SEHEMU YA PILI
“Mlipachafua Mahali Pangu Patakatifu”—Ibada Safi Yachafuliwa
WAZO KUU: Yuda na Yerusalemu wapotoka kiroho na kiadili
Yehova aliwapenda na kuwatunza Waisraeli wakiwa “mali iliyothaminiwa sana.” (Kut. 19:5, maelezo ya chini.) Lakini walimkosea Yehova heshima kwa kuabudu miungu ya uwongo katika hekalu lilelile lililokuwa na jina lake! Walimkasirisha Yehova na kumletea aibu. Kwa nini Waisraeli walipotoka sana? Tunajifunza nini kutokana na unabii wa Ezekieli kuhusu kuharibiwa kwa Yerusalemu? Na tunapata somo gani kutokana na jinsi Waisraeli walivyoshughulika na mataifa yaliyowazunguka?