WIMBO NA. 3
Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu
Makala Iliyochapishwa
1. Yehova umetupatia
tumaini bora.
Latusisimua sana,
tutalitangaza.
Mahangaiko ya maisha,
hutufanya tuhofu.
Nalo tumaini letu
Linadhoofika.
(KORASI)
Tumaini, nguvu,
na uhakika;
zatoka kwako Yehova.
Ili tuhubiri
kwa uhakika,
twakutegemea wewe.
2. Ichochee mioyo yetu,
tusikusahau.
Watufariji daima,
tunapolemewa.
Kutafakari wema wako,
kunatuimarisha.
Tuwajulishe wengine
jina lako kuu.
(KORASI)
Tumaini, nguvu,
na uhakika;
zatoka kwako Yehova.
Ili tuhubiri
kwa uhakika,
twakutegemea wewe.
(Ona pia Zab. 72:13, 14; Met. 3:5, 6, 26; Yer. 17:7.)