Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba
Juma Linaloanza Desemba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 20: “Wasaidie Wengine Wajifunze Juu ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Toa wonyesho katika fungu la 2 (na mhubiri aliye na maarifa) na katika fungu la 4 (na mhubiri mchanga). Tia moyo wote watoe kitabu Mtu Mkuu Zaidi katika nyumba kwa nyumba na katika ushahidi wa vivi-hivi.
Dak. 15: “‘Ufundishaji wa Kimungu’ Mkusanyiko wa Kimataifa—Nairobi.” Hotuba, na ushirika wa wasikilizaji. Shughulikia mipango na matangazo yoyote ya mwisho ya kutaniko kwa ajili ya mkusanyiko.
Wimbo 169 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu, ripoti ya hesabu, na shukrani za upaji wa hiari. Pongeza kutaniko kwa utegemezaji wenye ukarimu wa mahitaji ya kwenu, na kazi ya ulimwenguni pote ya Sosaiti. Dokeza jambo moja au mawili ya kuzungumzia ambayo yaweza kutumiwa katika maelezo ya utangulizi katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Wakati wa Desemba.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Unaposhughulikia fungu la 4, toa wonyesho wa jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia kwenye ziara ya kurudia. Tia moyo kila mtu aongoze funzo la Biblia kila mwezi, ikiwezekana.
Dak. 15: “Weka Kando Wakati kwa Ajili ya Utendaji wa Magazeti.” Hotuba, na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Unaposhughulikia fungu la 3, toa kielezi cha jinsi magazeti tofauti-tofauti ya karibuni yanavyoweza kutolewa watu aina tofauti-tofauti ambao waweza kupatikana katika eneo la mahali penu.
Wimbo 165 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 20
Dak. 7: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia.” Maswali na majibu pamoja na wonyesho. Kazia jambo la kwamba wote katika kutaniko wapaswa kufanyia kazi kusitawisha ustadi wa kufundisha. Baada ya kuangalia fungu la 3, mhubiri aonyesha jinsi ya kusababu na mwanafunzi wa Biblia kwa kutumia maswali na maandiko kutoka mafungu ya 13 na 14 katika sura ya 1 ya kitabu Kuishi Milele.
Dak. 8: “Kueneza Manufaa za Shule ya Mazoezi ya Kihuduma.” Hotuba ikitolewa na mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.
Dak. 15: “Kitabu-Mwaka—Hazina Yenye Kitia-Moyo.” Hotuba yenye idili ikikazia kutumiwa kwa maandiko yaliyowekwa bila manukuu. Pangia wahubiri waliojitayarisha vizuri waeleze wakiwa na hisia jambo lililoonwa katika makala hiyo na mambo yaliyoonwa yanayopatikana kwenye ukurasa wa 32 wa matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya Januari 1, 1990 (Kiingereza), Januari 1, 1987, na Januari 1, 1986. Wakumbushe wote kwamba Kitabu-Mwaka cha 1994 cha Kiswahili kina historia ya kazi katika Afrika Mashariki.
Wimbo 61 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Toa wonyesho wa jinsi ya kutumia fasihi ambayo itatolewa mahali penu katika Januari.
Dak. 15: Kuna Ubaya Gani Katika Kujaribu Dawa za Kulevya? Wahubiri wawili matineja waongea na mzee juu ya kuenea kwa utumizi wa dawa za kulevya shuleni. Wanataja kwamba vijana wengine hawaoni ubaya wa kutumia dawa za kulevya pindi kwa pindi. Mzee akubali kwamba mambo yamebadilika sana tangu awe shuleni. Aonyesha kwamba dawa za kulevya hazitajwi mahususi katika Biblia, lakini miongozo mizuri yapatikana katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 56-62. Vijana wasoma maandiko, na mzee asababu nao juu ya habari hiyo inaposhughulikiwa. Vijana watoa madokezo yao wenyewe ya njia mbalimbali ambazo zaweza kuwasaidia wakiwa mmoja-mmoja wakinze msongo wa marika.
Dak. 20: “Upanuzi Wenye Kuendelea Waongeza Uhitaji wa Majumba ya Ufalme.” Pitio la maswali na majibu la nyongeza. Kazia sababu kwa nini wazee wahitaji kuwasiliana na Halmashauri ya Ujenzi ya Kimkoa mwanzoni wanapofikiria mradi wa ujenzi wa Jumba la Ufalme.
Wimbo 120 na sala ya kumalizia.