungu litakaswe, Ufalme wake uje, na mapenzi yake yatendeke duniani. Ikiwa wewe ni mzazi, mweleze mtoto wako sala hiyo inamaanisha nini kwetu. Yesu hakumruhusu Shetani avunje ushikamanifu wake. Yesu aliwachagua mitume wake, nao wakawa washiriki wa kwanza wa Ufalme huo wakitimiza kusudi muhimu. Ona jinsi Yesu alivyokuwa na bidii kwa ajili ya ibada safi. Kwa kuwa alitaka kuwasaidia watu, Yesu aliponya wagonjwa, akalisha wenye njaa, na hata akawafanya watu wawe hai tena. Kupitia miujiza hiyo yote, alionyesha kile ambacho Ufalme utawafanyia wanadamu.