Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 10/1 kur. 435-438
  • Ni Katika Hekalu Gani Anamoweza Kupatikana Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Katika Hekalu Gani Anamoweza Kupatikana Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • HEKALU KUU LA KIROHO LA MUNGU
  • UA NA MADHABAHU YAKE
  • “PATAKATIFU SANA”
  • “PATAKATIFU”
  • KULETA UVUMBA KATIKA PATAKATIFU SANA
  • KUINGIA KWA KRISTO KATIKA PATAKATIFU SANA
  • Hekalu Kubwa la Kiroho la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Nyumba ya Sala kwa Mataifa Yote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Thamini Pendeleo Lako la Kuabudu Katika Hekalu la Kiroho la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Wakati Ibada Inapowekwa Juu ya Hekalu la Kidunia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 10/1 kur. 435-438

Ni Katika Hekalu Gani Anamoweza Kupatikana Mungu?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. Twaweza kutazamia kwa busara Mungu aturuhusu tumfikie yeye kwa njia yetu wenyewe au vyo vyote tu?

NI JAMBO la busara na inafaa kwamba Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote aonyeshe njia ya wazi ya watu wa dunia ya kumfikia yeye. Kiumbe kidogo cha kibinadamu hakiwezi kutazamia kumfikia vivi hivi bila ya ruhusa na nia na adabu ifaayo.

2. Onyesha kwamba Mungu hayuko mbali, si asiyeweza kufikiwa.

2 Mungu aweza kufikiwa. Yeye si “mfu,” kama wengine wasemavyo. Yaani, yeye hakujitenga, akiwaacha wanadamu peke yao, pasipo nia ya kusikiliza matatizo yetu au kuyatatua. Ni kama vile mtume wa Yesu Kristo alivyotangaza: “[Mungu] akiisha kuwawekea nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.”​—Matendo 17:26, 27.

3. Je! Mungu yuko mahali pote? Makao yake yako wapi?

3 Mungu hawi mahali pote kwa wakati mmoja, si roho anayeenea kote. Wala hakufanyizwa kwa vitu vyote. Yeye ndiye aliyeviumba. Kwa kuwa ni Mtu, yeye anapo mahali anapokaa anapoweza kufikiwa. Anakaa mbinguni, katika makao yasiyoonekana.​—Mt. 6:9.

4. Ni kwa sababu gani Mungu aliibadili sura ya makao yake ya kimbinguni?

4 Yeye amefanya mipango ya pekee kwa ajili ya faida ya watu wanaotaka kumfikia, si kwa ajili ya faida yake mwenyewe. Kwa kufanya hivyo aliibadili sura ya makao yake ya kimbinguni. Haikubadilishwa kwa upande wa malaika, ambao wamekuwa na ruhusa ya kumfikia sikuzote; kama alivyosema Yesu, wao “huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.” (Mt. 18:10) Ilibadilishwa wanadamu wenye dhambi waweze kuwa na njia ya kumwomba na nafasi ya kupata kibali yake.

HEKALU KUU LA KIROHO LA MUNGU

5. Je! mahekalu Yerusalemu yalikuwa kama ‘ile hema ya kweli, ambayo Yehova aliiweka wala si mwanadamu’? Eleza.

5 Jengo hili linaitwa “hekalu” au “ile hema ya kweli, ambayo [Yehova] aliiweka wala si mwanadamu.” (Ebr. 8:1, 2) Mahekalu ya zamani katika Yerusalemu yalikuwa “mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni” tu. (Ebr. 8:5) La mwisho la majengo hayo liliharibiwa na Warumi mwaka wa 70 C.E. Kwa hiyo, “hema” au jengo lililosimamishwa na Mungu ambalo kupitia kwake wanadamu wanaweza kumfikia si hekalu, kanisa au jengo la kidunia.

6, 7. Ni wakati gani “ile hema ya kweli” ilipotokea, nasi twawezaje kujua?

6 Katika toleo lililotangulia la gazeti hili tulizungumza sehemu za “hema” au hekalu la mfano kwa kirefu. Lakini je! ni wakati gani kitu chenyewe, hema au hekalu la mfano, lilipotokea? Ni katika vuli ya mwaka wa 29 C.E. Ikawaje hivyo?

7 Ili kupata jibu, na tuuchunguze utaratibu wa Siku ya Upatanisho ya mfano. Kwa njia hii twaweza kuona namna kila sehemu ya “ile hema ya kweli” au hekalu ilivyotokea.

UA NA MADHABAHU YAKE

8, 9. (a) Ua uliofananishwa ni nini? (b) Kristo alipataje kuwa na dhabihu iliyofaa kutoa?

8 Kama vile ua wa hekalu Yerusalemu ulivyokuwa mtakatifu na wanyama wa dhabihu walioletwa ndani yake walivyopaswa kutokuwa na kasoro, ndivyo na ua uliofananishwa wa makuhani ulivyoonyesha hali ya uana wenye haki wa kibinadamu usio na kasoro mbele za Mungu. Yesu alikuwa mwana wa Mungu wa kibinadamu aliye mkamilifu alipojitoa abatizwe katika Mto Yordani. Mungu alikuwa amekwisha hamisha uhai wa Mwanawe na kuutia katika tumbo la uzazi la bikira Mariamu. (Yohana 17:5; Luka 1:35) Kwa hiyo Yesu angeweza kumwambia Mungu hivi:

9 “Dhabihu na toleo hukutaka, lakini mwili uliniwekea tayari; sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo; . . . Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) niyafanye mapenzi yako, Mungu.”​—Ebr. 10:5-7.

10, 11. (a) Ni nini kilichofananishwa na madhabahu? Eleza. (b) Ni wakati gani ilipoanza Siku ya Upatanisho iliyo kuu?

10 Ndipo mtume Paulo anapoeleza: “Katika mapenzi hayo tumepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.”​—⁠Ebr. 10:10.

11 Kwa kweli Mungu hakutaka dhabihu na sadaka za dhambi za wanyama. (Ebr. 10:8) Mapenzi ya Mungu yalikuwa kwamba mwanadamu mkamilifu autoe uhai wake kama upatanisho na bei ya ukombozi kwa wanadamu, waliokuwa wamepoteza uzima kwa dhambi ya baba yao Adamu. Kwa hiyo “madhabahu” ya kiroho ambayo juu yake dhabihu ya Yesu iliwekwa ilikuwa “mapenzi” ya Mungu. Mwendo wa dhabihu wa Yesu ulianza wakati alipojitoa abatizwe na akakubaliwa na Mungu. “Madhabahu” ya kiroho, na vile vile “ua,” vilitokea vyenyewe sasa​—vilitenda kazi. Siku ya Upatanisho iliyo kuu iliyofananishwa ilikuwa imeanza sasa.

“PATAKATIFU SANA”

12. ‘Patakatifu Sana’ penyewe palitokeaje wakati huo?

12 Wakati ule ule pia, ‘Patakatifu Sana’ pa kiroho palitokea. Namna gani? Sasa makao ya Mungu yalipata kuwa na hali za pekee kwa habari ya uhusiano wa mbingu na wanadamu. Yehova alikuwa mwenye nia ya kupatanishwa na kutulizwa na sadaka ya dhambi yenye kuridhisha, hata ilikuwa kana kwamba aliweka kiti chake cha enzi juu ya kifuniko cha upatanisho cha sanduku la agano, agano jipya, ambalo lingehalalishwa na damu ya sadaka (dhabihu) hiyo. Sadaka aliyokuwa na nia ya kuikubali ilikuwa dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya Kuhani Mkuu Yesu Kristo.​—Luka 22:20; linganisha Ufunuo 11:19.

“PATAKATIFU”

13. Yesu alikuwaje katika ‘Patakatifu’ palipofananishwa wakati wa huduma yake ya kidunia?

13 Tangu wakati wa ubatizo wake, Yesu alitembea katika “ua” uliofananishwa akiisimamia dhabihu yake ya kibinadamu hata kufa. Humu angeweza kuonekana na watu wa dunia, kama ilivyokuwa kwa habari ya ua pamoja na madhabahu yake hemani katika jangwa. Lakini hema ya kidunia ilikuwa na kisitiri mbele yake kilichozuia chumba cha Patakatifu kisionekane ndani. Patakatifu palifananisha hali ya utakatifu mwingi zaidi kuliko vile ua ulivyofananisha; hii ilikuwa hali ya kuwa mwana wa Mungu aliyezaliwa kwa roho alipokuwa angali duniani. Kwa hiyo, wakati Yesu alipozaliwa kama Mwana wa Mungu wa kiroho wakati wa ubatizo wake, aliingia na Mungu katika uhusiano uliositiriwa usionekane na wengine​—usioonekana kwa macho yao ya kimwili. (Mt. 3:16, 17) Sasa alizaliwa upya kwa habari ya matumaini ya kimbinguni, arudie mbinguni katika wakati wake akawe pamoja na Baba yake.​—Linganisha 1 Petro 1:23.

14. Ni vitu gani vilivyotolewa kwa Yesu alipokuwa katika ‘Patakatifu’ pa hekalu kuu la kiroho?

14 Ndani ya Patakatifu kilikuwamo kinara cha taa cha dhahabu, meza ya mikate ya wonyesho na madhabahu ya uvumba. Wakati Yesu alipokuwa katika huduma yake ya waziwazi akatembea duniani miaka mitatu u nusu, alikuwamo pia katika hali iliyofananishwa na ‘Patakatifu’ pa hekalu kuu la kiroho la Mungu. Aliangazishwa na nuru ya kiroho kana kwamba kwa kinara cha taa, alipokea chakula cha kiroho kana kwamba katika meza ya mikate ya wonyesho, naye alitoa sala na sifa kwa Baba yake, kana kwamba zilikuwa uvumba.​—Luka 4:1; 6:12, 13; Yohana 4:32; 5:19, 20; Ebr. 5:7.

15. Kwa sababu gani Yesu asingeweza kuingia katika ‘Patakatifu Sana’ pa hekalu alipokuwa duniani, nalo hili lilifananishwaje?

15 Ingawa alikuwa Mwana wa Mungu wa kiroho kwa njia hiyo, kungali kulikuwako kitu cha kumzuia asiingie mbinguni akawe pamoja na Baba yake. Hicho kilikuwa mwili wake, sawa na vile pazia lililotenganisha Patakatifu na Patakatifu Sana hemani lilivyomzuia kuhani mkuu asiingie. (Ebr. 10:20) Kwa maana “nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu.” (1 Kor. 15:50) Ilikuwa lazima Yesu afe, akiuvua mwili wa nyama ili aweze kupokea “tabia ya Uungu,” kwa kufufuliwa “katika roho.”​—2 Pet. 1:4; 1 Pet. 3:18, NW.

KULETA UVUMBA KATIKA PATAKATIFU SANA

16-18. (a) Ni nini kilichofananishwa na kuingia kwa kuhani mkuu wa Israeli katika Patakatifu Sana pa hema kwanza akiwa na chetezo cha uvumba? (b) Yesu alimtoleaje Mungu uvumba kwa njia iliyofananishwa?

16 Kuhani mkuu wa Israeli aliingia katika hema mara kadha wakati wa mipango ya Siku ya Upatanisho, kama ionyeshwavyo katika Mambo ya Walawi sura ya 16. Mara ya kwanza aliingia akiwa na chetezo cha makaa ya moto ambapo uvumba uliwekwa. (Law. 16:12, 13) Hili lilitimizwaje na Yesu Kristo? Bila shaka, hii haikumaanisha kwamba Kristo aliingia mbinguni kabla dhabihu yake haijamalizika. Bali, kwa kuwa kuingia na uvumba kulifanywa mara ya kwanza ilionyesha kwamba kulifananisha jambo la lazima na la maana zaidi kuliko kutoa kwa Yesu mbinguni bei ya dhabihu yake ya kununulia wanadamu. Hili lilikuwa nini?

17 Kudumisha ukamilifu kwa Kristo akiwa chini ya jaribu ndiko kulikofananishwa, kwa njia hiyo ikihakikisha kwamba mwanadamu aweza kudumisha imani kamili na utii kwa Mungu. Kwa hiyo Yesu alimfunua Ibilisi kuwa mwongo katika shtaka lake kwamba Mungu hakuwa akivitawala viumbe vyake vyote vyenye akili kwa haki, kwamba hivi vilikuwa vikimtumikia kwa sababu ya choyo ama kwa kulazimishwa, si kwa sababu ya upendo na uaminifu wa kweli.​—Ayubu 1:9-11; 2:4, 5; Mwa. 3:1-5.

