YEHOVA-SHALOMU
(Yehova-shalomu) [Yehova Ni Amani].
Jina lililopewa madhabahu ambayo Gideoni alijenga huko Ofra, magharibi ya Yordani. Baada ya kumwona malaika wa Yehova, Gideoni aliogopa kwamba atakufa. Lakini alihakikishiwa hivi: “Uwe na amani. Usiogope; hutakufa.” Kwa shukrani, Gideoni alijenga madhabahu hiyo, si kwa ajili ya kutoa dhabihu bali ili iwe ukumbusho kwa Yehova.—Amu 6:22-24.