Jihadhari na Maelekeo ya Uzinzi!
MAPEMA katika mwaka wa 1972 gazeti la picha la Kiamerika lijulikanalo sana lilichapa orodha ya maulizo ya ndoa na kuwakaribisha wasomaji wake kuijaza na kuirudisha. Karibu miezi sita nyumaye lilisema kwamba lilikuwa limepokea majibu 62,000 kutoka kwa wasomaji ambao maitikio yao yalikuwa na maana ya “mateteo timamu, mara nyingi yenye shauku, nyakati nyingine ya hasira ya ndoa ya kimila.” Lakini ni jambo moja ‘kutetea ndoa ya kimila’ na tofauti kabisa kuishi kwa kulingana nayo.—Life, November 17, 1972.
Kwa mfano, alikuwako mwanamume mmoja aliyejulikana sana na kupendwa sana. Nyuma ya kutumikia kwa karibu miaka 20 kama mhudumu-msimamizi wa kundi fulani alitengwa na ushirika kama mzinzi asiyetubu. Haikuwa kana kwamba yeye alikusudia kufanya dhambi. Ni kwamba tu alipandishwa cheo katika mahali pa kazi yake ya kimwili kuwa mwenye heshima naye alitakiwa afunge safari ndefu za biashara. Katika hizi, kulikuwako kunywa na kula na kuwa na maongezi na watu wasio na mashaka juu ya kufanya uzinzi, naye alishindwa na shawishi.
Kama ilivyo kawaida katika visa kama hivyo, alimficha mkewe mambo haya na kundi la Kikristo, na kwa hiyo kwa muda aliishi kwa uongo. Yeye aliyapuza maonyo ya Maandiko kama vile: “Dhambi yenu itawapata hapana budi.” “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, . . . wengine dhambi zao [zadhihirika baadaye].” Hakuna shaka juu yake, alikuza maelekeo ya uzinzi, na nafasi ilipokuja akayatosheleza na kuendelea kufanya hivyo. Lo! msiba kama nini, sio kwake tu lakini vile vile kwa jamaa yake na kundi!—Hes. 32:23; 1 Tim. 5:24.
Kinachoshuhudia kuwako kwa maelekeo ya uzinzi kati ya wanaume ni kupendwa sana kwa magazeti fulani ya wanaume yanayoonyesha picha za wanawake walio uchi kabisa na mizaha ya mambo machafu. Gazeti moja linaposhindwa nyuma ya jingine kwa sababu ya bei zenye kupanda na ukosefu zaidi wa kupendezwa kuyasoma, yale magazeti yanayozungumza juu ya ufisadi yanazidi kuongezeka nao wanajivunia kuenezwa kwayo katika mamilioni mengi ijapokuwa bei ya juu kwa nakala.
Kwa habari ya wake wa Kiamerika, mmojawapo wa waandishi maarufu aliyeandika katika gazeti la wanawake alisema kwamba “siri isiyotolewa nje zaidi ya wake wengi wa Kiamerika ni . . . wao wanawaza wakiwa katika fahamu zao juu ya wanaume,” hivyo kwa njia ya ufisadi. Kwa kulingana naye, tabia hii haikuenea sana tu, lakini wako wengine waliomo katika utaalamu wa ugonjwa wa akili wanaokubaliana na kuwaza huko kwa mtu akiwa katika fahamu zake. Kwa kulingana na wataalamu hawa wa ugonjwa wa akili, kuwaza huko ni njia ya kuepukia uchovu au kukosa mahaba katika maisha zao. Lakini, wanaonya kwamba mawazo hayo yanaweza kuwa yenye nguvu sana na kudai hata kutisha imara ya ndoa ya mtu.
Maelekeo ya uzinzi ni matokeo ya wazazi wetu wa kwanza, kwa maana ni namna ya choyo, kuweka tamaa ya kichoyo mbele ya sheria za Mungu; kama vile Adamu na Hawa walivyofanya walipokosa.
Hakuna shaka juu yake, Muumba aliifanya tamaa ya kuoa katika wanadamu yenye nguvu sana kwamba kusingekuwa na hatari kwamba jamaa ya kibinadamu ingemalizika. Na kwa hekima na upendo yeye alifanya vile vile mwanamume na mwanamke vile vile kwamba waweze kuleteana faraja nyingi, raha na furaha.
Lakini Muumba hatoi zawadi tu, yeye anaweka masharti vile vile kwa haki na kwa hekima juu ya namna zawadi hizi zimepaswa zitumiwe. Hivyo alipanga kwamba wanadamu wahifadhiwe hai na utendaji unaopendeza wa kula na kunywa, lakini yeye hakukusudia kwamba wanadamu wawe walevi ama walafi; licha ya hayo hakukusudia kwamba waibe ama kuua kusudi wajipatie chakula walichotaka au kuhitaji. Ndiyo sababu Neno lake linakataza ulafi na ulevi, wizi na uuaji.—Zab. 104:15; Mit. 23:20; Flp. 3:19; 1 Pet. 4:15.
Ndivyo ilivyo na kwa zawadi ya Mungu ya ngono. Yeye alimwumba mwanadamu mwanamume na mwanamke, naye ndiye wa pekee aliye na haki ya kumwambia mwanadamu namna inavyopaswa zawadi hii kutumiwa. Kwa hiyo Neno lake linakataza uzinzi na uasherati. (Ebr. 13:4) Biblia haionyi tu juu dhambi hizi; inakataza vile vile maelekeo ya kufanya hayo. Hivyo Yesu alionya kwamba mwanamume aliyeoa alipoendelea kumtazama mwanamke, si kwa sababu ya kupendezwa na uzuri wake tu, lakini vile vile ili awe na tamaa ya kufanya ngono naye, tayari alikuwa anafanya uzinzi naye moyoni mwake.—Mt. 5:28.
Katika maana ile ile mtume Paulo alionya, si juu ya dhambi za uasherati na uzinzi tu, lakini vile vile juu ya uchafu wote na mwenendo mpotovu. Mambo yote hayo yangemzuia Mkristo asiupate uzima wa milele. (Gal. 5:19-21) Ufahamu wake juu ya jambo hili na fikira zake nzito juu yake vinaonekana kutokana na namna alivyomshauri rafiki yake Timotheo juu ya mambo hayo. Alimwonya Timotheo awatendee wanawake wazee kama vile ambavyo angemtendea mama yake mwenyewe, kwa heshima na fadhili, na wanawake vijana katika kundi kama dada zake mwenyewe za kimwili. Na kwa njia gani hivyo? “Katika usafi wote.” Nyumaye, alipokuwa akimwandikia Timotheo kwa mara ya pili, aliona ni muhimu kumshauri Timotheo tena juu ya jambo hili, akisema: “Zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.” Ikiwa moyo umejawa na mawazo machafu, awezaje mtu kumwita Yehova Mungu katika sala kwa moyo safi?—1 Tim. 5:2; 2 Tim. 2:22.
Maoni yenyewe ya mahaba yanapendeza kwa watu wengi waliooa au kuolewa ambao wenzi wao huenda hawaongozeki kwa wepesi, wasiowaza sana au wenye kutangulia kufanya shughuli zao. Lakini mahaba ni mtego yakiwa nje ya ndoa au yakiwa hayakusudiwi yaelekeze kwenye ndoa. Hivyo Dr. Mace, katika kitabu chake Marriage—East and West, anaeleza aliyoyasema mwanamke wa Mashariki kwa habari ya rafiki yake aliyekuwa na mapenzi nje ya ndoa: “Usinielewe vibaya tafadhali. Mimi nampenda mume wangu nami naithamini nyumba yangu wala sina kusudi la kuufuata mfano wake.” Kisha akichekelea, akaongeza, “Lakini hudhani ni jambo la mahaba kidogo?”
Kizuizi chake? Juu ya yote, kuna uhitaji wa kuulinda moyo kwa kujihadhari akili inatwaa mambo gani. (Mit. 4:23) Epuka kujifurahisha kunakokazia mwenendo usio wa Kikristo; epuka kusoma mambo kama hayo katika magazeti ama vitabu. Mahali pa kukaa katika hadithi “za mahaba,” litii onyo la mtume: “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.” Lo! hicho ni kizuizi cha kuwaza juu ya mahaba namna gani!—Flp. 4:8.
Kutokana na Neno la Mungu twajifunza kwamba urafiki huo wa mahaba haramu ni mbaya, nalo linatuambia vile vile tuyachukie yaliyo mabaya. (Zab. 97:10) Hata tusipoyageuza mawazo ya mahaba kuwa matendo yanadhuru bado. Kwa njia gani hivyo? Kwa sababu yataudhoofisha upendo wa mtu na heshima kwa mwenzi wa mtu, kumfanya mtu awe asiyejihadhari kumpendeza Muumba katika mambo mengine, kutokeza dhamiri yenye hatia na kudhoofisha bidii ya mtu kwa ajili ya haki.
Kwa kweli Neno la Mungu linaonyesha waziwazi ulipo mwendo wa hekima—siyo katika kushindwa na maoni ya ndani ya upumbavu na makusudi—bali katika kujitia wenyewe adabu, katika kufuata kanuni za haki, katika kupendezwa na sheria ya Mungu, kuitafakari na kuongozwa nayo.—Zab. 1:1-6; Mit. 2:1-9.