Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 3/15 kur. 126-131
  • Usiache ‘Kuizoea Kweli’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usiache ‘Kuizoea Kweli’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SI VYEPESI KUTEMBEA NURUNI
  • KUIZOEA KWELI KATIKA MWENENDO WETU WA KILA SIKU
  • KUIZOEA KWELI KWA KUANGALIA MASHIRIKA YETU
  • Nuru Kutoka kwa Mungu Huondoa Giza!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Fuata Nuru ya Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • “Kuzivaa Silaha Za Nuru”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • “Nuru Imekuja Ulimwenguni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 3/15 kur. 126-131

Usiache ‘Kuizoea Kweli’

“Tukisema: ‘Tunakuwa na ushirika naye,’ na hali twaendelea kutembea gizani, tunasema uongo wala hatuizoei kweli.”​—1 Yohana 1:6, NW.

1. (a) Nuru ni yenye ubora namna gani? (b) Ni nuru gani yenye ubora mwingi zaidi, na imetupasa tuioneje?

“MUNGU ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake.” (1 Yohana 1:5) Kweli hii ya maana sana imepaswa iwe kichocheo kwa watu wote wanaojaribu kuzoea kweli, kuishi kulingana na kanuni za haki. Ikiwa mtu yumo katika umoja na Mungu anatembea nuruni. Na lo! nuru ni yenye thamani namna gani! Kwa kweli, kama kusingalikuwa na nuru kutoka juani katika mbingu kusingekuwa na uhai duniani. Kila mmoja wetu aweza kuthamini ubora wa nuru tujikutapo kwa ghafula mahali penye giza tititi. Itikio la kwanza la mtu ni kuagiza taa iwashwe. Kwa hiyo mtu apatapo kufahamu kwamba Mungu ni nuru, tamaa yake imepaswa iwe kuwa katika ushirika au umoja na Mungu, Chanzo cha nuru yote ya kweli.

2. Ni ukosefu gani mzito wa nuru uliosemwa na Isaya uliopo leo?

2 Walakini, ulimwengu wetu umejawa na wanadamu wasiomjua Mungu nao hawataki kumjua mara nyingi. Ni kama vile Isaya alivyoandika karne nyingi zilizopita kwa uongozi wa Mungu: “Maana, tazama, giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu.” (Isa. 60:2) Hili si giza linaloletwa na ukosefu wa nuru ya jua lenye kuangaza mpaka duniani. Hili ni giza baya zaidi, giza linaloletwa na ukosefu wa nuru ya kiroho kutoka kwa Yehova Mungu, Baba wa mianga ya mbinguni.

3. (a) Ni nani mwenye kufanyiza giza hili, na Waefeso 6:12 yaelezaje washirika wake? (b) Mwenye kufanyiza giza la akilini ana kusudi gani, na mtume Paulo asema yeye amefaulu kupofusha nani?

3 Mwenye kufanyiza giza hili ndiye adui mkuu wa Mungu na nuru, Shetani Ibilisi, na washirika wake wa kishetani. Wanasemwa katika Waefeso 6:12 kuwa “wakuu wa giza hili, . . . majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” Kusudi lake Shetani na mashetani zake ni kuweka wanadamu gizani, wakiwa wametenganishwa na nuru ya Yehova Mungu. Kwa kadiri kubwa yaonekana kwamba wamefaulu kufanya hivi. Kwa uongozi wa roho takatifu, mtume Paulo alimwita Ibilisi “mungu wa taratibu hii ya mambo,” ambaye “amepofusha akili za wasioamini, ili mwangaza wa habari njema zenye utukufu juu ya Kristo, ambaye ni mfano wa Mungu, usipate kung’aa kwa kupenya.” ‘Kupofusha akili’ huku kunaleta giza la kiroho.​—2 Kor. 4:4. NW.

4. Kuna ushuhuda gani kwamba nuru itokayo kwa Mungu na Mwanawe imefikia wengi kati ya wanadamu katika historia yote ya mwanadamu?

4 Ujapokuwa uhakika wa kwamba watu wanaishi katika ulimwengu wa namna hiyo, hii haimaanishi kwamba nuru itokayo kwa Mungu na Mwanawe, ambaye ndiye “mfano wa Mungu,” na kwa hiyo yeye pia ni nuru, haifikii wengine kati ya wanadamu na hivyo kuwaweka huru na giza. (Yohana 8:12) Mungu wa nuru na Mwanawe wametoa nuru ya kweli kadiri ambavyo katika historia yote ya wanadamu kumekuwa na watu mmoja mmoja ambao wametembea nuruni wakawa na kibali na baraka ya Muumba. Sura ya kumi na moja ya Waebrania yataja wachache wa watu hao wa kabla ya nyakati za Kikristo. Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yasimulia historia ya mianzo ya Ukristo na kutuingiza katika siku za mwisho za karne ya kwanza, yakisimulia juu ya Kristo Yesu na wafuasi wake, waliotembea nuruni. Na ingawa tuna historia ndogo iliyoandikwa hasa kuwatambua wafuasi wa nuru katika karne zilizofuata kifo cha mitume na wanafunzi wa kwanza wa Kristo mpaka nyakati zetu za kisasa, hata hivyo, twahakikishiwa na mfano wa Yesu Kristo juu ya ngano na magugu kwamba wakati huo wote wangekuwako wale wanaotembea katika nuru ya Mungu, wakifuata Neno lake, Kitabu cha nuru. (Mt. 13:24-30, 36-43) Katika nyakati za kisasa, utimizo wa mfano wa ngano na magugu ufikiapo upeo, “wana wa ufalme” wanatukuzwa katika Ufalme uliosimamishwa, mabaki ambayo wangali duniani waking’aa “kama jua,” wakitoa nuru ya kiroho ili wengine waweze kukusanywa upande wa Mungu wa nuru wapate kuhifadhiwa wakati ujao.

SI VYEPESI KUTEMBEA NURUNI

5. Shetani na mashetani zake wametumia maarifa gani kuzuia watu wasione nuru ya Neno la Mungu?

5 Pigano la kuondoa watu katika nuru ya Neno la Mungu wasitembee katika nuru ya Mungu ni vita kali inayopigwa na mamlaka za giza, Shetani, mashetani zake na tengenezo lake la kidunia lionekanalo. (1 Yohana 5:19) Mara nyingi kuna vizuizi vyote viwezavyo kuwapo kwa wale wanaoiona nuru vikiwa vimewekwa katika njia yao kuwafanya wajikwae na kwa hiyo waendelee kuwamo gizani. Huenda ukawa ni mkazo kutoka kwa jamaa wapingao kweli. Huenda yakawa ni mashaka juu ya ukweli wa Neno la Mungu, kwa sababu ya kupofushwa kwa mtu kwa muda mrefu sana na mafundisho ya uongo ya mamlaka za kidini za giza. Huenda ukawa ni mkazo kutoka kwa washiriki alio nao mtu au maelekeo yenye dhambi ya mtu mwenyewe yanayofanya iwe vigumu kuishi kulingana na matakwa ya kimungu waliyowekewa watoto wa nuru.

6. (a) Mtu aweza kupatwa na nini hata baada ya kuwekwa huru na utumwa kwa giza? (b) Yatupasa tuangalie maulizo gani?

6 Hata baada ya mtu kujiweka huru na uongozi wa mamlaka za giza na kuingia nuruni anakabili mashambulio yenye kuendelea kutoka kwa taratibu hii ya mambo. Kwa hiyo huenda nyakati nyingine ikawa vigumu kwa wengine ‘kuizoea kweli,’ lakini imewapasa wajihadhari wasije wakarudia njia yao ya zamani ya maisha. Mtume Yohana aliandika hivi: “Tukisema: ‘Tunakuwa na ushirika naye,’ na hali twaendelea kutembea gizani, tunasema uongo wala hatuizoei kweli.” (1 Yohana 1:6, NW) Kweli, nyakati nyingine sote tunapungukiwa, lakini ni mambo gani tuzoeayo? Je! wengine wetu wanatembea gizani badala ya nuruni, ingawa twajidai tumetoka katika giza la ulimwengu huu tukaingia nuruni? Je! tunazoea kweli kabisa, au mfano wetu wa maisha waonyesha kwamba tunaacha, tukijidanganya wenyewe, tukijiambia uongo?​—1 Yohana 1:8–2:2.

7. Ni kujichunguza gani kuliko kwa lazima, nako kumepaswa kufanywe juu ya msingi gani?

7 Kujichunguza ni kwa lazima katika shauri hili, kutumia Neno la Mungu kama kiongozi cha mambo anayopaswa mtu kuwa akifanya ikiwa anazoea kweli, kutembea nuruni. Kujichunguza huku kunaingia katika maeneo kadha ya lazima, maeneo ambamo kila mmoja wetu amepaswa apendezwe. Imetupasa tujichunguze hivyo, tukiyakumbuka maneno ya mtume Paulo alipokuwa akisema na kundi la Korintho: “Kwa kuwa hatuthubutu kujihesabu pamoja na baadhi yao wanaojisifu wenyewe, wala kujilinganisha nao; bali wao wenyewe wakijipima nafsi zao na nafsi zao, na wakijilinganisha nafsi zao na nafsi zao, hawana akili.” (2 Kor. 10:12) Kujichunguza kwetu kumepaswa kufanywe juu ya msingi wa Kitabu cha nuru, Neno la Mungu. Paulo aliendelea kusema hivi: “Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake. Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.” (Gal. 6:3, 4) Neno la Mungu na limwonyeshe kila mtu mmoja mmoja anayohitaji Mungu kwa wale wasemao ‘wanaizoea kweli.’ Na tusiwe tukijipima kulingana na mwanadamu mwingine, au kulingana na kanuni za kibinadamu.

KUIZOEA KWELI KATIKA MWENENDO WETU WA KILA SIKU

8. Katika barua yake kwa Waefeso, mtume Paulo alishauri mtu aepuke nini?

8 Mtume Paulo aliandika maneno haya kwa kundi lililokuwamo Efeso: “Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msienende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao; ambao akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao; ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.”​—Efe. 4:17-19.

9. Ni kanuni gani za ulimwengu leo zionyeshazo kwamba akili nyingi zimo gizani?

9 Kanuni za ulimwengu huu, kanuni zao za adabu, ndizo zimetokeza akili zilizomo gizani, zilizotenganishwa na uzima ulio wa Mungu. Kwa sababu hiyo ulimwengu wasema, “Fanya lako mwenyewe,” ikimaanisha kwamba mtu ni mtunga sheria kwake mwenyewe, bila ya kufanyiwa sharti na orodha nyingine yo yote ya sheria au kanuni ambayo ingepunguza uhuru wake. Kanuni hii yaruhusu mtu awe mpumbavu moyoni mwake. Usemi unakuwa, “Lo lote lafaa.”

10, 11. Ni nani wamo kati ya wale waliomo gizani kwa akili, na kwa sababu gani?

10 Viongozi wengi wa dini wa Kristendomu wamo kati ya wale waliomo gizani kwa akili waungao mkono kanuni hizo za kilimwengu. Badala ya kutia watu moyo wazoee kweli, wanaridhishwa na mikazo ya mataifa na watu wenye vyeo vikubwa wanaoachilia mwenendo mbaya. Ili kutegemeza maneno haya, angalia aliyosema kasisi wa chuo kikuu katika United States juu ya uzinzi: ‘Maisha kamili yaweza kupatikana wakati mwanamume​—na mkewe, pia​—wako huru kufanya mambo [uzinzi] nje ya ndoa, si kwa siri, bali kila mmoja wao akijua na kukubali.’ Kasema hivi kiongozi wa dini wa San Francisco katika gazeti la kila juma la Episcopal Church: “Hakuna ngono iliyo yenye dhambi yenyewe. . . . Mimi naamini pia kwamba watu wawili wa namna ile ile (mwanamume na mwanamume au mwanamke na mwanamke) wanaweza kuonyeshana upendo na kuzidisha upendo huo kwa ngono [ulawiti].”

11 Giza hili la akili linafikia pia mambo ya kujifurahisha. Na, kwa kweli, wale waliomo katika mambo hayo ndio watunga mashauri, au wenye kuweka mitindo kwa kizazi hiki. Si jambo lisilo la kawaida kusoma magazetini juu ya wanaume na wanawake wanaoishi pamoja, na kuzaa watoto nje ya kifungo cha ndoa, bila ya kuonea uasherati huo aibu yo yote. Kwa kweli, wowote ambao wangeteta mara nyingi wanaibishwa kama wenye haya mno, wasiofanya mambo ya nyakati za kisasa. Maonyesho katika radio na televisheni yanawaonyesha watu hawa wenye sifa isiyo njema mara nyingi kama wenye kipindi chenye kuvutia zaidi. Wanapenda kufanya maisha zao kitabu kilicho wazi wote wakisome na kukiona, kana kwamba walikuwa wanajaribu kwa njia yo yote iwezekanayo kushtua wenye adabu za kawaida. Hawajui sana kwamba wao wenyewe ndio watakaoshtuka siku zijazo watakapokuwa wakivuna wanachopanda kwa sababu ya mwenendo wao mpotovu.

12. Ni maelezo gani ya wale waliomo katika giza la akili yanayotolewa katika Warumi 1:24-27?

12 Mtume Paulo alisimulia vema mtu wa namna hii katika barua yake kwa Warumi alioishi chini ya hali kama hizi miaka kumi na tisa iliyopita. Alisema hivi: “Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao. Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidwa milele. . . . Hivyo Mungu aliwaacha afuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.”​—⁠Rum. 1:24-27.

13. Paulo anaielezaje akili na moyo wa walimwengu wajinga?

13 Katika barua yake kwa Waefeso, Paulo alisema kwamba watu wa namna hiyo “akili zao zimetiwa giza, . . . kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.” Tena, katika barua kwa Warumi, Paulo alisema kwamba watu hao ni ‘waliopotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.’ (Efe. 4:18; Rum. 1:21) Angalia kwamba katika mifano yote hii miwili hao hawashirikishwi na nuru, bali na giza, na ukosefu wa nuru na ufahamu.

14. Onyesha yanayotokana na wale waliomo gizani ‘waliopotea katika uzushi wao,’ kulingana na Warumi 1:28-32?

14 Paulo aliendelea kuonyesha matokeo zaidi ya ujinga huo, akisema: “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.”​—Rum. 1:28-32.

15. Eleza ugumu wa wale wanaotaka kutembea nuruni.

15 Namna hizi za watu ‘hawaizoei kweli,’ kama ilivyosemwa na mtume Yohana, bali ‘wanazoea mambo yastahiliyo mauti,’ nayo dunia hii imejawa na watu wa namna hiyo kwa sababu ya ‘mamlaka ya giza.’ Ugumu unaowakabili wale wanaotaka kutembea nuruni, wawe katika umoja na Chanzo cha nuru na Mwanawe, Bwana Yesu Kristo, kwa ufupi, kuizoea kweli, ni namna ya kuendeleza usawa ufaao wa akili katikati ya giza liwazungukalo na kutoshawishwa watoke katika njia ya nuru. Basi, ni nini kinachohitajiwa kwao waendeleze usawa ufaao wa akili, ili wasishawishwe?

16. (a) Eleza maana ya ‘kutembea nuruni.’ (b) Twaepukaje kufikiri kubaya na matendo mabaya, na ni maisha ya nani yaliyo kitia moyo katika upande huu?

16 Ikiwa tutaizoea kweli lazima tuwe ‘tunatembea nuruni.’ (1 Yohana 1:7, NW) Ili kutembea nuruni lazima tuzidi kulitii shauri tunalopewa na Mungu wa nuru na kusitawisha upendo kwa njia zake. Tukifanya hivyo, basi tuionapo taratibu hii ya mambo ikikubali kanuni zinazokatazwa na Mungu wa nuru, Yehova, hatutajiacha tuufikirie sana unaoelekea kuwa uradhi wa mwendo huo. Hatutafikiria namna ambavyo ingekuwa vizuri kufurahia anasa hizo kwa kitambo tu, tukiona kwamba kidogo kanuni hizo za chini zaidi za ulimwengu zina sifa fulani zinazosawazisha makosa yake. Hatutajidanganya tufikiri kwamba, ingawaje, kitambo cha raha chaweza kustahilisha kuvunja kanuni za nuru. Bali, tutamwomba Mungu na kujaribu kufuata kanuni za haki, tunapoizoea kweli. Kwa mfano, tunapotazama Biblia twaona maisha ya mtumishi wa Yehova Musa yameandikwa. Imeandikwa juu yake kwamba alikataa kuitwa mwana wa binti Farao, “akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo.” Musa aliwezaje kufanya hili? Maandishi yasema, “akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.” (Ebr. 11:24-26) Hiyo ndiyo maana ya kuizoea kweli. Hiyo ndiyo maana ya kutembea nuruni.

KUIZOEA KWELI KWA KUANGALIA MASHIRIKA YETU

17. Kuna ukamatano gani kati ya kuizoea kweli na kuangalia mashirika yetu?

17 Bila shaka wengi wenu mnaosoma habari hii mmesikia semi hizi, ‘Niambie rafiki zako ni nani nami nitakuambia wewe u mtu wa namna gani,’ na, ‘Watu wa tabia moja hutembea pamoja.’ Semi zote hizi mbili zina maana ya kwamba unafanana sana na wale unaoshirikiana nao. Mtu akitafuta ushirika wa wale wa ulimwengu huu uliotiwa giza wanaopendezwa na kufanya watakavyo tu, bila kufikiria matakwa ya maisha manyofu yanayoelezwa katika Biblia, basi yaelekea kwamba ataona si vigumu kujitambua na ushirika huo na kuwa kama wao. Onyo la Biblia juu ya jambo hili ni, “Mashirika mabaya yanaharibu mazoea mazuri.” (1 Kor. 15:33, NW) Hivyo kila mtu anayetaka kuzoea kweli lazima ajiulize kwa unyofu wote kama wale anaoshirikiana nao wanamsaidia kutembea nuruni au wanazuia maendeleo yake katika kumtumikia Mungu wa nuru.

18. (a) Ikiwa tengenezo la kidini laachilia wahudumu watiao moyo ufisadi ufanywe, kwa sababu gani uhakika wa kwamba si kila mtu tengenezoni azoeaye maisha mapotovu usingekuwa sababu ya kwamba mtu anayeizoea kweli aweza bado kujitambulisha na tengenezo hilo? (b) Basi, wale wazoeao kweli lazima wawe wapi?

18 Katika kuwaza kwa kidini, je! inapatana kwa mtu asemaye kwamba ataka ‘kutembea nuruni’ kushirikiana pia na tengenezo la kidini liachilialo ziitwazo kanuni za adabu za taratibu hii? Tengenezo la kanisa likiruhusu mmoja wa wahudumo wake ahubiri jukwaani akiunga mkono uzinzi, ulawiti, na namna nyingine za maisha mapotovu, mtu anayejaribu kujifunza njia ya Mungu ili atembee katika njia ya nuru angewezaje kuendelea kushirikiana na tengenezo hilo? Si kitu hata kama wengine katika tengenezo la kanisa hilo hawazoei mambo hayo, huku wengine wakifanya hivyo. Tengenezo hilo lingali linaachilia mtu aaminiye na kuhubiri yaliyo tofauti na mapenzi ya wazi ya Mungu wa nuru. Shauri la Paulo juu ya mtu mfisadi katika kundi la Korintho la karne ya kwanza lilikuwa hili: “Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.” (1 Kor. 5:13) Kwa hiyo wale wanaotaka kupata kibali ya Yehova Mungu na kuzoea kweli lazima wafuate onyo la upole la Ufunuo 18:4, lisemalo hivi juu ya Babeli Mkuu wa kidini “Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” Ndiyo, hapo ndipo inawapasa wote wazoeao kweli na kutembea nuruni wawe nje kabisa ya matengenezo ya uongo ya kidini ya Babeli Mkuu!

19. Mtu ataangaliaje mashirika yake katika mambo ya kujifurahisha, na kwa hiyo ni uchaguzi gani unaokuwa wa lazima?

19 Bila shaka, lazima mtu aangalie pia anashirikiana na nani katika mambo ya kujifurahisha. Ingawa huenda ushirika hapa usiwe wa kipekee sana​—watu walio wengi hawashirikiani moja kwa moja na wale waliomo katika ulimwengu wenye kujifurahisha​—hata hivyo yampasa mtu aangalie mazoea yake katika usomaji wa vitabu na magazeti yanayofuata kanuni mbovu ya ulimwengu huu, au katika kutazama sinema na televisheni zinazotukuza na kusifu mambo yanayokatazwa na Neno la Mungu, kama yale yanayoelezwa katika kitabu cha Warumi, yaliyotajwa mapema. Mtu hawezi kutembea katika nuru ya Mungu huku akishirikiana na wale wa jamii hii mbovu yenye ugonjwa ikubaliyo kila jambo ambalo Mungu wa nuru achukia sana. Ni juu ya kila mtu kuchagua watu atakaoshirikiana nao, lakini uamuzi wa kama mtu huyo anaizoea kweli ni juu ya Yehova Mungu. Kumbuka kwamba haya ndiyo maneno ya 1 Yohana 1:6, NW: “Tukisema: ‘Tunakuwa na ushirika naye,’ [yaani, na Mungu wa nuru] na hali twaendelea kutembea gizani, tunasema uongo wala hatuizoei kweli.” Maana i wazi na ni yenye nguvu. Ni wajibu wa Wakristo wote, wafuasi wa Bwana, Yesu Kristo, kulitii shauri la Neno la Mungu na kuongoza maisha zao kulingana na shauri hilo.

20. Taja mambo mengine ya lazima ambayo lazima mtu ayaangalie linapokuwa shauri la kuizoea kweli.

20 Lakini mengi zaidi yahusika katika kuzoea kweli kuliko kuangalia mwenendo wetu wa kila siku na kushirikiana na watu wafaao. Kuizoea kweli kwatuhitaji tuangalie mambo mengine ya lazima. Kwa mfano, mtu azoeaye kweli auonaje ushirika na wale wenye imani ile ile yenye thamani sana katika mikutano ya kundi? Kama jambo la lazima, au kama jambo la kufanya wakati tu mtu hana jambo bora la kufanya? Na namna gani kushiriki katika kuwaeleza wengine juu ya Mungu wa nuru na juu ya Mwanawe, ambaye ndiye nuru ya ulimwengu? Je! mtu aweza kuizoea kweli asiwe mwenye nia na tamaa ya kueleza wengine baraka zilizo akibani kwa wanadamu kama ilivyoelezwa mapema kwa unabii katika Neno la Mungu? Halafu kuna shauri la kusaidia wale wa nyumba ya imani, wale wanaoshiriki sasa katika kuizoea kweli katika kundi la Kikristo. Je! kuzoea kwetu kweli kwahusuje uhusiano huu na madaraka yake? Ili mtu awe na ushirika na Yehova Mungu wa nuru na Mwanawe, ili aweze kusema kwa kweli anaizoea kweli wala hatembei gizani, anahitajiwa atimize matakwa fulani ya msingi. Haya yanazungumzwa katika makala ifuatayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki