Wimbo Na. 152
Tumaini, Nguvu, na Uhakika Wetu
Makala Iliyochapishwa
Ee Yehova watupatia
tumaini bora.
Tunatangazia watu
tumaini hilo.
Mahangaiko maishani
hufanya tuogope,
Hivyo tumaini letu
laweza fifia.
(KORASI)
Tumaini, nguvu,
na uhakika.
Watoka kwako Yehova.
Ili tuhubiri
kwa uhakika,
twakutegemea wewe.
Ee Yehova mioyo yetu
isikusahau,
Unatufariji kila
tunapolemewa.
Kutafakari jambo hilo
kunatuimarisha,
Tutangaze kote jina
lako bila woga.
(KORASI)
Tumaini, nguvu,
na uhakika.
Watoka kwako Yehova.
Ili tuhubiri
kwa uhakika,
twakutegemea wewe.
(Ona pia Zab. 72:13, 14; Met. 3:5, 6, 26; Yer. 17:7.)