Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 55
  • Unga Mkono Kutaniko Lenu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unga Mkono Kutaniko Lenu
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Tunamshukuru Yehova kwa Upendo Wenu
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • “Jaza Mkono Zawadi kwa Ajili ya Yehova”
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
  • Maoni ya Biblia Kuhusu Pesa na Kazi
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kwa Nini Umpe Yule Aliye na Kila Kitu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 55
Somo la 55. Ndugu na dada wakisaidia kufanya marekebisho nje ya Jumba lao la Ufalme.

SOMO LA 55

Unga Mkono Kutaniko Lenu

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Ulimwenguni pote, mamilioni ya watu wanamwabudu Yehova kwa shangwe katika maelfu ya makutaniko. Wanafurahi kupokea maagizo na mwongozo, na wanaunga mkono kutaniko kwa bidii katika njia nyingi. Je, unahisi hivyo kuhusu kutaniko lenu?

1. Unawezaje kutumia muda na nguvu zako kuunga mkono kutaniko?

Sisi sote tunaweza kuunga mkono kutaniko. Kwa mfano, je, katika kutaniko lenu kuna watu wenye umri mkubwa au wenye matatizo ya afya? Je, unaweza kuwasaidia kufika kwenye mikutano? Au je, unaweza kuwasaidia kwa njia nyingine, kama vile kufanya ununuzi au kazi za nyumbani? (Soma Yakobo 1:27.) Pia, tunaweza kujitolea kusafisha na kudumisha Jumba letu la Ufalme. Hakuna mtu anayetulazimisha kufanya mambo hayo. Kumpenda Mungu na ndugu zetu hutuchochea ‘kujitoa wenyewe kwa hiari.’​—Zaburi 110:3.

Mashahidi waliobatizwa wanaweza kuunga mkono kutaniko kwa njia nyingine. Akina ndugu wenye sifa za kustahili wanaweza kutumikia wakiwa watumishi wa huduma, na baadaye wakiwa wazee. Akina ndugu na dada wanaweza kuunga mkono kwa bidii kazi ya kuhubiri kwa kutumikia wakiwa mapainia. Baadhi ya Mashahidi wanaweza kusaidia katika ujenzi wa majengo ya ibada au kuhamia katika kutaniko linalohitaji msaada kwa njia nyingine.

2. Tunawezaje kutumia pesa na mali zetu kuunga mkono kutaniko?

Tunaweza ‘kumheshimu Yehova kwa vitu vyetu vyenye thamani.’ (Methali 3:9) Tunafurahi kuwa na pendeleo la kutoa michango ya pesa na mali nyingine ili kuunga mkono kutaniko letu na kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. (Soma 2 Wakorintho 9:7.) Michango yetu hutumiwa pia kutoa msaada wakati wa misiba. Wengi huamua “kuweka kando kitu fulani” kwa ukawaida ili kutoa mchango. (Soma 1 Wakorintho 16:2.) Tunaweza kuweka michango yetu katika masanduku ya michango yaliyo kwenye sehemu zetu za ibada au mtandaoni kupitia donate.jw.org. Yehova anatupatia nafasi ya kuonyesha kwamba tunampenda kupitia jinsi tunavyoamua kutumia mali zetu.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza baadhi ya njia unazoweza kuunga mkono kutaniko.

3. Tunaweza kutumia mali zetu

Yehova na Yesu wanawapenda watu wanaotoa kwa uchangamfu. Kwa mfano, Yesu alimsifu mjane maskini ambaye alitoa mchango mdogo sana. Soma Luka 21:1-4, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Je, tunahitaji kutoa mchango wa pesa nyingi ili kumfurahisha Yehova?

  • Yehova na Yesu wanahisije tunapotoa michango kwa hiari?

Ili ujifunze jinsi michango yetu inavyotumiwa, Onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: ‘Jaza Mkono Zawadi kwa Ajili ya Yehova’ (4:47)

  • Michango hutumiwaje kutegemeza makutaniko ulimwenguni pote?

Dada mwenye umri mkubwa akiweka mchango kwenye sanduku la michango.

4. Tunaweza kujitolea kusaidia

Katika nyakati za Biblia, waabudu wa Yehova walifanya kazi kwa bidii ili kudumisha sehemu zao za ibada. Lakini hilo lilihusisha mengi zaidi ya kutoa mchango wa pesa. Soma 2 Mambo ya Nyakati 34:9-11, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kila Mwisraeli alisaidiaje kutunza nyumba ya Yehova, au mahali pa ibada?

Ili uone jinsi Mashahidi wa Yehova wanavyoiga mfano huo, onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

VIDEO: Kutunza Maeneo Yetu ya Ibada (3:31)

Picha ya video ‘Kutunza Maeneo Yetu ya Ibada.’ Wanaume, wanawake, na watoto wanafanya usafi ndani ya Jumba lao la Ufalme.
  • Kwa nini ni muhimu kudumisha Jumba letu la Ufalme likiwa safi na katika hali nzuri?

  • Unaweza kusaidia katika njia gani?

Kikundi cha wajitoleaji Mashahidi wakisaidia katika ujenzi wa Jumba la Ufalme.

5. Akina ndugu wanaweza kujitahidi kufikia mapendeleo zaidi

Maandiko yanawatia moyo wanaume Wakristo wajitahidi kufanya mengi zaidi ili kuunga mkono kutaniko. Ili uone mfano, onyesha VIDEO. Kisha ujibu swali linalofuata.

VIDEO: Akina Ndugu–Jitahidini Kufikia Kazi Njema (5:19)

  • Katika video hiyo, Ryan alifanya jitihada gani ili kuunga mkono kutaniko kikamili zaidi?

Biblia inataja sifa ambazo akina ndugu wanahitaji ili wastahili kutumikia wakiwa watumishi wa huduma au wazee. Soma 1 Timotheo 3:1-13, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Akina ndugu wanaotamani kutumikia wakiwa watumishi wa huduma na wazee wanapaswa kuwa na sifa gani?

  • Familia zao zinapaswa kuwa na sifa gani?​—Ona mstari wa 4 na 11.

  • Akina ndugu wanapojitahidi kutimiza sifa hizo, kila mmoja katika kutaniko hunufaikaje?

Ndugu kijana akisukuma kigari cha ndugu aliyezeeka wanapohubiri nyumba kwa nyumba.

HUENDA MTU AKAULIZA: “Mashahidi wa Yehova wanapata wapi pesa za kuendeleza kazi yao?”

  • Wewe ungejibuje?

MUHTASARI

Yehova anathamini sana jitihada zetu za kuunga mkono kutaniko kupitia muda, nguvu, na mali zetu.

Ungejibuje?

  • Tunawezaje kutumia muda na nguvu zetu kuunga mkono kutaniko?

  • Tunawezaje kutumia mali zetu kuunga mkono kutaniko?

  • Ungependa kuunga mkono kutaniko kupitia njia gani?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Chunguza kwa nini leo Mungu hajawawekea waabudu wake sheria ya kutoa sehemu ya kumi.

“Biblia Inasema Nini Kuhusu Kutoa Fungu la Kumi?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Biblia huwapatia baadhi ya majukumu wanaume waliobatizwa. Hata hivyo, vipi ikiwa mwanamke aliyebatizwa atahitaji kutimiza majukumu hayo?

Kuuelewa Mpango wa Ukichwa Kutanikoni (Mnara wa Mlinzi, Februari 2021)

Ona baadhi ya Mashahidi wenye ujasiri wanaojidhabihu sana ili kuwapelekea waabudu wenzao machapisho.

Usambazaji wa Machapisho ya Biblia Nchini Kongo (4:25)

Ona jinsi kazi yetu inavyotegemezwa kifedha kwa njia tofauti sana na mashirika mengine ya kidini.

“Kazi ya Mashahidi wa Yehova Inagharimiwaje?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki