Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 8/1 kur. 359-360
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa Kati ya Watu wa Rangi Tofauti?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kuwekea Nyumba Yako Msingi Mzuri
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Jinsi ya Kufanikiwa Katika Ndoa ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Ndoa Inaweza Kufanikiwa Katika Ulimwengu wa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 8/1 kur. 359-360

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● N’nini maoni ya mashahidi wa Yehova juu ya ndoa kati ya watu wa mataifa mbalimbali?​—Ufaransa.

Nyakati zote mashahidi wa Yehova wanajaribu kuonyesha maoni ya Biblia juu ya mambo. Biblia haizungumzi ndoa kati ya watu wa mataifa mbalimbali waziwazi. Lakini, inaonyesha namna ambavyo Yehova anawaona wanadamu nayo inatoa kanuni za kuwaongoza wale wanaofikiria ndoa.

Ukuu wa taifa moja kupita jingine haufundishwi au kuonyeshwa po pote katika Biblia. Yehova anawakubali watu wa mataifa yote kama watumishi wake waliokubaliwa, bila ya ubaguzi. Biblia yatuambia hivi: “[Mungu] alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote, akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone.” (Matendo 17:26, 27) “Mungu hana upendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.”​—Matendo 10:34, 35.

Kwa hiyo, Biblia haionyeshi po pote kwamba tofauti za mataifa zenyewe ndizo zinazofanya ndoa iwe yenye kufaa. Juu ya ndoa ya wajane, mtume Paulo aliandika hivi: “Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.” (1 Kor. 7:39) Hivyo Mkristo yu huru kuoa au kuolewa na ye yote ambaye yu huru kufanya hivyo kulingana na Maandiko na kwa kisheria, maadamu huyo ni mwamini mwenzetu kwa kweli.

Kwa hiyo je!, kuna mambo mengine yo yote yanayostahili kuangaliwa? Ndiyo, kwa maana Wakristo wanajaribu kutumia uamuzi mzuri na hekima katika yote wayafanyayo. Kati ya mambo mengine, wanatiwa moyo ‘waenende kwa hekima mbele yao walio nje,’ wale walioko nje ya kundi la Kikristo.​—Kol. 4:5.

Katika maeneo mengi ndoa kati ya watu wa mataifa mbalimbali zinazidi kufanywa na watu wengi. Watu wanasafiri zaidi, na mara nyingi wanaziona njia na desturi za watu wa nchi nyingine kuwa za kuvuta. Vile vile, vita imeshiriki, na askari wengi wa Ulaya na Amerika ya Kaskazini wameoa wake wa Kiasia. Kwa hiyo, kuna maoni mengi kidogo kwa upande wa wengi juu ya ndoa kati ya watu wa mataifa mbalimbali.

Hata hivyo, si watu wote wanaoyashiriki maoni haya mengi, wala si wote wanaofahamu kanuni za Biblia. Maoni mengi mabaya yenye nguvu lakini yasiyo na msingi wa kweli yangali yamo katika ulimwengu wa wanadamu. Mkristo, akiwa mwenye busara, lazima apambane na maisha kama yalivyo​—si kwa namna ambavyo yeye angetaka yawe.

Katika mahali pachache, hata kuna sheria zinazokataza ndoa kati ya watu wa mataifa mbalimbali kwa kisheria. Inapokuwa hivyo, Wakristo wako chini ya wajibu wa Maandiko kuzitii, kwa maana sheria hizo hazifanyi isiwezekane wamwabudu Mungu kwa “roho na kweli.” (Yohana 4:24; Rum. 13:1) Bila shaka, ikiwa Mkristo angependa zaidi ahamie eneo ambako sheria hizo hazifikilizwi, yu huru kabisa kufanya hivyo.

Katika maeneo mengine, maoni mabaya yasiyo na msingi ya mahali yanaleta ubaguzi na dhuluma kwa wale walio wa mataifa fulani ya wanadamu. Maoni haya mabaya hayafanyi ndoa kati ya watu wa mataifa mbalimbali iwe mbaya. Hata hivyo, kwa Mkristo mwenye busara, huenda yakawa sababu ya kufikiri juu ya kufaa kwa ndoa ya namna hiyo. Bila ya kujali wenzi wametoka katika mataifa gani, ndoa yenyewe yahitaji mapatano mengi kwa upande wa watu wawili ipate kufanikiwa na kuleta furaha. Kutokukamilika kwa kibinadamu kwafanya ndoa zote zilete kadiri fulani ya “dhiki katika mwili,” kama vile mtume Paulo anavyoonyesha kwa hekima. (1 Kor. 7:28) Katika maeneo fulani, ambako maoni ya kuchukia watu wa mataifa fulani yana nguvu, hii ingeweza kuweka mkazo zaidi katika ukamatano wa ndoa na ingeweza kuwa shida zaidi kwa watoto wanaozaliwa. Kwa hiyo yampasa Mkristo afikirie sana matokeo yanayoweza kuwapo mbele ya kutumainia kuoa mtu wa taifa jingine.

Huenda watu wa mataifa mbalimbali wakawa na hali zinazolingana, kwa njia ya malezi, ya kijamii na ya elimu. Au huenda hali zao zikatofautiana. Nyakati nyingine tabia zao mbalimbali, nia na desturi zinazofuatana na hali mbalimbali zinaelekea kuufanya mwungano wa ndoa upendeze zaidi. Na hali hali zinazotofautiana sana, hata kati ya wenzi wa ndoa wa taifa moja, zaweza kutokeza magumu nazo zimefanya hivyo nyakati nyingine, zikifanya mapatano ya ndoa kuwa magumu zaidi. Katika kufanya uamuzi wake, yampasa Mkristo ayafikirie vile vile mambo haya kwa njia ifaayo​—kwa ajili ya furaha ya yule mwingine na yake mwenyewe vile vile.

Mkristo yuko chini ya wajibu wa kuwatangazia wengine habari njema za Ufalme. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Kama uhakika, basi, anaweza akafikiria kama kuoa au kuolewa na mtu wa taifa jingine kutaelekea kuifanya nia ya watu katika mtaa wake iwe mbaya sana juu ya kazi hii ya kuutangaza Ufalme. Mifano ya Kristo Yesu na mitume wake yaonyesha kwamba wao walikuwa wenye nia ya kujinyima vitu ambavyo walikuwa na haki ya kuwa navyo kuliko kuwazuia watu kwa kadiri kubwa wasiipokee kweli ya Neno la Mungu.​—Rum. 15:3; 1 Kor. 10:32, 33.

Lakini, nyuma ya kuyafikiria mambo haya yote kwa uzito, kila Mkristo atafanya uamuzi wake mwenyewe​—kwa dhamiri njema na kwa kusukumwa na upendo kwa Mungu na kwa jirani yake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki