Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 3/1 kur. 116-120
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Heshimu “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Maoni ya Biblia Kuhusu Talaka na Kutengana
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 3/1 kur. 116-120

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Ikiwa, baada ya talaka ya kisheria kupatikana, mtu ajua kwamba mwenzi wake (mwanamume au mwanamke) alikuwa na hatia ya uzinzi au ufisadi mwingine mzito kabla ya talaka, je! hiyo ingetoa uthabiti unaolingana na Maandiko kwa talaka ya kisheria? Pia, je! msamaha wa tendo moja la uzinzi ungekataza kupata talaka juu ya sababu za Maandiko ikiwa baadaye yagunduliwa kwamba matendo mengi ya ufisadi yalihusika?​—Sweden.

Ziko nyakati ambapo kujua habari za uzinzi wa mwenzi aliyetalikiwa au mazoea yake ya ufisadi mwingine mzito kabla ya talaka kungetoa uthabiti kwa talaka ambayo tayari imepatikana. Pia, msamaha kwa tendo moja la uzinzi haumaanishi kwa lazima kwamba uchafu mwingine wa zamani usioelezwa wazi wa malazi ya ndoa umesamehewa vile vile.

Kulingana na Maandiko, uzinzi au ufisadi mwingine mzito hauvunji kifungo cha ndoa vivyo hivyo tu, bali unampa mwenzi asiye na hatia msingi kufanya hivyo. (Mt. 5:32; 19:9) Kwa upande mwingine, machoni pa Mungu, talaka iliyopatikana bila msingi wa Maandiko haimruhusu ye yote wa wenzi aoe au aolewe tena. Talaka hiyo inafanana na kutengana kisheria kulingana na maoni ya Maandiko.

Shauri la mtume Paulo kwa watu waliooana ni: “Mke asiachane na mumewe; lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.”​—1 Kor. 7:10, 11.

Hata hivyo, mtengano waweza kutokea na waweza kufanywa wa kisheria na tendo la talaka juu ya sababu nyingine zisizo “uasherati,” ingawa hili halitokei sana kati ya Wakristo wa kweli. Mkristo akijikuta katika hali hii huenda baadaye akajua mwenzi aliyetalikiwa alifanya uzinzi kabla ya talaka. Huyo sasa anakabiliwa na uamuzi wa kama atatumia huu kama msingi wa kuthibitishia kundi uhuru wake unaolingana na Maandiko wa kuoa au kuolewa tena. Ikiwa, baada ya kuthibitishia halmashauri ya hukumu ya kundi kuwa kwake huru kutokana na mwenzake, anaamua kuoa au kuolewa tena, huyo hawezi kushtakiwa juu ya uzinzi.

Walakini, mwenzi asiye na hatia aweza kuamua kutotumia huu kama msingi wa kuthibitisha uhuru wake unaolingana na Maandiko wa kuoa au kuolewa tena. Pengine uzinzi au ufisadi mzito wenyewe ulifanywa na mwenzi miaka mingi iliyopita. Asiye na hatia huenda akawa ameishi miaka mingi na mwenzake katika mpango wa ndoa baada ya tendo hilo la ufisadi (ingawa halikujulikana wakati huo) na kabla ya mtengano. Kwa hiyo, ingawa sasa wametalikiana, asiye na hatia aweza kutaka kusamehe kosa lililotokea zamani, akiamini kwamba hivyo ndivyo yeye angalifanya kama jambo hili lingalielezwa wazi wakati huo. (Efe. 4:32) Asiye na hatia aweza kulifikiria tumaini la kukubaliana tena na mwenzi wa ndoa wa zamani na kuingia katika ndoa ya kisheria tena na huyo.

