SEHEMU YA TATU
‘Nitawakusanya Pamoja’ Ahadi ya Kurudishwa kwa Ibada Safi
WAZO KUU: Unabii wa Ezekieli wafunua kurudishwa kwa ibada safi
Taifa la Israeli limesambaratika—halina umoja kwa sababu ya uasi imani. Linapatwa na matokeo ya matendo yake; lilichafua ibada safi na kuliletea suto jina la Mungu. Katika hali hiyo ya kusikitisha, Yehova anamchochea Ezekieli atoe mfululizo wa unabii unaoleta tumaini. Akitumia lugha ya mfano na maono yenye kustaajabisha, Yehova anawatia moyo mateka wa Israeli na wote wanaotamani kuona ibada safi ikirudishwa.