Kitabu-Mwaka—Hazina Yenye Kitia-Moyo
1 Ripoti na mambo yaliyoonwa kuhusu kazi za Yehova za ajabu zimekuwa zikiburudisha watumishi wa Mungu sikuzote. (Ayu. 38:4, 7; Mit. 25:25; Lk. 7:22; Mdo. 15:31) Ndio sababu Kitabu-Mwaka cha Mashahidi wa Yehova ni hazina ya kitia-moyo.
2 Kila Kitabu-Mwaka hutoa ripoti zenye kujenga kutoka ulimwenguni pote juu ya utendaji na matimizo ya Mashahidi wa Yehova. Mambo yaliyoonwa ya kutia imani nguvu yaonyesha mwongozo, ulinzi, na baraka za Yehova kwa watu wake. Kitabu-Mwaka chaeleza juu ya wanaume na wanawake waaminifu ambao waliacha familia, marafiki, na nchi za kwao ili kuleta kweli za Biblia kwa watu wa mabara yote na karibu visiwa vyote vya bahari.
3 Kitabu-Mwaka kimesukuma wasomaji wengi kuongeza utumishi wao kwa Mungu. Msomaji mmoja aliandika hivi: “Siwezi kukisoma kwa mwendo wa kasi vya kutosha. Yale ambayo nimesoma kufikia sasa yamekuwa yenye kutia moyo sana. Hunifanya nihisi kwamba naweza kufanya zaidi katika kuhubiri habari njema ninapoona wengine wakifanya hivyo wakiwa na msongo.”
4 Kila mwaka tangu 1927, Kitabu-Mwaka cha Mashahidi wa Yehova kimekuwa hazina kwelikweli ya ripoti na mambo yaliyoonwa yenye kuchochea. Je! unanufaika kikamili na chanzo cha kitia-moyo hiki kisicho na kifani? Ili kufanya hivyo, hakikisha unasoma Kitabu-Mwaka mara unapokipata. Kisha katika mwaka wote, pitia sehemu mahususi zacho kwa ajili ya kitia-moyo ambacho wewe na familia yako mwahitaji.