Namna gani juu ya ile hali nyingine, ile ya mtu ambaye angali ameoa au ameolewa ambaye, baada ya kusamehe tendo moja la uzinzi, baadaye anapata kujua matendo mengine ya ufisadi au upotovu yaliyofanywa na mwenzi mwenye hatia, matendo yaliyofanywa kabla ya msamaha huo kutolewa? Hii ingempa mwenzi asiye na hatia nafasi ya kulifikiria jambo hili tena. Biblia yaonyesha kwamba hata Yehova Mungu aona mazoea ya dhambi kama mazito zaidi kuliko tendo moja la dhambi. (1 Yohana 1:8–2:1; 3:4-6) Ingawa mwanamume au mwanamke aweza kuwa na nia ya kusamehe tendo moja la uzinzi, aweza kujisikia tofauti juu ya kusamehe mazoea ya makosa ya ufisadi ya kipindi kilichorefushwa. Ikiwa hivyo, watu wengine wangechagua tena kumsamehe mwenzi mwenye hatia lakini huenda wengine wakataka kuutumia ushuhuda huu mpya wapate talaka na kulithibitishia kundi uhuru wao unaolingana na Maandiko wa kuoa au kuolewa tena. Hii ingetumika kwa watu waliotengana pia sawa na wale ambao wangali wanaishi pamoja kama mume na mke.

Kwa hiyo, matendo ya kutoaminika kwa mambo ya ndoa yasiyosamehewa zamani yaweza kutoa msingi wa kuthibitisha kwa Maandiko haki ya kuvunja kifungo cha ndoa machoni pa Mungu. Bila shaka, mtu achaguaye kufanya hivi lazima awe na nia ya kuchukua daraka hilo mbele za Muumba wake. Ijapokuwa wazee wa kundi wenyewe wanaweza kuona kwamba msamaha ungalifaa zaidi, wanaliacha jambo hili mikononi mwa Yehova kama Mwamuzi wa mwisho. Yeye peke yake aujua moyo na makusudi ya mtu anayejaribu kuthibitisha uhuru unaolingana na Maandiko wa kuoa au kuolewa tena. (1 Kor. 4:5) Kwa habari ya tendo lo lote la kutoaminika katika mambo ya ndoa lililokuwa limesamehewa kwa wazi zamani, baadaye haliwezi kutumiwa kama msingi wa Maandiko wa kupatia talaka wala wa kuthibitishia haki ya kuoa au kuolewa tena.

Yaweza kuangaliwa kwamba katika mambo haya kundi la Kikristo linaongozwa na Maandiko wala si na masharti ya kisheria yanayoshikamanwa nayo katika maeneo fulani yasiyoruhusu ushuhuda mpya utolewe baada ya kesi kusikiwa mara moja na kuamuliwa.

● Katika visa vya uzinzi, je! ziko hali zo zote ambapo mwenye hatia angeweza kupata talaka na kuonwa na kundi mwenye uhuru wa kuoa au kuolewa tena?​—Jamaica.

Zaweza kuwako hali ambazo zingeruhusu kundi, kupitia kwa wazee wake waliowekwa, kuwa na maoni hayo. Walakini, kabla ya kufikiria hali hizo imetupasa kwanza turudie kuangalia kanuni za Biblia za msingi juu ya talaka.

Maneno ya Yesu katika Mathayo 5:31, 32 na 19:9 yaonyesha kwamba kufanya “uasherati” (Kigiriki: porneia) kwa mwenzi kwafanyiza msingi wa pekee wa talaka iliyo thabiti machoni pa Mungu. Maneno yake yaonyesha pia kwamba Mungu ampa mwenzi asiye na hatia haki ya kukomesha ndoa, kuvunja vifungo vya ndoa.

Walakini, yapaswa iangaliwe kwamba si tendo la uasherati tu lifungualo vifungo hivyo. Mwenzi asiye na hatia aweza kuchagua kulisamehe tendo baya la mwenzi mzinzi. Ikiwa hivyo vifungo vya ndoa vyabaki pasipo kufunguliwa. Kwa hiyo, basi, jambo lenye kuamua nyakati zote ni uamuzi wa mwenzi asiye na hatia kusamehe au kukataa kusamehe mwenzi mzinifu.

Namna gani, basi, ikiwa​—baada ya mwenzi kufanya “uasherati”​—mwenzi asiye na hatia anakataa kumkubalia huyo arudi, pengine akikataa wasiishi nyumba moja au, ingawa wanaishi katika nyumba moja, anakataa asifanye ngono na mwenye hatia, na hali hakutafuta talaka ya kisheria katika korti za nchi? Namna gani hali hii ikiendelea kwa muda uliorefushwa, mwaka mmoja au hata miaka mingi, kwa njia hiyo akinyima mwenzi aliyekuwa ameufanya ubaya ngono zo zote zenye kuheshimika kwa kumlipa haki ya ndoa?

Biblia yaonyesha kwamba watu waliooana hawapaswi kunyimana haki ya ndoa “isipokuwa mmepatana kwa muda,” ama sivyo kishawishi chaweza kuingia. (1 Kor. 7:2-5) Kumnyima mwenzi haki hiyo kwa muda mrefu au usio na kikomo ungekuwa mwendo usio wa upendo. Kama mwenzi asiye mzinifu akifanya hivyo ingefanyiza shuhuda wa kwamba msamaha wa kweli wa tendo la uzinifu haukutolewa. Kwa makusudi yote na nia, mwenzi asiye mzinifu amemkataa mwenye kukosa asiwe mwenzi wake wa ndoa. Na, kama ambavyo imeonwa, kuvunjwa kwa ndoa kunakolingana na Maandiko kwategemea uamuzi wa mwenzi asiye mzinifu kusamehe au kutosamehe kutenda “uasherati” kwa yule mwenzi mwingine.

Bila shaka Yehova Mungu angejua kukataa huko ingawa mwenzi asiye mzinifu hakwenda mbele ya korti za “Kaisari” kuhakikisha kuvunjwa kwa ndoa. Ni vema kukumbuka kwamba sheria za korti ya kimungu ya Yehova ndizo za maana zaidi. Mamlaka ya Kaisari ni ya kadiri nayo haiamui kama vifungo vya ndoa vinavunjwa au vinabaki vimefungwa machoni pa Mungu. (Linganisha Matendo 5:29.) Kaisari aweza kusema tu kama atoa utambuzi au sivyo wa kama ndoa ingali yaendelea. Hivyo, usipokuwapo msingi wa Maandiko (“uasherati”), hata Kaisari akitoa talaka, haithibitiki machoni pa Mungu hata kuweza kuwapa wenye kutalikiana uhuru wa kuoa au kuolewa tena.

Bila shaka, kwa ‘kujipendekeza mwenyewe kwa kila dhamiri ya kibinadamu,’ kwa kufaa Mkristo atajitahidi apate utambuzi huo wa kisheria kutoka kwa Serikali katika ndoa au katika talaka. (2 Kor. 4:2, NW) Lakini utambuzi huo wa kisheria silo jambo la maana; la maana ni uamuzi wa hukumu ya Mungu. Hii ikiwa hivyo, na kwa kuwa uamuzi wa mwenzi asiye mzinifu wa kusamehe au kutosamehe ndilo jambo la maana sana katika kuvunjwa kwa ndoa, mwenzi mwenye hatia aweza kufanya nini akikabiliwa na hali ambamo mwenzi asiye mzinifu hakumsamehe lakini hataki kuhakikisha kuvunjwa kwa ndoa mbele ya Kaisari? Mwenzi mwenye hatia aweza kuchukua hatua authibitishe uhakika huu kwamba amekataliwa kweli na mwenzi asiye mzinifu. Kwanza hii imepaswa ifanywe mbele ya wazee wa kundi, akiwapa ushuhuda kwamba amekataliwa kabisa na kwa uthabiti, si kwa muda. Halafu yeye ambaye mwenzi wake akataa kumsamehe aweza kutafuta utambuzi wa kisheria wa kukataliwa huko katika korti za Kaisari, akitumia sababu zo zote za kweli za talaka zitakazokubaliwa na korti hizo, baada ya hapo akiwa huru kuoa au kuolewa tena. Katika nchi zisizo na mpango huo, utaratibu wake ungefuata ule unaoelezwa katika ukurasa wa 151 wa kitabu Amani ya Kweli na Usalama wa Kweli​—Kutoka Chanzo Gani?

Wazee kundini, wakikabiliwa na kesi kama hiyo, wamepaswa wapime mambo kwa usawa, wakiamua kwamba kweli kuna ushuhuda wa wazi na wenye kusadikisha wa kukataliwa hasa na mwenzi asiye mzinifu. Kwa mfano, mwenzi aliyekosewa huenda asitake kurudia tena kufanya ngono juma chache au hata miezi kwa sababu angali aukumbuka sana uzinzi akilini. Huku kusingekuwa kukataliwa kwa kweli. Yapaswa iangaliwe pia kwamba habari zilizotangulia hazisemi kwamba kukosa kulipa haki ya ndoa kwenyewe ni msingi wa talaka. Lazima “uasherati” (msingi unaolingana na Maandiko wa talaka) uwe ulifanywa na mtu ambaye baada ya hapo ananyimwa haki ya ndoa na ambaye, kwa kweli, amekataliwa na mwenzi asiye mzinifu.

● Je! mazoea machafu kwa upande wa mtu aliyeoa juu ya mwenzi wake mwenyewe yanafanyiza msingi unaolingana na Maandiko kwa mwenzi aliyekosewa apate talaka?

Ziko nyakati ambapo mazoea machafu ndani ya mpango wa ndoa yangetoa msingi wa talaka inayolingana na Maandiko. Bila shaka, Maandiko Matakatifu hayatii moyo kuwepo na talaka wala hayamwamuru asiye na hatia amtaliki mwenzi anayefanya uzinzi au upotovu mwingine mzito wa ngono.

Kwa habari ya talaka, Yesu Kristo alisema hivi: “Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini.” (Mt. 19:9) “Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.”​—Mt. 5:32.

Hivyo “uasherati” waonyeshwa kama msingi wa pekee wa talaka. Katika Kigiriki cha kawaida ambacho katika hicho maneno ya Yesu yameandikwa, neno “uasherati” ni por·neiʹa, linalomaanisha namna zote za ngono ya ufisadi, mazoea mapotovu na machafu kama yale yawezayo kuendeshwa katika nyumba ya ukahaba, kutia na ngono za kutumia mdomo na mkundu.

Kwa habari ya maneno ya Yesu juu ya talaka, hayaonyeshi wazi “uasherati” au por·neiʹa unafanywa na nani. Yanaliacha shauri hilo hivyo. Kwamba por·neiʹa laweza kufikiriwa kwa kufaa kama lenye kutia ndani mapotovu ndani ya mpango wa ndoa yaonekana kwa sababu mwanamume amlazimishaye mkewe afanye ngono zisizo za asili naye kwa njia hiyo ‘por·neiʹa, kwa maana kiarifa cha Kigiriki kinachohusiana na hili por·neiʹa chamaanisha “kufanyia ukahaba, kufisidi.”

Kwa hiyo, hali zaweza kutokea ambazo zingefanya mazoea machafu ya mtu aliyeoa juu ya mwenzi wake wa ndoa yawe msingi unaolingana na Maandiko wa talaka. Kwa mfano, mke aweza kufanya yote awezayo kumzuia mumewe asimlazimishe kufanya mapotovu kama yale yanayoendeshwa katika nyumba ya makahaba. Lakini, kwa sababu ya nguvu nyingi zaidi za mume, aweza kumshinda mke nguvu na kumtumia kwa ngono iliyopotoshwa. Ili asifanyiwe ukahaba kwa njia hii tena, mke wa Kikristo aweza kuamua kupata talaka. Aweza kuthibitishia kundi kwamba sababu yake ni por·neiʹa kisha aendelee na kupata talaka ya kisheria juu ya sababu zo zote za kweli zinazokubalika na korti za nchi.

Ikiwa, kwa upande mwingine, mazoea machafu yaliingiliwa wote wakiwa wamekubaliana, hakuna mwenzi ye yote kati yao angekuwa na msingi wa kudai por·neiʹa kama msingi unaolingana na Maandiko wa talaka. Ndivyo ilivyo kwa sababu hakuna asiye na hatia kati yao wala anayetafuta uhuru wa kutokuwa na mwenzi mwenye hatia ya por·neiʹa. Wenzi wote wawili wa ndoa ni wenye hatia. Kisa kama hicho, kikikaziwa fikira za wazee kundini, kingeshughulikiwa kama kosa jingine lo lote zito.

● Je! yafaa mwanamke wa Kikristo atobolewe ndewe (masikioni) atie vipuli (pete za sikio)?​—B.C., Canada.

Maandiko hayatoi habari zenye kuwezesha kutoa jibu la ndiyo kabisa au sivyo kwa ulizo hili. Kama mtu atatobolewa ndewe zake kwa kusudi hili ni shauri la uamuzi wa kipekee.

Tunayo kanuni katika Mambo ya Walawi 19:28, iliyokataza kukata-kata nyama ya mwili wa mtu kwa ajili ya nafsi iliyokufa. Haya yalikuwa mazoea yaliyopatikana kati ya wale waliokuwa na imani za uongo za kidini. Huenda wengine wakaona kwamba katazo hili lingetumika kwa kanuni kwa kukata-kata kwingine kusiko kwa lazima.

Mtu aweza kuangalia pia kwamba Mungu alipoumba miili ya kibinadamu kwanza aliiona kazi yake kuwa ‘njema sana.’ Kwa hiyo mtu asingetaka aharibu sana mwili wake.​—Mwa. 1:27, 31.

Kwa upande mwingine, Biblia yataja vipuli (pia pete za puani) na leo hakuna njia ya kujua kama matumizi haya yalitia na kutoboa masikio au sivyo.​—Mwa. 24:22, 47; Kut. 32:2; 35:22; Eze. 16:12.

Twaweza pia kuangalia kwamba agano la Torati liliruhusu kutobolewa sikio la mtumwa aliyekuwa ametimiza kipindi chake kilichohitajiwa cha utumwa na aliyetaka aendelee kuwa mtumwa wa bwana mwema. (Kut. 21:2-6) Bwana alipaswa atoboe mojawapo ya ndewe za mtumwa kwa msharasi kama ishara ya hili. Bila shaka, hii haikuwa kama mapambo tu kama vile kwa habari ya kutoboa masikio kwa ajili ya kutia vipuli, lakini matokeo juu ya nyama ya mwili wa mtu yalikuwa yale yale.

Katika kuyaangalia mambo haya mbalimbali pamoja ni wazi kwamba hakuna jibu la kukata maneno liwezalo kutolewa. Lazima kila mwanamke wa Kikristo atumie dhamiri yake mwenyewe katika shauri hili. Kwa kutumia kanuni zilizotajwa juu, huenda wengine wasitake kutobolewa masikio yao; wengine huenda wakaona wanaweza kufanya hivyo kulingana na dhamiri. Mwanamke aliyeolewa anayependelea kutobolewa masikio amepaswa kwa haki kwanza amwulize mume wake aliye kichwa. Vivyo hivyo, mtoto angezungumza shauri hili na wazazi wake na kushikamana na uamuzi wao, kupatana na mpango wa Yehova wa jamaa.​—Kol. 3:18, 20; Efe. 5:22–6:4.

Kama Wakristo imetupasa pia tufikirie maoni ya wengine. Twaweza kulikumbuka shauri la mtume linaloonyesha kwamba kuvaa mapambo si kwa maana kama kujipamba “pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi” na “matendo mema.”​—1 Pet. 3:3; 1 Tim. 2:9, 10.

● Je! wale watakaofufuliwa duniani watakuwa wangali wasiokamilika na wenye kutaabishwa na dhambi ya Adamu, kwa kuwa Warumi 6:7 yasema kwamba mtu “aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi?”​—U.S.A.

Warumi 6:7 yasema: “Kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.” Kuangalia maneno yanayozunguka kwaonyesha kwamba mtume Paulo alikuwa akizungumza juu ya Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho waliokuwa hai wakati huo. Wakiwa wangali hai, walikuwa wamebatizwa katika Kristo Yesu na kupokea tumaini thabiti la uzima wa kimbinguni. Ili kutiwa mafuta kwa roho takatifu na kukubaliwa kama wana wa Mungu wa kiroho, iliwapasa wafe kwa habari ya mwendo wao wa zamani katika maisha kama wanadamu wasiokamilika, wasamehewe dhambi zao na Mungu na wahesabiwe ukamilifu wa kibinadamu.

Lakini kwa kutoa maelezo haya kwa habari ya Wakristo waliotiwa mafuta, Paulo alikuwa akitokeza mfano wa asili na kweli. Katika matumizi yake mengi, yaweza kusemwa kwa kweli kwamba mtu ambaye amekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.

Mauti, si utaratibu wa kufa wenyewe, ndiyo malipo kamili ya dhambi. Biblia yasema: “Mshahara wa dhambi ni mauti.” (Rum. 6:23) Hii yamaanisha kwamba wakati ambapo mtu amekufa kumbukumbu lake lenye dhambi halibaki kumwelekea. Na kama isingalikuwa kwa sababu ya dhabihu ya Yesu Kristo na kusudi la Mungu kumfufua mtu huyo, asingeishi tena. Hata hivyo, angebaki amehesabiwa haki mbali na dhambi, kwa maana Mungu asingechunguza-chunguza habari yake kisha amhukumie namna nyingine za adhabu kwa sababu ya dhambi yake.

Hii yaweza kulinganishwa na hali ya mtu anayetumikia kifungoni kwa sababu ya tendo fulani la uvunjaji wa sheria. Amalizapo kifungo chake, hahukumiwi tena na tena na kuadhibiwa kwa uvunjaji ule ule wa sheria.

Sasa kwa habari ya mtu aliyefufuliwa kwenye maisha ya kidunia, kumbukumbu lenye dhambi lililomfanya ahukumiwe kifo halibaki kumwelekea tena. Kama mtu aliyefunguliwa kifungoni, anayo nafasi ya kujipatanisha na sheria. Hata hivyo, mwenye kufufuliwa ni mwanadamu yule yule. Kifo chake hakikutokeza badiliko lo lote ndani yake kwa habari ya utu na maelekeo yenye dhambi. Kwa kufufuliwa hakuwa mwanadamu mkamilifu, asiye na matokeo yote ya dhambi na kutokamilika kulikorithiwa kwa Adamu. Hakutangazwa kuwa mwenye haki kwa sababu ya kufa. Kama vile katika habari ya mtu aliyekuwa mfungwa, lazima atie jitihada asishindwe na udhaifu wake wa kimwili. Twaweza kusema, lazima aanzie alipoachia katika maisha na kutumia kwa faida kabisa mipango ya Mungu uzima wa milele duniani.

Kwa sababu ya maisha waliyoishi kabla kufa kwao, watu wengine wataelekea zaidi kufanya mabaya kuliko wengine. Kwa kweli, Biblia yasema: “Kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia.” (Matendo 24:15) Kwa hiyo wale waliokuwa wasio haki wakati wa kufa kwao watakuwa wasio haki wakati wa kufufuliwa kwao kwenye maisha ya kidunia.

Kwa hiyo ingawa inamhesabu mtu kuwa mwenye haki mbali na kumbukumbu la dhambi, mauti haitokezi badiliko lo lote kwa namna mtu alivyo. Wale watakaofufuliwa duniani ni wa wale wale waliokufa, wazao wa Adamu mtenda dhambi. Wao ni wanadamu wasiokamilika, kama walivyokuwa wale waliofufuliwa na Eliya, Elisha, Yesu Kristo, Petro na Paulo karne nyingi zilizopita. Kufa na kufufuliwa kwa watu zama hakukuwageuza wakawa watu wakamilifu wawezao kuishi milele. Kwa hiyo kwa habari wale watakaofufuliwa duniani katika Taratibu Mpya, kutumia kwao mipango yenye kulipia dhambi ya dhabihu ya Yesu ndiko kutakakowakinga na kifo.

Katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo, mpango wa Mungu wa uzima, kutia na mpango wenye kulipia dhambi, unaonyeshwa kwa mfano kama mto wa maji ya uzima. (Ufu. 22:1, 2) Kwa hiyo ni kwa kunywa katika ‘mto’ huu kwamba watakaofufuliwa watakombolewa polepole na maelekeo yote yenye dhambi na kuwa wanadamu wakamilifu.

Yehova Mungu hawaoni kama wamekuwa hai kabisa mpaka watakapokuwa wanadamu wakamilifu. Kwa wazi ni kwa sababu hiyo Biblia yasema juu ya wale watakaofufuliwa duniani kwamba ‘hawawi hai hata itimie ile miaka elfu’ ya utawala wa Ufalme wa Kristo, wakati ambapo faida za dhabihu yake yenye kulipia dhambi zitatumiwa kwa wanadamu.​—Ufu. 20:5.

● Zaburi 5:4 yasema hivi juu ya Yehova, “Mtu mwovu hatakaa kwako.” Kwa sababu gani basi, Yehova alimruhusu Shetani abaki mbinguni kwa maelfu ya miaka na hata aje mbele Zake wakati fulani?​—U.S.A.

Maneno yanayozunguka mstari huo yaonyesha wazi kwamba Shetani ‘hakukaa’ na Yehova Mungu katika maana inayotajwa na mtunga zaburi Daudi. Katika zaburi ya tano, Daudi alionyesha matumaini katika nia ya Yehova ya kusikiliza sala yake. Halafu, akitoa sababu yake kwa hili, Daudi aonyesha haki ya Mungu, akisema hivi: “Maana huwi Mungu apendezwaye na ubaya; mtu mwovu hatakaa kwako.” (Zab. 5:3, 4) ‘Kukaa’ huko na Mungu kwamaanisha kuwa mgeni aliyekubaliwa katika nyumba au hekalu lake takatifu. (Linganisha Zaburi 15:1-5.) Hii ni wazi kutokana na maneno ya Daudi yaliyofuata. Akiitofautisha hali yake mwenyewe na wazoeao mabaya, ambao hawaruhusiwi ‘kukaa’ na Yehova, yeye asema hivi: “Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, nitaingia nyumbani mwako; na kusujudu kwa kicho, nikilielekea hekalu lako takatifu.”​—Zab. 5:7.

Shetani Ibilisi aliruhusiwa aendelee kuwamo mbinguni kwa maelfu ya miaka na nyakati fulani (kwa wazi kwa sababu fulani ya pekee) akaruhusiwa awepo katika kusanyiko la wana wa Mungu. (Ayubu 1:6, 7; 2:1) Lakini ilikuwa kwa sababu ya ulizo la adili tu lililohitaji kuamuliwa kwamba Yehova Mungu alimruhusu Shetani awepo mbinguni. Kama ilivyo wazi kutokana na kitabu cha Ayubu, Shetani alishikilia kwamba viumbe vyote vyenye akili vilikuwa vichoyo hasa navyo vingeonekana kuwa visivyoaminika kwa Mungu kama visingeelekea tena kupata faida ya vitu vya kimwili au ya kipekee kwa sababu ya kumtii Yeye. (Ayubu 2:4, 5) Ili ulizo hili la maana katika ulimwengu wote liamuliwe, Yehova Mungu alimruhusu Shetani ajaribu kuhakikisha dai lake. Hii ilimruhusu Shetani atumie maongozi yake ajaribu wana wengine wa kimalaika wajidaie uhuru wao, kwa njia hiyo akiwatia katika jaribu la uaminifu wao kwa Mungu.

Malaika wengi wakawa wasioaminika. Lakini wote hao wasioaminika, walipoteza vyeo vyao vya matumaini na daraka, ingawa walikuwa bado wakiruhusiwa kufika mbinguni. Walishushwa, wakatiwa kizuizini na kunyimwa mwanga zaidi wa kimungu. Kwa njia ya mfano hali hii inatajwa katika Yuda 6: “Malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.”

Hivyo malaika hawa wasioaminika walifukuzwa katika jamaa ya Mungu ya viumbe viaminifu vya kiroho. Wala hivyo wala mtawala wavyo, Shetani, hawakuendelea kukaa na Yehova Mungu kwa njia waliyokuwa wamefurahia kama wana wake watiifu. Ingawa vilikuwa na ruhusa kufika kwenye makao ya kimbinguni, sasa vilikuwa viumbe vilivyofukuzwa makwao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki