Kufundisha Mwalimu na Darasa
“Siku moja nilipata simu kutoka kwa mwalimu wa mwana wangu,” anaripoti mmoja wa Mashahidi wa Yehova, anayeishi Ohio, (U.S.A.) “Katika mazungumzo alisema kwamba alitaka mimi niende shuleni upesi iwezekanavyo, kwa sababu mwana wangu wa miaka minane ‘alikuwa akivuruga shule yote.’ Nilipofika, niliambiwa kwamba mwanangu alikuwa akiwaambia wanadarasa wenzake kwamba jina la Mungu ni Yehova. Kwa hiyo nikamweleza mwalimu huyo kwa sababu gani Mungu ana jina, namna linavyotajwa zaidi ya mara 6,000 katika Maandiko ya Kiebrania, na nikamalizia kwa kumsomea Zaburi 83:18. Tangu wakati huo mwalimu huyo amemwuliza mwanangu maulizo mengi juu ya imani za Kikristo.”