WIMBO NA. 105
“Mungu Ni Upendo”
Makala Iliyochapishwa
1. Mungu ni mwenye upendo,
Hutaka tumuige.
Upendo tukiwa nao,
Tutatenda mema tu.
Ndiyo siri ya maisha;
Maisha ya Wakristo.
Upendo kama wa Kristo,
Kamwe hautashindwa.
2. Kupenda kweli na Mungu;
Hutuchochea sana.
Husamehe tukosapo;
Nguvu anatutia.
Upendo hauna wivu;
Huvumilia yote.
Na tupende ndugu zetu,
Pasipo unafiki.
3. ’Siwe na kinyongo kamwe;
Na kisikutawale.
Mtegemee Yehova;
Ufwate amri zake:
Penda Mungu na jirani,
Penda toka moyoni.
Na tuonyeshe upendo
Upendo wa Kikristo.
(Ona pia Marko 12:30, 31; 1 Kor. 12:31–13:8; 1 Yoh. 3:23.)