Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • it kur. 861-862
  • Kusamehe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusamehe
  • Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova—Mfano Bora wa Kusamehe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Je, Wewe Husamehe Kama Afanyavyo Yehova?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Je, Mungu Atanisamehe?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Yehova, Mungu Aliye “Tayari Kusamehe”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Ufahamu wa Kina wa Maandiko
it kur. 861-862

KUSAMEHE

Tendo la kumwia radhi aliyekosea; kutokuwa na kinyongo kumwelekea kwa sababu ya kosa lake na kuacha kulipiza kisasi. Neno la Kiebrania sa·lachʹ (samehe) linatumiwa tu kuhusiana na Mungu kumsamehe mtenda dhambi. Neno la Kigiriki a·phiʹe·mi kihalisi linamaanisha “kuacha kabisa.”​—Ona SAMEHE.

Kulingana na sheria ambayo Mungu aliwapa watu wa taifa la Israeli, ili mtu aliyemtendea dhambi Mungu au mwanadamu mwenzake asamehewe, alipaswa kwanza kurekebisha kosa lake kama Sheria ilivyoagiza kisha, katika visa vingi, angemtolea Yehova dhabihu ya damu. (Law 5:5-6:7) Ndiyo sababu Paulo alitaja kanuni hii: “Ndiyo, kulingana na Sheria karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na hakuna msamaha unaopatikana bila kumwaga damu.” (Ebr 9:22) Hata hivyo, kwa kweli damu ya dhabihu za wanyama haingeweza kuondoa dhambi na kumwezesha mtu kuwa na dhamiri safi kabisa. (Ebr 10:1-4; 9:9, 13, 14) Kinyume chake, agano jipya lililotabiriwa liliwawezesha watu kusamehewa kikweli, kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo. (Yer 31:33, 34; Mt 26:28; 1Ko 11:25; Efe 1:7) Hata alipokuwa duniani, Yesu, alionyesha alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi alipomponya mtu aliyepooza.​—Mt 9:2-7.

Yehova husamehe “kwa njia kubwa,” kama inavyoonyeshwa na mfano wa Yesu kuhusu mwana mpotevu na mfano wa mfalme aliyemsamehe mtumwa wake deni la talanta 10,000 (dinari 60,000,000, au dola 40,000,000 hivi), lakini mtumwa huyo hakutaka kumsamehe mtumwa mwenzake deni la dinari mia moja tu (dola 70 hivi). (Isa 55:7; Lu 15:11-32; Mt 18:23-25) Hata hivyo, msamaha wa Yehova hautegemei hisia, kwa sababu hakosi kuwaadhibu watu wanaotenda dhambi. (Zb 99:8) Yoshua aliwaonya Waisraeli kwamba Yehova hangesamehe uasi imani wao.​—Yos 24:19, 20; linganisha Isa 2:6-9.

Mungu ameweka utaratibu wa kutafuta na kupata msamaha wake. Lazima mtu akubali dhambi yake, atambue kwamba amemkosea Mungu, atubu bila masharti, ahuzunike kutoka moyoni kwa kosa alilofanya, na aazimie kugeuka na kuacha kabisa mwenendo au zoea hilo. (Zb 32:5; 51:4; 1Yo 1:8, 9; 2Ko 7:8-11) Lazima afanye yote awezayo ili kurekebisha kosa au madhara aliyosababisha. (Mt 5:23, 24) Kisha lazima asali kwa Mungu, akiomba msamaha kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Kristo.​—Efe 1:7; ona TOBA.

Isitoshe, ni takwa la Kikristo kuwasamehe wengine wanapotukosea, haidhuru wametukosea mara ngapi. (Lu 17:3, 4; Efe 4:32; Kol 3:13) Mungu hawezi kuwasamehe wale wanaokataa kuwasamehe wengine. (Mt 6:14, 15) Lakini hata “mtu mwovu” aliyetengwa kutoka katika kutaniko la Kikristo kwa sababu ya kutenda dhambi nzito, anaweza kusamehewa baada ya muda akithibitisha kwamba ametubu kikweli. Wakati huo, wote kutanikoni wanaweza kumthibitishia upendo wao. (1Ko 5:13; 2Ko 2:6-11) Hata hivyo, Wakristo hawapaswi kuwasamehe wale wanaozoea kutenda dhambi kimakusudi kwa nia ya kuwadhuru wengine na bila kutubu. Watu hao wanakuwa adui za Mungu.​—Ebr 10:26-31; Zb 139:21, 22.

Ni jambo linalofaa kusali kwa Mungu tukimwomba msamaha kwa niaba ya wengine, hata kwa niaba ya kutaniko zima. Musa alifanya hivyo kwa niaba ya taifa la Israeli, alikiri dhambi za taifa zima na akaomba msamaha, Yehova alimsikiliza. (Hes 14:19, 20) Pia, hekalu lilipokuwa likiwekwa wakfu, Sulemani alimwomba Yehova awasamehe watu wake ikiwa wangetenda dhambi na baadaye kutubu. (1Fa 8:30, 33-40, 46-52) Ezra aliwawakilisha Wayahudi waliorudishwa kwa kutubu hadharani dhambi zao. Alisali na kusihi kutoka moyoni hivi kwamba watu wakachochewa kuchukua hatua ili Yehova awasamehe. (Ezr 9:13-10:4, 10-19, 44) Yakobo alimhimiza mtu aliye mgonjwa kiroho awaite wazee wa kutaniko ili wasali kwa ajili yake, na “ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.” (Yak 5:14-16) Hata hivyo, kuna “dhambi ambayo huleta kifo,” dhambi dhidi ya roho takatifu, kuzoea kutenda dhambi kimakusudi, dhambi hiyo haina msamaha. Mkristo hapaswi kusali kwa ajili ya wale wanaotenda dhambi hiyo.​—1Yo 5:16; Mt 12:31; Ebr 10:26, 27; ona DHAMBI, I; ROHO.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki