Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/93 uku. 1
  • Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Jitayarishe Vizuri Kufundisha
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 10/93 uku. 1

Kuongoza Funzo la Biblia Nyumbani

1 Funzo la Biblia nyumbani lenye matokeo huongozwaje? Tuna kielelezo gani cha msingi? Maandiko katika habari ya funzo yaweza kuzungumzwaje? Ni nani anayepaswa kusoma mafungu? Kuongezea ule utaratibu wa msingi wa kuongoza funzo, ni nini zaidi linalohitajiwa ili kusaidia mwanafunzi aifanye kweli iwe yake mwenyewe? Ni matanzi gani ambayo lazima yaepukwe?

2 Jinsi ya Kuongoza Funzo: Kwa kawaida, funzo la Biblia nyumbani hufuata kigezo cha Funzo la Kitabu la Kutaniko. Kwanza, fungu litakalozungumzwa husomwa. Halafu yule anayeongoza funzo huuliza swali lililochapwa la fungu hilo na kumruhusu mwanafunzi ajibu. Ikiwa mwanafunzi asita, kiongozi apaswa awe tayari kuuliza maswali yenye kudokeza yatakayomfanya mwanafunzi asababu juu ya habari hiyo na kufikia mkataa unaofaa.

3 Fikiria jinsi maandiko yanavyotumika kwenye habari katika fungu. Mwonyeshe mwanafunzi jinsi ya kutambua maandiko yaliyonukuliwa na kusababu naye juu ya jinsi yatumikavyo. Ikiwa maandiko yaonyeshwa bila kunukuliwa, ni vyema kuyachunguza katika Biblia, maadamu si marefu mno. Halafu mruhusu mwanafunzi ayasome na aeleze jinsi yanavyounga mkono au kuelewesha yale yaliyoonyeshwa katika fungu.

4 Msaidie Mwanafunzi Afanye Kweli Iwe Yake Mwenyewe: Watie moyo wanafunzi wajitayarishe vyema kwa ajili ya funzo. Kazia kwamba ni muhimu kusoma ili kujifunza. Kadiri mwanafunzi anavyosoma na kutafakari habari zaidi ya funzo, ndivyo ilivyo bora zaidi. Viongozi fulani huwataka wanafunzi wasome mafungu yote wakati wa funzo la Biblia. Wengine husoma mafungu kwa zamu pamoja na mwanafunzi. Uamuzi mzuri wapaswa kufanywa, kwa kukumbuka maendeleo ya kiroho ya mwanafunzi.

5 Huenda kuzungumzia habari ya funzo kwa njia ya usomi kukamsaidia mwanafunzi apate ujuzi, lakini je, yeye aamini yale anayojifunza? Ikiwa atafanya kweli iwe yake mwenyewe, ni lazima aone jinsi habari hiyo inavyomwathiri kibinafsi. Yeye ayaonaje yale anayojifunza? Yeye aweza kutumiaje yale aliyojifunza? Tumia maswali kama hayo ili kufikia moyo wa mwanafunzi.

6 Epuka Matanzi: Kuna matanzi ya kuepuka tunapoongoza funzo la Biblia. Habari inapotokea isiyohusiana na habari inayozungumzwa, kwa kawaida ni bora zaidi kuizungumzia mwishoni mwa funzo au katika pindi nyingine. Pia, ni jambo la maana mwanafunzi atoe majibu kwa maneno yake mwenyewe badala ya kuyasoma kutoka kwenye kitabu. Hilo litasaidia kiongozi kuamua kama mwanafunzi aelewa habari hiyo.

7 Kwa nini usifanye mradi wako uwe kuongoza angalau funzo moja la Biblia? Si jambo gumu ukimtegemea Yehova na kufuata utaratibu wa msingi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko. Kuongoza funzo la Biblia nyumbani ndiyo njia yenye matokeo zaidi ya kufundisha wengine kweli na kufanya wanafunzi. Kwa kufanya hivyo, wewe pia waweza kupata shangwe inayotokana na kuwa na ushiriki kamili katika kutimiza amri ya Yesu kwenye Mathayo 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki