Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 8/1 kur. 345-347
  • Je! Wewe Utatendaje Utakapopatwa na Mkazo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Utatendaje Utakapopatwa na Mkazo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UPINZANI KUTOKA JAMAA YA MTU
  • VISHAWISHI VYA UWEKEVU WA MALI
  • KUJIEPUSHA NA NJIA YA UFISADI YA MAISHA
  • Je, Vijana Wenzako Wanaweza Kukuathiri Sana?
    Amkeni!—2002
  • Msongo wa Marika na Pendeleo Lako la Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Vijana—Msikubali Kusongwa na Marafiki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Jinsi ya Kuepuka Kushinikizwa na Marafiki
    Amkeni!—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 8/1 kur. 345-347

Je! Wewe Utatendaje Utakapopatwa na Mkazo?

KILA mwaka makumi ya maelfu ya watu wanajifunza juu ya Yehova Mungu na kuanza kumwabudu yeye pamoja na watu wake waliotengenezwa. Mara nyingi wanapatwa na upinzani na mkazo waridhiane na wanaowapinga tangu mwanzo wa ushirika wao na mashahidi wa Yehova.

Je! haya ndiyo yaliyokupata? Ikiwa ndivyo, usishangae. Yesu mwenyewe alipingwa kwa sababu ya uaminifu wake kwa kweli ya Mungu naye akawaonya wafuasi wake: “Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi.”​—Yohana 15:20.

Je! wewe utatendaje utakapopatwa na mkazo huu wa kukuondosha katika ibada ya kweli? Je! utavunjika moyo? Au kwako itakuwa kama ilivyokuwa kwa Wakristo wa karne ya kwanza kwamba “tukiudhiwa twastahimili”?​—1 Kor. 4:12.

Mbele ya kujibu ulizo hilo angalia ni nani hasa anayeleta mkazo. Petro wa Kwanza 5:8 anatusihi: “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Kama “mkuu wa ulimwengu” wa wanadamu, “mungu wa hii taratibu ya mambo” na “mtawala wa mashetani,” Shetani aweza kuongoza watu kwa hila na hali kusudi apapige mahali pa mtu palipo dhaifu zaidi. (Yohana 14:30; 2 Kor. 4:4; Mt. 12:24, NW) Aweza kuelekeza jamaa ya mtu, marafiki au wasiri wajitahidi sana kumlazimisha mtu aache kushirikiana na mashahidi wa Yehova.

Mara nyingi maarifa ya Shetani ni matusi ya maneno. Je! wafanya kazi wenzako, wanashule wenzako au washiriki wengine wameanza kukufanyia mzaha au kukutukana? Usishangae. Kumbuka kwamba umeanza kujiepusha na desturi za watu wengi na mazoea yasiyopatana na Maandiko. Matokeo ambayo hili lingekuwa nayo juu ya wengine wa washiriki wako yaonyeshwa katika 1 Petro 4:4: “Mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.”

Hata hivyo, uwe mwangalifu usije ‘ukalipa ovu kwa ovu.’ (Rum. 12:17) Yesu, ambaye mwenyewe ‘aliyastahimili mapingamizi makuu . . . ya watendao dhambi,’ alishauri: “Endeleeni . . . kuwabariki wale wawalaanio, kuwaombea wale wawatukanao.” (Ebr. 12:3; Luka 6:27, 28, NW) Njia hiyo ya kutenda mtu anapotukanwa kwa maneno mara nyingi imegeuza moyo wa wapinzani.

UPINZANI KUTOKA JAMAA YA MTU

Maarifa mengine ya mkazo ni upinzani wa jamaa. Yesu alitangulia kuwaonya wafuasi wake watazamie hili. (Mt. 10:35, 36) Huenda washiriki wa jamaa yako wakalalamika kwamba kujifunza kwako Biblia kumeleta wasiwasi nyumbani na kwamba kama wewe ‘unawapenda kweli’ ungeacha. Wengine wameshindwa na namna hii ya mkazo, wakiwaza kwamba lingekuwa jambo bora kuacha kujifunza Biblia kwa muda wakitumaini kwamba nyumaye mambo yatatengenezwa.

Lakini je! kuwaza huko kwafaa? Je! lo lote laweza kutengenezwa kwa kuacha funzo la Biblia, ambayo ndiyo kitu kile kile ‘kilichoongozwa na roho ya Mungu na chenye faida . . . kwa kutengeneza mambo’? (2 Tim. 3:16, NW) Ni afadhali kulitii shauri lililomo katika Wagalatia 6:9: “Tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.” Na ‘utakachovuna’ chaweza sana kuwa furaha ya kuona washiriki wa jamaa yako wakiikubali kweli kwa sababu ya mfano wako imara. Shahidi wa Yehova anasimulia namna hili lilivyotukia kuwa kweli kwa habari yake:

“Karibu kuanzia mwanzoni mume wangu alipinga kuhudhuria kwangu mafunzo ya Biblia ya kundi . . . Nilijaribu mara nyingi kujadiliana naye, na hata nikamkaribisha kwenye mikutano akajionee mwenyewe umuhimu wa mambo yanayozungumzwa huko, lakini ilikuwa kazi bure.” Upinzani wake ukaongezeka kutoka vitisho vya maneno kuwa mapigo. “Lakini hata hilo halikuigeuza nia yangu,” alieleza mwanamke huyu. Nini yaliyokuwa matokeo ya ‘kutochoshwa’ kwa mwanamke huyu na ibada ya Yehova? Mumewe alianza kuhudhuria mikutano ya mashahidi wa Yehova ‘achunguze.’ Alipendezwa na aliyoyasikia, akazungumza na dada yake juu yake naye, vile vile, akaanza kwenda penye Jumba la Ufalme. Muda mfupi kufuata hapo mume yule na dada yake walibatizwa kwenye kusanyiko moja wote wawili. Lo! ni matokeo mazuri namna gani! Na haya yote kwa sababu mke wa Kikristo alikataa asishindwe na mkazo wa upinzani wa jamaa.

VISHAWISHI VYA UWEKEVU WA MALI

Je! wewe utatendaje mkazo ukiwa ni juu ya uwekevu wa mali? Pengine wakati ule ule ambapo umekuwa tayari kukata maneno uyatoe maisha yako kwa Yehova inatukia kwamba utapandishwa cheo katika kazi yako ya kimwili. Huenda ikatia ndani na ongezeko la mshahara lenye kushawishi na/au faida nyingine za kimwili. Bila shaka, mambo haya yenyewe si mabaya. Lakini je! yatatia ndani na madaraka zaidi au saa za ziada kazini? Je! hii itakatiza wakati uliowekwa kando kwa ajili ya funzo la kipekee la Biblia, kuhudhuria mikutano ya Kikristo na utendaji wa kuuhubiri Ufalme?

Jiulize mwenyewe, Kwa nini toleo hilo linakuja wakati huu? Ni nani hasa ambaye angefurahia kuuza kwangu wakati niliokwisha ‘kuukomboa’ kwa ajili ya ibada ya Yehova Mungu kwa faida za kimwili? (Efe. 5:16; Kol. 4:5) Kumbuka kwamba Ibilisi anadai wewe unapendezwa na amana yako ya mali zaidi kuliko ibada ya Mungu, na kwamba mambo yakiwa magumu utamwacha Yehova. Yeye alifanya dai hilo kwa habari ya mtumishi wa Mungu Ayubu. Lakini, ajapokuwa alinyang’anywa jamaa, marafiki na mali, Ayubu alikataa asishindwe na maarifa hayo yenye mkazo. Hivyo aliyahakikisha mashtaka ya Shetani kuwa ya uongo. Kwa sababu ya ustahimilivu wa uaminifu akiwa chini ya mkazo Yehova “akaubarikia huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake.” Je! tendo lako juu ya mkazo wa uwekevu wa mali litakuwa kama lile la Ayubu? Ikiwa ndivyo waweza kuwa na uhakika wa kupata thawabu inayolingana.​—Ayubu sura ya 1 na ya 2; 42:12.

KUJIEPUSHA NA NJIA YA UFISADI YA MAISHA

Inayoitwa leo “adili mpya” ni jambo jingine lenye mkazo kwa watu wanaotaka kuzipatanisha maisha zao na mafundisho ya Biblia. Kwa mfano, katika sehemu nyingine ni jambo la kawaida kwa mwanamume na mwanamke kuishi pamoja, hata kukuza jamaa, wajapokuwa hawajaoana.

Wakati watu kama hao wanapokubali kujifunza Biblia na mashahidi wa Yehova wanajifunza kwamba Mungu anahesabu ukamatano huo wa kuridhiana kwa watu wawili lakini bila ya kuandikishwa kisheria kama uasherati. Neno la Yehova linashauri: “Ukimbieni uasherati.” (1 Kor. 6:18, NW) Watu mmoja mmoja walio wanyenyekevu wanaitii amri hiyo nao wanapokea baraka nyingi kwa kufanya hivyo.

Kweli ya Biblia ilipouvuta moyo wa mwanamke mmoja katika Surinam aliamua kumwacha mwenzi wake wa kuridhiana naye ambaye alikuwa ameishi naye miaka mitano, akimzalia hesabu fulani ya watoto. Mwanamume mwenyewe alikasirika sana, akampiga mwanamke huyu, na hata akatisha kumwua kama angemwacha. Hata hivyo yeye alifanya hivyo. Matokeo? Anasema: “Mimi mwenyewe nakiri kwamba furaha niliyo nayo wakati huu na watoto wangu inayapita kwa mbali magumu tuliyopata.”

Kwa kweli, kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova tukiwa chini ya mkazo ndilo jambo la busara la kufanya peke yake. Kwaonyesha upendo kwa Mungu na jirani, kwamhakikisha Ibilisi kuwa mwongo, kwahakikisha ulinzi na baraka ya Yehova na hata kwaweza kuwasaidia wale walio karibu nawe waichunguze kweli kwa makini. Kwa sababu ya hili, je! wewe utatendaje utakapopatwa na mkazo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki