SOMO LA 17
Habari Inayoeleweka
1 Wakorintho 14:9
MUHTASARI: Wasaidie wasikilizaji waelewe maana ya ujumbe wako.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Jifunze kwa makini habari unayotayarisha. Jitahidi kuelewa kabisa habari ili uweze kuieleza kwa njia rahisi na kwa maneno yako.
Tumia sentensi fupi na maneno rahisi. Ingawa unaweza kutumia sentensi ndefu, wasilisha mawazo makuu ukitumia maneno machache na sentensi fupi.
Fafanua maneno yasiyojulikana. Usitumie maneno mengi ambayo wasikilizaji wako hawayaelewi. Ikiwa ni lazima utumie neno lisilojulikana, mhusika katika Biblia, vipimo au utamaduni wa kale, wafafanulie wasikilizaji mambo hayo.