Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 25
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Kusudi Lenyewe la Uhai
    Amkeni!—1992
  • Uhai Una Kusudi Tukufu
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Mungu Ni Nani?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Uhai Ulianzaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 25
Somo la 25. Dunia inavyoonekana kutoka angani.

SOMO LA 25

Mungu Ana Kusudi Gani kwa Wanadamu?

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Biblia inasema kwamba maisha ya wanadamu ni ‘mafupi na yamejaa taabu.’ (Ayubu 14:1) Je, Mungu anataka tuwe na maisha kama hayo? Ikiwa sivyo, ana kusudi gani kwa wanadamu? Je, kusudi hilo litatimizwa? Chunguza majibu yenye kufariji yanayopatikana katika Biblia.

1. Yehova anataka tuishi maisha ya aina gani?

Yehova anataka tuwe na maisha bora kabisa. Alipowaumba wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa, aliwaweka katika paradiso maridadi, bustani ya Edeni. Kisha “Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia na kuitiisha.’” (Mwanzo 1:28) Yehova alitaka wapate watoto, waifanye dunia nzima kuwa paradiso na kuwatunza wanyama. Alikusudia kwamba watu wote wawe na afya kamilifu na waishi milele.

Ingawa mambo ni tofauti leo,a kusudi la Mungu halijabadilika. (Isaya 46:10, 11) Bado anataka wanadamu watiifu waishi milele katika hali kamilifu.​—Soma Ufunuo 21:3, 4.

2. Tunawezaje kuwa na maisha yenye kusudi leo?

Yehova alituumba tukiwa na ‘uhitaji wa kiroho,’ yaani, tamaa ya kumjua na kumwabudu. (Soma Mathayo 5:3-6.) Anataka tuwe na urafiki wa karibu pamoja naye, ‘tutembee katika njia zake zote, tumpende,’ na kumtumikia ‘kwa moyo wetu wote.’ (Kumbukumbu la Torati 10:12; Zaburi 25:14) Tunapofanya hivyo, tunakuwa na furaha ya kweli hata ingawa tunakabili matatizo. Tunapomwabudu Yehova, maisha yetu yanakuwa na kusudi la kweli kwa sababu tunaishi kulingana na viwango vyake.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kuhusu upendo mkubwa ambao Yehova alionyesha alipoumba dunia kwa ajili ya wanadamu na kile ambacho Neno lake linasema kuhusu kusudi la uhai.

Adamu na Hawa wakitazama bustani maridadi iliyokuwa makao yao yenye mimea na wanyama.

3. Yehova anataka wanadamu wafurahie maisha yenye kusudi

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Kwa Nini Mungu Aliiumba Dunia?​—Kisehemu (1:41)

  • Kwa nini Mungu aliiumba dunia yetu maridadi?

Soma Mhubiri 3:11, kisha mzungumzie swali hili:

  • Andiko hili linakufundisha nini kumhusu Yehova?

4. Kusudi la Yehova halijabadilika

Soma Zaburi 37:11, 29 na Isaya 55:11, kisha mzungumzie swali hili:

  • Tunajuaje kwamba kusudi la Yehova kwa wanadamu halijabadilika?

A. Nyumba iliyoharibika. Paa limeanguka, madirisha yamevunjika, na bustani imejaa takataka. B. Sasa nyumba hiyo imerekebishwa na bustani imetunzwa vizuri.

Nyumba iliyoharibika kwa sababu ya kupuuzwa inaweza kurekebishwa. Vivyo hivyo, ingawa wanadamu wamekosa kuitunza dunia, Mungu atairekebisha kwa ajili ya wale wanaompenda

5. Kumwabudu Yehova hufanya maisha yetu yawe na kusudi la kweli

Tunapata furaha tunapojua kusudi la uhai. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Nilijifunza Kuhusu Kusudi la Uhai (5:03)

  • Terumi alinufaikaje alipojifunza kusudi la uhai?

Soma Mhubiri 12:13, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kwa kuwa Yehova ametufanyia mambo mengi sana, tunawezaje kumwonyesha shukrani?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Maisha yana kusudi gani?”

  • Wewe ungejibuje swali hilo?

MUHTASARI

Yehova anataka tufurahie maisha milele katika hali kamilifu hapa duniani. Tunapomwabudu kwa moyo wetu wote, maisha yetu yanakuwa na kusudi hata sasa.

Ungejibuje?

  • Yehova alikuwa na kusudi gani alipowaumba Adamu na Hawa?

  • Tunajuaje kwamba kusudi la Mungu kwa wanadamu halijabadilika?

  • Unawezaje kupata kusudi la kweli maishani?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Chunguza mambo yanayothibitisha kwamba bustani ya Edeni ilikuwepo.

“Je, Bustani ya Edeni Ilikuwa Halisi au Ni Hadithi Tu?” (Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2011)

Chunguza uone kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba dunia itadumu milele.

“Je, Dunia Itaharibiwa?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Jifunze Biblia inasema nini kuhusu jinsi unavyoweza kupata kusudi maishani.

“Ni Nini Maana ya Uhai?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Ona jinsi mwanamume aliyefikiri ana kila kitu alivyopata kusudi maishani.

Sasa Nimepata Kusudi Maishani (3:55)

a Katika somo linalofuata, utajifunza kwa nini kusudi la Mungu halikutimia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki