Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 5
  • Busara

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Busara
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Paulo Alifanya Nini
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Paulo?
  • Mwige Paulo
  • “Wamtafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wampate”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Unyenyekevu
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Unayaonaje Mashamba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Ni Nani Tunayeweza Kutegemea kwa Haki ya Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 5

KUANZISHA MAZUNGUMZO

Mtume Paulo akijadiliana na watu wa Athene.

Matendo 17:​22, 23

SOMO LA 5

Busara

Kanuni: “Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote.”—Kol. 4:6.

Paulo Alifanya Nini

Mtume Paulo akijadiliana na watu wa Athene.

VIDEO: Paulo Anawahubiria Waathene

1. Tazama VIDEO, au soma Matendo 17:​22, 23. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Paulo alihisije kuhusu mazoea ya dini za uwongo aliyoona katika jiji la Athene?—Ona Matendo 17:16.

  2. Badala ya kuwahukumu Waathene, Paulo alitumiaje kwa busara mambo waliyoamini kama njia ya kuwahubiria habari njema?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Paulo?

2. Huenda watu wakatusikiliza zaidi ikiwa tutachagua kwa uangalifu mambo tutakayozungumza, jinsi tutakavyozungumza na wakati wa kuzungumza.

Mwige Paulo

3. Chagua maneno yanayofaa. Kwa mfano, unapozungumza na mtu ambaye si Mkristo, huenda ukahitaji kubadili jinsi unavyoitaja Biblia au unavyomrejelea Yesu.

4. Usiwe na haraka ya kumkosoa mtu. Mruhusu ajieleze. Ikiwa atasema jambo lolote lisilopatana na mafundisho ya Biblia, usibishane naye. (Yak. 1:19) Ukimsikiliza, utajua mambo anayoamini na kwa nini anayaamini.—Met. 20:5.

5. Kubaliana naye na mpongeze inapofaa kufanya hivyo. Huenda anaamini kwamba mafundisho ya dini yake ni sahihi. Kwanza, jaribu kuzungumzia mambo mnayokubaliana, kisha msaidie hatua kwa hatua aelewe mambo ambayo Biblia inafundisha.

SOMA PIA

Met. 25:15; 2 Tim. 2:​23-26; 1 Pet. 3:15

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki