Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 6/1 uku. 264
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Thamini Ifaavyo Zawadi Yako ya Uhai
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kuuthamini Utakatifu wa Uhai na Damu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kwa Nini Ni Lazima Tuwe Watakatifu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Heshima ya Kimungu ya Damu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 6/1 uku. 264

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Nini “mwosho uliotuleta kwenye uzima” unaosemwa katika Tito 3:5, NW?​—U.S.A.

Mtume Paulo alikuwa akiwataja wale ambao wakawa Wakristo waliotiwa matuta na roho ya Mungu, alipoandika: “Fadhili na upendo wa mwanadamu kwa upande wa Mwokozi wetu, Mungu, ilidhihirishwa, si kwa sababu ya kazi zo zote zenye haki tulizozitenda, lakini kwa sababu ya rehema yake alituokoa kupitia kwa mwosho uliotuleta kwenye uzima na kwa kutufanya wapya kwa roho takatifu.”​—Tito 3:4, 5, NW.

Usemi “mwosho uliotuleta kwenye uzima” waweza vile vile kutafsiriwa “mwosho wa kuzaliwa mara ya pili.” Kwa hiyo, mwosho huu lazima uwe ni kusafishwa kunakoongoza kwenye kuzaliwa mara ya pili. Njia ambayo kwayo kusafishwa huku kunatukia inaonyeshwa katika 1 Yohana 1:7: “Damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.” Na, ukimtaja Yesu Kristo, Ufunuo 1:5 unasema: “Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake.” Kwamba kusafishwa huku kutoka kwa dhambi kunaleta maisha mapya inahakikishwa na maneno ya Waefeso 2:1, NW: “Ndio ninyi ambao Mungu aliwafufua ijapokuwa mlikuwa wafu katika makosa yenu na dhambi zenu.”​—Tazama vile vile Waefeso 2:4, 5 na Wakolosai 2:13, 14.

Bila shaka, kusafishwa kunakoletwa kupitia kwa damu ya Yesu si kwa Wakristo waliotiwa mafuta na roho ya Mungu peke yao. Si wao peke yao wanaofaidika kutokana na wonyesho wa fadhili ya Mungu na upendo kwa mwanadamu kwa kumtoa Mwanawe. Mtume aliyetiwa mafuta Yohana aliandika hivi juu ya Yesu Kristo: “Ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” (1 Yohana 2:1, 2) Kwa kupatana na hilo Ufunuo 7:9, 14 unaonyesha “mkutano mkubwa” ambao “wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Hivyo kwa sababu ya damu ya Yesu huu “mkutano mkubwa” waweza kupata hali safi mbele za Yehova Mungu. Lakini, kama inavyoonekana katika maneno yanayozunguka ya Tito sura ya 3, si wao wanaotajwa kama wakipata ‘mwosho ambao unaleta uzima.’

Uhakika wa kwamba ‘mwosho ambao unaleta kwenye uzima unatajwa mbele ya ‘kufanywa upya na roho takatifu’ unaonyesha kwamba mwosho huu unatangulia kuzaliwa na roho. Ili mtu achaguliwe kama mwana wa kiroho wa Mungu, lazima kwanza atetewe au kutangazwa mwenye haki, yaani, lazima ahesabiwe mwana mkamilifu wa kibinadamu. Hii ni kwa maana Yehova Mungu, akiwa mkamilifu na mtakatifu, hawezi kumkubali ye yote mchafu kama mwana. Lakini, kwa sababu ya damu ya Yesu iliyomwagwa, yeye anaweza kuwatetea wanadamu wenye dhambi. Ni kama vile mtume Paulo anavyosema: “Wale walio katika umoja na Kristo Yesu hawana laana. Kwa maana sheria ya roho hiyo inayotoa uzima katika umoja na Kristo Yesu imewaweka huru na sheria ya dhambi na ya mauti.”​—Rum. 8:1, 2, 33, NW.

Hivyo yaweza kuonekana kwamba Yehova Mungu anawasafisha au ‘anawaosha’ wale ambao analeta katika ujamaa au wana. Yeye ‘anawaosha’ katika damu ya Mwanawe, akiutumia kwa ajili yao ustahili wa dhabihu ya ukombozi ya Yesu. Kupitia kwa “mwosho” huu unaowafanya watetewe, wanapata cheo cha wana wakamilifu wa kibinadamu. Hii inawaweka katika hali ya ‘kufanywa wapya kupitia kwa roho takatifu,’ yaani, kuwa wana wa Mungu waliozaliwa na roho. Wanakuwa “kiumbe kipya.”​—2 Kor. 5:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki