WIMBO NA. 48
Kutembea na Yehova Kila Siku
Makala Iliyochapishwa
(Mika 6:8)
1. Twatembea na Yehova,
Tukiwa na unyenyekevu.
Anatuonyesha sisi
Fadhili tusizostahili!
Mungu ametupa fursa
Ya kutembea naye.
Hivyo twajiweka wakfu.
Twasimama na Yehova.
2. Shetani ana hasira,
Na mwisho unakaribia,
Tunapata upinzani
Uwezao kutuogofya.
Yehova anatulinda;
Tunamkaribia.
Twamtumikia Yeye.
Sikuzote tumpende.
3. Tunapata msaada
Kupitia Neno na roho,
Kutaniko la Kikristo,
Nazo sala asikiazo.
Tutembeapo na Mungu,
Anatutegemeza.
Tuwe washikamanifu,
Na kuwa wenye kiasi.
(Ona pia Mwa. 5:24; 6:9; 1 Fal. 2:3, 4.)