18 Yesu alilitaja kusudi lake la kwanza la kuja duniani wakati aliposema: “Kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli.” (Yohana 18:37) Alidumisha ukamilifu, akimwonyesha Shetani kuwa mwongo. (Yohana 12:31; 14:30) Kama Yesu angalishindwa yeye mwenyewe angaliupoteza uzima wake na asingaliweza kuwa amewakomboa wanadamu. Kama vile kuhani mkuu alivyoleta uvumba katika Patakatifu Sana, ndivyo na Yesu alivyomtolea Mungu sala, utumishi na uaminifu usio na kasoro kwa bidii wakati wote wa huduma yake.

KUINGIA KWA KRISTO KATIKA PATAKATIFU SANA

19, 20. (a) Ni wakati gani na kwa njia gani Yesu alivyomtolea Yehova “damu” yake? (b) Ni nini kilichofananishwa na damu ya ng’ombe dume, kisha ile ya mbuzi, iliyokuwa ikitolewa katika Patakatifu Sana?

19 Kwa kuwa dhabihu ya uzima wake mkamilifu wa kibinadamu ilikuwa imekamilishwa, Kristo angeweza kuingia katika ‘Patakatifu Sana’ penyewe baada ya ufufuo wake, si akiwa na damu halisi ya dhabihu yake, bali akiwa wa bei ya uzima wake mkamilifu wa kibinadamu. Kama vile kuhani mkuu wa Israeli alivyoitakasa nyumba yake mwenyewe kwanza kwa damu ya dhabihu ya ng’ombe dume, kisha akawatakasa watu kwa damu ya ‘mbuzi wa Bwana,’ ndivyo na ubora wa upatanisho wa dhabihu ya Yesu ungetumiwa kwanza kwa nyumba yake ya makuhani wadogo, washiriki 144,000 waliotiwa mafuta waliozaliwa kwa roho wa kundi la Kikristo, ndugu zake wa kiroho. Baadaye, ungetumiwa kwa wanadamu kwa ujumla, kwa maana Kristo aliwanunua wanadamu wote kwa damu yake.​—1 Yohana 2:1, 2; Rum. 8:29, 30; linganisha Waebrania 11:39, 40; Ufunuo 7:9, 10; Warumi 8:21.

20 Kwa kuwa mbuzi aliyechukua dhambi za watu Siku ya Upatanisho alikwenda jangwani, naye Yesu aliziondolea mbali dhambi za wanadamu, zisahauliwe kabisa.​—Law. 16:20-22.

21. (a) Ni wakati gani ilipoanza na kumalizika ile Siku ya Upatanisho iliyo kuu, nayo ilichukua kipindi cha muda mrefu namna gani? (b) Ni ushuhuda gani uliohakikisha dhabihu ilikuwa imekuwa ya kukubalika kwa Mungu?

21 Wakati ubora wa dhabihu ya Kristo ulipotolewa mbinguni Siku ya Upatanisho iliyo kuu ilimalizika. “Siku” hii ilianza wakati wa ubatizo wa Yesu katika vuli ya mwaka wa 29 C.E. mpaka wakati wa kutolewa kwa bei ya dhabihu yake mbinguni katika masika ya mwaka wa 33 C.E. Siku kumi baada ya kupaa kwa Yesu mbinguni ushuhuda ulitolewa kwa wanafunzi wake waaminifu kwamba ubora wa dhabihu yake kamilifu ya kibinadamu uliotolewa kwa Mungu katika ‘Patakatifu Sana’ pa kimbinguni ulikuwa umekubaliwa. Namna gani? Kwa kumiminwa kwa roho takatifu juu yao Yerusalemu siku ya Pentekoste, mwaka wa 33 C.E.​—Matendo 2:1-36.

22. Je! mtu ye yote aweza kumpata Mungu? Ni nini kinachohitajiwa?

22 Kwa hiyo, kuna mahali ambapo Mungu aweza kupatikana kweli​—ndani ya hekalu lake la kweli, ambalo ndilo jengo lake la kiroho la ibada safi. Njia ya kumfikia i wazi kwa watu wote, bila ya kujali hali yao ya maisha. Ili kumfikia Mungu lazima uamini kwamba yeye yupo na kwamba si “mfu,” asiyependezwa nawe. Mtume Paulo anaandika: “Mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.”​—Ebr. 11:6.

[Picha on page 436]

HEMA Kama ambavyo huenda ilionekana ndani yake ikionyeshwa wazi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki