Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/93 uku. 1
  • Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Kazia Uangalifu ‘Ufundi Wako wa Kufundisha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Jitayarishe Vizuri Kufundisha
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 12/93 uku. 1

Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia

1 Je! wataka mwanafunzi wako wa Biblia atende kulingana na yale anayojifunza? Ni lazima afanye hivyo ikiwa atanufaika na ujuzi anaopata. Ili umchochee mwanafunzi wako wa Biblia atende, ni lazima wewe uufikie moyo wake. Katika siku ya Pentekoste 33 W.K., hotuba ya mtume Petro yenye kuchochea ‘ilichoma mioyo’ ya watu 3,000 hivi, ambao “walilipokea neno lake [kwa moyo]” na wakabatizwa siku hiyo. (Mdo. 2:37, 41) Waweza kufikiaje moyo wa mwanafunzi wako wa Biblia?

2 Jitayarishe Kikamili: Usijaribu kuzungumzia habari nyingi mno hivi kwamba kunakuwa na wakati mchache wa kusababu pamoja na mwanafunzi juu ya habari hiyo. Amua kimbele mambo makuu utakayokazia, na uhakikishe kwamba unaelewa na unaweza kutumia maandiko kwa matokeo. Fikiria kimbele maswali ambayo huenda yakatokea kwenye akili ya mwanafunzi kwa sababu ya malezi yake. Ikiwa unafahamiana vizuri na mwanafunzi wako, ujuzi huo utakusaidia ujitayarishe na habari ambayo itamfaa yeye hasa.

3 Iga Njia ya Yesu ya Kufundisha: Yesu alitumia vielezi ili kurahisisha mambo magumu na kusaidia wanafunzi wake wapate maana na hisi ya hali. (Lk. 10:29-37) Vivyo hivyo, waweza kukazia mafundisho yafaayo katika moyo wa mwanafunzi wako wa Biblia kwa kutoa vielezi rahisi, ukivitumia kutoka kwa mambo ya kawaida ya maisha, na kuvitumia hasa kwa hali za mwanafunzi.

4 Maswali yana msaada hasa katika kufikia mioyo ya wanafunzi wa Biblia, kama Yesu alivyoonyesha mara nyingi. (Lk. 10:36) Lakini usitosheke ikiwa mwanafunzi anasoma jibu tu kutoka kwenye kitabu. Tumia maswali yenye kuongoza ili kuelekeza akili yake kwenye mkataa ambao huenda ikawa hakuufikiria kabla ya hapo. Njia hiyo pia husaidia mwanafunzi akuze uwezo wa kufikiri. Uliza maswali ya maoni ujue yeye mwenyewe huamini nini juu ya jambo fulani. Kisha huenda ukatambua mahali panapohitaji msaada, na waweza kufuatia kwa kumpa msaada hususa.

5 Ikiwa mwanafunzi wa Biblia hafanyi maendeleo, wahitaji kumfanya aseme sababu. Hilo huenda likatia ndani kumtembelea wakati mwingine licha ya wakati wa kawaida wa kujifunza. Kwa nini anasita kutenda? Je! kuna jambo fulani la Kimaandiko asiloelewa? Je! anasita kufanya mabadiliko fulani katika njia yake ya maisha? Ikiwa mwanafunzi wa Biblia anajaribu ‘kusita-sita katikati ya mawazo mawili,’ msaidie atambue hatari ya kufanya hivyo.—1 Fal. 18:21.

6 Mtume Paulo alitambua kuwa kufundisha watu wenye kupendezwa na kweli za Biblia ni kazi ya kuokoa uhai, na hivyo aliwashauri Wakristo wote ‘watoe uangalifu kwa mafundisho yao.’ (1 Tim. 4:16) Wale unaoongoza mafunzo ya Biblia nao lazima wajue mengi kuliko mambo hakika ya Biblia na matukio ya ulimwengu tu. Lazima wapate ujuzi sahihi kuhusu Yehova na Yesu na wasaidiwe kusitawisha uhusiano mchangamfu pamoja nao. Ni kwa kufanya hivyo tu kwamba watasukumwa kuonyesha imani yao kwa matendo. (Yak. 2:17, 21, 22) Moyo wa mwanafunzi unapofikiwa, atachochewa kufuata mwendo ambao utamheshimu Yehova na kulinda salama uhai wake mwenyewe.—Mit. 2:20-22.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki