Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lffi somo la 1
  • Biblia Inawezaje Kukusaidia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inawezaje Kukusaidia?
  • Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Biblia Inawezaje Kukusaidia?
    Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
  • Jinsi Unavyoweza Kunufaika Zaidi Unaposoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ni Nini Kitakachokusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
lffi somo la 1
Somo la 1. Biblia.

SOMO LA 1

Biblia Inawezaje Kukusaidia?

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Sisi sote hujiuliza maswali kuhusu maisha, kuteseka, kifo, na wakati ujao. Pia tunahangaikia shughuli za kila siku, kama vile kupata riziki na jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Watu wengi wametambua kwamba Biblia imewasaidia kupata majibu ya maswali muhimu maishani na pia ushauri unaotegemeka kuhusu maisha ya kila siku. Je, unamjua mtu yeyote ambaye anaweza kunufaika kwa kujifunza Biblia?

1. Biblia inajibu maswali gani?

Biblia inajibu maswali haya muhimu: Uhai ulianzaje? Maisha yana kusudi gani? Kwa nini watu huteseka? Ni nini humpata mtu anapokufa? Ingawa kila mtu anapenda amani, kwa nini kuna vita ulimwenguni? Ni nini kitakachoipata dunia wakati ujao? Biblia inatutia moyo tutafute majibu ya maswali hayo, na watu wengi wamepata majibu yenye kuridhisha.

2. Biblia inawezaje kutusaidia tufurahie maisha ya kila siku?

Biblia hutupatia ushauri mzuri. Kwa mfano, inatufundisha jinsi ya kuwa na familia yenye furaha. Pia, inatoa ushauri kuhusu kukabiliana na mikazo na jinsi ya kufurahia kazi. Utajifunza yale ambayo Biblia inafundisha kuhusu mambo hayo na mengine mengi katika chapisho hili. Tuna hakika utakubali kwamba “kila Andiko [katika Biblia] . . . ni lenye faida.”​—2 Timotheo 3:16.

Chapisho hili si Biblia. Hata hivyo, litakusaidia kuichunguza Biblia. Kwa hiyo, tunakutia moyo usome maandiko yaliyo kwenye masomo haya na uyalinganishe na mambo unayojifunza.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze jinsi ambavyo Biblia imewasaidia watu, jinsi unavyoweza kufurahia kuisoma, na kwa nini unapaswa kutafuta msaada ili kuielewa.

3. Biblia inaweza kutuongoza

Biblia ni kama tochi yenye mwangaza mkali. Tunaweza kutumia Biblia kujua jinsi ya kufanya maamuzi mazuri na kutambua mambo yatakayotokea wakati ujao.

Soma Zaburi 119:​105, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yule aliyeandika andiko hili alikuwa na maoni gani kuhusu Biblia?

  • Wewe una maoni gani kuhusu Biblia?

Mwanamume akitembea gizani kwenye ufuo wenye mawe, anatumia tochi kumulika njia yake.

4. Biblia inajibu maswali tunayojiuliza

Mwanamke fulani alitambua kwamba Biblia ina majibu ya maswali yaliyomhangaisha kwa miaka mingi. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:

VIDEO: Usikate Tamaa Kamwe! (1:48)

  • Katika video hiyo, mwanamke huyo alijiuliza maswali gani?

  • Kujifunza Biblia kulimsaidiaje?

Biblia inatutia moyo tuulize maswali. Soma Mathayo 7:​7, kisha mzungumzie swali hili:

  • Wewe hujiuliza maswali gani ambayo yanaweza kujibiwa na Biblia?

5. Unaweza kufurahia kusoma Biblia

Watu wengi wanafurahia kusoma Biblia na wananufaika kwa kufanya hivyo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:

VIDEO: Kusoma Biblia (2:05)

  • Katika video hiyo, vijana hao walihisije kuhusu kusoma?

  • Kwa nini sasa wanapenda kusoma Biblia?

Biblia inasema kwamba inaweza kutupatia mwongozo unaotupatia faraja na tumaini. Soma Waroma 15:4, kisha mzungumzie swali hili:

  • Je, unafurahia ahadi ya Biblia ya kukupatia faraja na tumaini?

6. Watu wengine wanaweza kutusaidia kuelewa Biblia

Zaidi ya kusoma Biblia wakiwa peke yao, watu wengi wametambua kwamba wanaielewa vizuri zaidi wanaposaidiwa na watu wengine. Soma Matendo 8:26-31, kisha mzungumzie swali hili:

  • Tunawezaje kuielewa Biblia vizuri?​—Ona mstari wa 30 na 31.

Picha: 1. Mweneza-injili Filipo anamfafanulia Maandiko mwanamume Mwethiopia. 2. Shahidi wa Yehova akijifunza Biblia pamoja na mama na watoto wake wawili.

Mwanamume Mwethiopia alihitaji msaada ili kuelewa Maandiko. Leo watu wengi wananufaika kwa kujifunza Biblia pamoja na wengine

WATU FULANI HUSEMA: “Kujifunza Biblia ni kupoteza wakati.”

  • Wewe una maoni gani? Kwa nini?

MUHTASARI

Biblia inatoa ushauri mzuri kuhusu maisha ya kila siku, inajibu maswali muhimu, na inawapa watu faraja na tumaini.

Ungejibuje?

  • Biblia inatoa ushauri wa aina gani?

  • Biblia inajibu maswali gani?

  • Ungependa kujifunza nini katika Biblia?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi ushauri wa Biblia unavyotufaa leo.

“Mafundisho ya Biblia​—Hekima Isiyopitwa na Wakati” (Mnara wa Mlinzi Na. 1 2018)

Ona jinsi Biblia ilivyomsaidia mwanamume aliyepambana na hisia mbaya tangu utotoni.

Jinsi Nilivyoanza Kufurahia Maisha Mapya (2:53)

Chunguza ushauri wa Biblia kuhusu maisha ya familia.

“Siri 12 za Mafanikio Katika Familia” (Amkeni! Na. 2 2018)

Jifunze jinsi Biblia inavyofunua ukweli kuhusu yule anayeutawala ulimwengu huu.

Kwa Nini Ujifunze Biblia?​—Video Nzima (3:14)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki