Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 2/15 kur. 93-94
  • Daraka la Wale Ambao Wanatoa Shauri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Daraka la Wale Ambao Wanatoa Shauri
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UJUZI NI WA MAANA KWA SHAURI LENYE HEKIMA
  • ‘Sikiliza Maneno ya Wenye Hekima’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Washauri Wastadi—Baraka kwa Ndugu Zao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Usipinge Shauri la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Je, Shauri Unalotoa “Huufanya Moyo Ushangilie”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 2/15 kur. 93-94

Daraka la Wale Ambao Wanatoa Shauri

SHAURI lenye hekima lina ubora mwingi. Watu, wa wakati uliopita na wa kisasa, wamekuwa wenye nia kulipa fedha kwa ajili ya shauri jema, siyo katika mambo kama vile sheria tu, lakini katika pande nyingine nyingi za maisha. Wafalme na watawala wamewapendelea sana na wakawaajiri watu wenye uwezo wa kutoa shauri lenye hekima.

Shauri lililo bora kupita yote ni lile linalokamatana na kupata kwetu njia ya uzima katika kibali cha Mungu na kushikamana nayo. Na, kama vile Israeli wa kale walivyokuwa na washauri wenye uwezo wa kuwasaidia watu, ndivyo na leo katika kundi la watu wa Mungu duniani kulivyo na wanaume wazee walio na daraka la kutoa shauri. Hii ni kwa ajili ya kuwaongoza, kuwatia nguvu na kuwalinda ndugu zao za Kikristo.​—1 Pet. 5:2, 3.

Kutoa shauri kama hilo ni pendeleo lakini vile vile daraka zito. Kushauri ni namna ya kufundisha. Nao wale wafundishao wanakuwa na daraka juu ya wanayoyafundisha na matokeo juu ya wale waliofundishwa.​—Yak. 3:1.

Shauri laweza kuwa lenye kuadhibisha, katika namna ya karipio. Mithali 25:12 inasema: “Kipuli cha dhahabu, na pambo la dhahabu safi; ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo.” Lakini, angalia kwamba inasema mwonyaji mwenye hekima. Siyo nia tu ya kutoa shauri iliyo ya maana. Huenda kijana asiye na ujuzi akawa na nia ya kushauri au kujaribu kushauri. Lakini je! anastahili? Anaposihi kusaidia ndugu ambao wanaweza kuchukua hatua ya uongo, mtume anasema: “Ninyi mlio na sifa za kiroho jaribuni kumtengeneza upya mtu huyo.” (Gal. 6:1, NW) Si wote walio na sifa hizo za kiroho. Kwa hiyo, Mungu alipomfanya Musa apange wanaume waangalie magumu kati ya Israeli wa kimwili, Musa aliamuru kwamba wawe “watu wenye akili na fahamu.” (Kum. 1:13-15) Wale wanaotumikia kama wachungaji na waangalizi katika kundi la Kikristo vivyo hivyo wanapaswa kuwa wanaume wanaoonyesha hekima ya kiroho na busara na walio na ujuzi.

UJUZI NI WA MAANA KWA SHAURI LENYE HEKIMA

Kama linatolewa kwa mtu mmoja au kwa kikundi, shauri kwa msingi ni la namna mbili: Lile linalotolewa kwa kujibu ombi la kuelimishwa au uongozi, na shauri lisiloombwa linalotolewa kwa sababu ya kulihitaji kwa wazi. Katika lo lote la haya, kuna uhitaji wa busara inayofaa.

Zaidi juu ya shauri lisiloombwa, imempasa mtu aangalie kwanza ni kwa kadiri gani linavyohitajiwa kweli. Hali yenyewe ni nzito namna gani? Kumbuka, Mafarisayo wa siku za Yesu walielekea kufanya maulizo makubwa ya mambo madogo, nyakati nyingine ya kuasi sheria yenye msingi wa kanuni za kibinadamu na si juu ya maagizo ama kanuni za Neno la Mungu. Kwa kukazia mambo madogo kwa upande mmoja, waliyaficha mambo yaliyo mazito zaidi ya Neno la Mungu. (Marko 7:1-9, 14, 15, 20-23; Mt. 23:23) Vile vile, angalia kama hali na wakati vinafaa kwa kutoa shauri hilo lisiloombwa. Kumbuka, “Neno linenwalo wakati wa kufaa, ni kama machungwa katika vyano vya fedha.”​—Mit. 25:11.

Kwa namna zote mbili za shauri, lililoombwa na lisiloombwa, mshauri mwenye hekima anatafuta ujuzi​—anataka kuhakikisha ameyafahamu vya kutosha mambo yaliyomo kusudi atoe shauri la haki, lenye msingi imara​—siyo lenye mashaka tu au lisilofahamika vizuri. (Mit. 9:9; 18:17) Yeye hawi mwepesi wa kudanganyika ama mjinga. (Mit. 14:15) Anasikiliza vyema, ni “mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema,” kwa maana “yeye ajibuye kabla hajasikia [yaani, mbele ya kusikia maneno yote na kupata maana yake], ni upumbavu na aibu kwake.” (Yak. 1:19; Mit. 18:13; tazama vile vile 29:20.) Kupendezwa huku na habari zote ni kwa maana ikiwa ataonyesha wazi ufahamu wa kweli na busara katika kushughulikia ulizo lo lote au ugumu.​—Mit. 15:14; 18:15.

Ni ambapo mtu mwenye hekima anapopata busara hiyo tu​—kwa habari ya hali za msingi, na sababu za ugumu​—kwamba ‘anapokea maarifa,’ yaani, sasa anajua namna atakavyokata maneno na shauri atakalotoa. (Mit. 21:11) Ijapokuwa huenda hili lichukue wakati, linaleta faida zaidi. Wakati mshauri anapoonyesha ufahamu wa mambo ya hakika, maoni yaliyosawazika ya mambo, ufahamu wa ugumu wa mtu na hali zinazoshiriki kuuleta, yule anayeshauriwa inaelekea sana atalipokea shauri linalotolewa. Ndiyo, kwa maana atajua kwamba mshauri anayo mapendezi ya kutoka moyoni katika kutoa msaada wenye ufahamu​—yeye hasemi tu asiyoyafahamu, akizungumza kwa juujuu au akiachilia mbali mambo ambayo huenda yakatofautisha kisa cha mtu huyu na kile cha wengine wenye ugumu unaofanana na huo. Haya yote yanaongeza ushawishi, ndiyo, “utamu” wenye kuvuta, kwa maneno ya mshauri.​—Mit. 16:20, 21, 23.

Bila shaka, uchunguzi huu wa habari haupaswi ufanywe kupita kadiri ama sivyo mtu asingefanikiwa wakati wo wote katika kutoa shauri. Maulizo machache huenda yakatokeza mambo ya hakika yanayohitajiwa. Na, ikiwa anaona kwamba habari fulani hazikutokea, yule anayeshauri huenda akasema: ‘Basi, juu ya msingi wa yale uliyoniambia, ningesema haya. . . . Lakini, ikiwa kuna mambo mengine ambayo hukutaja, hii yaweza kugeuza mambo.’ Haimpasi mtu kuchunguza hata kufikia kutia haya isiyohitajika. Maulizo ya waziwazi yakimaanisha shuku ya matendo ya ufisadi au maovu, mahali pasipo na sababu, huenda yakaleta majeraha mabaya yawezayo kuchukua muda mrefu kuponyeka. (Mit. 12:18) Kumbuka, uwezo wa mzee wa kushauri wapaswa kutumiwa kwa “kujenga wala si kwa kubomoa.” (2 Kor. 13:10) Vile vile ndio mwendo wa hekima kutojitia kupita kadiri katika maisha za faragha za watu.

“Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu.” (Mit. 15:28) Shauri linaloupasa ujamaa wa watu mmoja mmoja kwa Mungu linahitaji fikira hizo. Ili kufaidi, lazima shauri liwe la hakika, na hiyo yamaanisha lazima liwe linapatana na Neno la Mungu. Maulizo juu ya ndoa, talaka, kutokuwamo kwa Mkristo na mambo mazito mengineyo yakijibiwa isivyofaa, maumivu makubwa yaweza kutokea. Huenda maisha yote ya mtu yakapaswa kwa njia yenye kudhuru. Siyo hekima ya kibinadamu au filosofia bali hekima inayotoka kwa Washauri walio juu zaidi, Yehova Mungu na Kristo Yesu, iliyo imara, yenye kuendelea, yenye kufaidi milele.​—1 Kor. 2:4, 5; Zab. 33:11; Mit. 21:30; Isa. 9:6.

Usitilie hili shaka: Hakuna kinginecho katika maisha isipokuwa kanuni za Neno la Mungu, Biblia, kinachoweza kuongoza kikimwezesha Mkristo awe “kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” (2 Tim. 3:16, 17) Kwa hiyo, hakuna sababu wakati wo wote ya kutegemea hekima ya mtu mwenyewe katika kushauri. (Mit. 3:5-7) Kuliko kwenda upande kwa sababu ya maoni ya kipekee au maelezo, endelea kukaa ‘katikati ya njia’ kwa kukaa kabisa ndani ya mipaka ya shauri la Maandiko. (Mit. 8:20) Sala ya unyenyekevu kwa Mungu yapaswa iwe ndilo kimbilio la sikuzote la mtu anayejaribu kushauri kwa hekima.​—Yak. 1:5; 1 Fal. 3:7-12.

Washauri wa Kikristo wanaojionyesha wenyewe watiifu kwa shauri la Neno la Mungu, watakuwa baraka kweli kweli kwa ndugu zao. Zaidi ya hayo, watapendelewa na Wafalme wakuu, Yehova Mungu na Mwanawe Kristo Yesu.​—Mit. 27:9; 14:35; 16:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki