Maswali Kutoka kwa Wasomaji
● Kwa sababu gani mashahidi wa Yehova wanajizuia wasishiriki katika maadhimisho ya Mwaka Mpya?—U.S.A.
Maadhimisho ya Mwaka Mpya yanayoshirikishwa na mwisho wa mwaka mmoja na mwanzo wa unaofuata Januari 1 yana uhusiano wa dini ya uongo. Siku ya kwanza ya Januari ilikuwa takatifu kwa mungu wa Kirumi Yanu mwenye nyuso mbili na kwa hiyo ilikuwa ya kipagani. Lakini pana sababu nyingine yenye nguvu ya kutokuwapo kwa Wakristo.
Wakristo wanaonywa hivi: “Na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati.” (Rum. 13:13) Maadhimisho ya mwaka Mpya, hata hivyo, yanakuwa mara nyingi na mazoea hayo na mambo ya kupita kiasi. Chasema hivi Standard Dictionary of Folklore, Mythology, and Legend: “Nchi nyingi za Mashariki zaonyesha kupita kwa mwaka wa zamani na kufika kwa mwaka mpya kwa dansi zenye mambo mengi, kunywa, na kwa kawaida mwenendo wa ufisadi.” Juu ya desturi zisizo za nchi za Ulaya na Amerika, kitabu kile kile chasema kwamba hizo pia ‘zinaona kwisha kwa mwaka mmoja na kuanza kwa unaofuata kama wakati wa mapendezi.’
Kuhusika kwa mtu katika mwadhimisho wa Mwaka Mpya, hata akiendeleza kujiweza, kungeweza kumaanisha kuachilia mwenendo usiozuiwa wa wengine na kukubali mazoea yenye msingi wa dini ya uongo. Kukataa kwa mashahidi wa Yehova kujitia katika maadhimisho hayo hakumaanishi hawafurahii burudisho na tafrija. Wanafurahia. Lakini wanajaribu kuendeleza dhamiri njema mbele za Mungu na wanadamu, wakiepuka mambo ya kupita kiasi na pia maelekeo ya kuadhimisha sikukuu za kipagani.