Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 11
  • Fundisha kwa Njia Rahisi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fundisha kwa Njia Rahisi
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alifanya Nini?
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
  • Mwige Yesu
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jinsi ya Kuongoza Mafunzo ya Biblia kwa Kutumia Kitabu “Furahia Maisha Milele!”
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Kazia Uangalifu ‘Ufundi Wako wa Kufundisha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 11

KUFANYA WANAFUNZI

Yesu akiwafundisha watu karibu na mto. Ndege wanapaa angani, na maua ya porini yamechanua.

Mt. 6:​25-27

SOMO LA 11

Fundisha kwa Njia Rahisi

Kanuni: ‘Sema maneno yanayoeleweka kwa urahisi.’ —1 Kor. 14:9.

Yesu Alifanya Nini?

Yesu akiwafundisha watu karibu na mto. Ndege wanapaa angani, na maua ya porini yamechanua.

VIDEO: Yesu Anafafanua Jinsi Baba Yetu Anavyotujali

1. Tazama VIDEO, au soma Mathayo 6:​25-27. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Yesu alifafanuaje jinsi Yehova anavyotujali?

  2. Ingawa Yesu alijua mambo mengi kuhusu ndege, alikazia mambo gani rahisi? Kwa nini hiyo ilikuwa njia nzuri ya kufundisha?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Tunapofundisha kwa njia rahisi, watu watakumbuka mambo tunayowafundisha na tutagusa mioyo yao.

Mwige Yesu

3. Usizungumze kupita kiasi. Badala ya kuzungumzia kila kitu unachojua kuhusu somo hilo, kazia habari zilizo katika chapisho mnalojifunza. Baada ya kuuliza swali, subiri mwanafunzi wako atoe jibu. Ikiwa hajui jibu au anasema jambo lisilopatana na mafundisho ya Biblia, tumia maswali ya ziada kumsaidia aelewe habari hiyo. Mwanafunzi wako anapoelewa jambo kuu, endelea na sehemu inayofuata.

4. Msaidie mwanafunzi wako aone jinsi mafundisho mapya yanavyohusiana na mambo anayojua. Kwa mfano, kabla ya kuanza kujifunza kuhusu ufufuo, mnaweza kurudia kwa ufupi mambo ambayo mwanafunzi wako amejifunza kuhusu hali ya wafu.

5. Tumia mifano kwa uangalifu. Kabla ya kutumia mfano, jiulize hivi:

  1. ‘Je, mfano huu ni rahisi?’

  2. ‘Je, mwanafunzi wangu atauelewa kwa urahisi?’

  3. ‘Je, utamsaidia mwanafunzi wangu kukumbuka jambo kuu?’

SOMA PIA

Mt. 11:25; Yoh. 16:12; 1 Kor. 2:1

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki