Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • th somo la 6 uku. 9
  • Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko
  • Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kutumia Maandiko Vizuri
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Umalizio Wenye Matokeo
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kuonyesha Wasikilizaji Manufaa ya Habari Unayozungumzia
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
Pata Habari Zaidi
Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
th somo la 6 uku. 9

SOMO LA 6

Kuonyesha Waziwazi Matumizi ya Andiko

Andiko lililotajwa

Yohana 10:33-36

MUHTASARI: Usisome tu andiko na kuanza kuzungumzia jambo linalofuata. Hakikisha wasikilizaji wako wanaona waziwazi uhusiano kati ya andiko ulilosoma na jambo unalokazia.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tenga maneno makuu. Baada ya kusoma andiko, onyesha wazi maneno yanayohusiana moja kwa moja na jambo kuu. Unaweza kufanya hivyo kwa kurudia maneno hayo au kwa kuuliza swali linalowafanya wasikilizaji watambulishe maneno makuu.

    Dokezo linalofaa

    Ukiamua kutumia maneno tofauti kutaja wazo kuu la andiko, hakikisha kwamba bado wasikilizaji wanaweza kuona jinsi maneno katika Biblia yanavyohusiana na jambo kuu unalozungumzia.

  • Kazia jambo kuu. Ikiwa kabla ya kusoma andiko ulieleza sababu ya kulisoma, eleza jinsi maneno makuu ya andiko hilo yanavyopatana na sababu hiyo.

    Dokezo linalofaa

    Unapoeleza andiko hilo, iache Biblia yako wazi. Ukifanya hivyo wasikilizaji watakuiga na wataona mambo unayoeleza katika Biblia zao.

  • Rahisisha matumizi ya andiko. Epuka kuzungumzia mambo ambayo hayasaidii kuonyesha wazi jambo kuu. Kwa kutegemea wasikilizaji wako wanajua nini tayari kuhusu habari hiyo, amua ni mambo mangapi ambayo lazima yatajwe ili matumizi yawe wazi na yaeleweke.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki