Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/09 uku. 2
  • Jitayarishe Vizuri Kufundisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jitayarishe Vizuri Kufundisha
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 6/09 uku. 2

Jitayarishe Vizuri Kufundisha

1. Kwa nini tunapaswa kujitahidi sana kumsaidia mwanafunzi wa Biblia athamini kweli za Biblia?

1 Tunapoongoza funzo la Biblia, ni lazima tujitayarishe vizuri ikiwa tutafaulu kumchochea mwanafunzi amtumikie Yehova. Jitihada zetu zitakuwa na matokeo mazuri tukimsaidia mwanafunzi kuthamini kweli za Biblia. Mwanafunzi akithamini kweli za Biblia, atatamani kumtumikia Yehova. (Kum. 6:5; Met. 4:23; 1 Kor. 9:26) Tunawezaje kumsaidia mwanafunzi athamini kweli za Biblia?

2. Sala inawezaje kutusaidia kujitayarisha vizuri?

2 Sali Kabla ya Kujitayarisha: Kwa kuwa Yehova ndiye anayekuza mbegu za kweli katika moyo wa mwanafunzi, inafaa tusali kumhusu mwanafunzi na mahitaji yake kabla ya kuanza kujitayarisha kwa ajili ya funzo. (1 Kor. 3:6; Yak. 1:5) Sala kama hizo zinaweza kutusaidia pia kutambua jinsi tunavyoweza kumsaidia kuendelea kupata “ujuzi sahihi” kuhusu mapenzi ya Yehova.—Kol. 1:9, 10.

3. Tunaweza kumfikiria mwanafunzi jinsi gani tunapojitayarisha kwa ajili ya funzo?

3 Mfikirie Mwanafunzi: Yesu alijua kwamba ili kupata matokeo mazuri wakati wa kufundisha ni muhimu kuwafikiria wasikilizaji. Yesu aliulizwa swali hili angalau mara mbili: “Nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” Kila mara Yesu alijibu kwa njia tofauti. (Luka 10:25-28; 18:18-20) Tunapotayarisha funzo tunapaswa kufikiria mambo ambayo mwanafunzi anahitaji kujua. Tutasoma pamoja naye maandiko gani yasiyonukuliwa? Tutajaribu kujifunza habari nyingi kiasi gani? Ni mambo gani katika somo ambayo huenda mwanafunzi akaona kuwa vigumu kuyaelewa au kuyaamini? Tukijaribu kuwazia maswali ambayo huenda mwanafunzi akauliza, tutaweza kumjibu vizuri zaidi.

4. Kutayarisha funzo vizuri kunahusisha nini?

4 Pitia Habari Kabla ya Funzo: Huenda tumejifunza habari zilizo katika somo mara nyingi, lakini itakuwa mara ya kwanza kujifunza habari hizo pamoja na mwanafunzi huyu. Ili tuufikie moyo wake, ni lazima tujitayarishe vizuri kabla ya kila kipindi cha funzo. Jambo hilo linamaanisha kwamba tunafanya yaleyale ambayo tunamtia moyo mwanafunzi wetu afanye. Inatubidi kupitia habari za funzo na kusoma maandiko yasiyonukuliwa, huku tukimfikiria mwanafunzi. Inafaa pia kupiga mstari chini ya mambo muhimu.—Rom. 2:21, 22.

5. Tunaweza kumwiga Yehova jinsi gani?

5 Yehova anajali sana maendeleo ya kila mwanafunzi wa Biblia. (2 Pet. 3:9) Tunapotenga wakati ili kujitayarisha kwa ajili ya kila kipindi cha funzo, tunaonyesha kwamba tunamjali mwanafunzi wa Biblia kama Yehova anavyomjali.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki