Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 1/15 kur. 27-29
  • Matokeo Mazito ya Kuwaza Kubaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matokeo Mazito ya Kuwaza Kubaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MTUMWA ASIYETHAMINI MAMBO
  • MTUMWA MLEGEVU WA KISASA
  • KUTAKA HESABU
  • HATARI KWA WOTE WANAOSITAWISHA NIA MBAYA
  • Kielezi cha Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Somo Kuhusu Bidii​—Talanta
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Jifunze Kutokana na Mfano wa Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 1/15 kur. 27-29

Matokeo Mazito ya Kuwaza Kubaya

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1-3. Mtu anayeweza vibaya hasa juu ya mambo ya Mungu aweza ndani ya matendo gani yenye hatari?

KWA kawaida ni hatari kuwa na maoni mabaya, na ni hatari hasa wakati mtu ana maoni yasiyofaa juu ya mambo ya Mungu. Mtu aliye na maoni yasiyofaa aweza kufuata kuwaza kwenye ukali na aweza kweli kuwa mwovu.

2 Mtu huyo kwa kawaida ni mvivu pia, akifanya machache sana. Ili kuepuka kufanya jambo mwenye kuwaza kubaya, mtu mvivu, atatoa udhuru wa kutetea mwendo wake. “Mtu mvivu husema, Simba yuko nje; nitauawa katika njia kuu.”​—Mit. 22:13.

3 Juu ya matokeo ya mtu huyo, Biblia yasema: “Nalipita karibu na shamba la mvivu, na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili [au, kusudi jema]. Kumbe! lote pia limemea miiba; uso wake ulifunikwa kwa viwawi; na ukuta wake wa mawe umebomoka. Ndipo nilipoangalia na kufikiri sana; naliona, nikapata mafundisho. Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono upate usingizi! Hivyo, umaskini wako huja kama mnyang’anyi, na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.”​—Mit. 24:30-34.

4. Shauri lililomo katika Mithali linatumikaje kwa njia ya kiroho kama lilivyotajwa katika mafungu ya pili na tatu?

4 Mithali zina matumizi ya kiroho na ya halisi vile vile. Watu kama ambao Mithali zinawasimulia huenda kwanza walikuwa na roho na nia ifaayo, lakini ndipo walipositawisha maoni mabaya juu ya matendo yenye haki. Kwa hiyo inahitaji tuwe waangalifu kwa upande wetu kuepuka kusitawisha roho hiyo ya kusikitisha.​—Mit. 4:23.

MTUMWA ASIYETHAMINI MAMBO

5. Je! bwana wa watumwa alimtia mtumwa wa tatu chini ya kizuizi kwa kumpa talanta moja tu wakati wengine walipopokea zaidi?

5 Mtu kama huyo mwenye maoni mabaya, au jamii hiyo ya watu, inasimuliwa katika mfano wa Yesu wa “talanta.” Katika matoleo yaliyotangulia tumewazungumza watumwa waaminifu wawili wanaotajwa katika mfano, waliopokea talanta tano na talanta mbili, kila mtu kwa kadiri yake. Mtumwa wa tatu alipokea talanta moja (talanta moja ikiwa ni sehemu moja ya fedha). Lakini, kwa kuwa bwana wake alimpa kila mmoja “kwa kadiri ya uwezo wake,” huyu mtumwa wa tatu hakuwa chini ya kizuizi cho chote. Wale watumwa wengine walileta faida ya kiasi cha 100 kwa mia kila mmoja juu ya pesa walizokabidhiwa wakati bwana wao alipokuwa ameondoka. Mtumwa mwenye talanta moja angaliweza kufanya vivyo hivyo na kwa njia hiyo ampendeze bwana wake; haikuwa lazima apate faida ya talanta tano, au hata talanta mbili.

6. Kwa sababu gani mtumwa mwenye talanta moja alifanya alivyofanya, naye alitoa udhuru gani?

6 Lakini yeye alifanya nini? Mfano wasema hivi: “Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.” (Mt. 25:18) Kushindwa kwake kuleta ongezeko lilikuwa kosa lake mwenyewe; yeye hakujitahidi kama watumwa wenzake. Wakati bwana wake aliporudi kutaka hesabu, huyo alitoa udhuru gani? Alilalamika hivi: “Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya; basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.”​—Mt. 25:24, 25.

7. Mtumwa huyu alijaribuje kujitetea?

7 Kwa kuwaza kwake kubaya mtumwa huyu alijaribu kujitetea wakati hesabu ilipofanywa. Alijaribu kumsingizia ubaya bwana wake. Alimshtakia bwana wake kupata mavuno, si kutoka katika ardhi yake mwenyewe tu, bali pia kutoka katika ardhi ambayo hakuwa amelima, na kukusanya nafaka asiyotawanya makapi yake. Kuwaza kwake kwa uongo kulikuwa kwamba bwana wake hakupata hasara yo yote kwa sababu ya tendo lake​—ingawaje, aliirudisha ile talanta moja. Lakini mtumwa huyu alikuwa asiyeaminika, kwa sababu aliikubali fedha kama mtumwa kwa ufahamu wa kwamba imepaswa ilete faida. Bila shaka alizikubali faida zote zilizohusika katika kuwa mtumwa wa bwana wake, lakini hakumpenda bwana wake wala hakuzifikiria mali za bwana wake. Kwa kweli alimhasirisha bwana wake.

8. Bwana aliutumiaje udhuru wa mtumwa mwenyewe kumlaani?

8 Bwana wa mtumwa alimpindukia, akiuchukua udhuru wa mtumwa mwenyewe uliotungwa kwa uongo na kuutumia kumpasisha hukumu: ‘Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya; basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.’​—Mt. 25:26, 27.

MTUMWA MLEGEVU WA KISASA

9. Ni nini kilichofananishwa na mtumwa asiyeaminika?

9 Tumeona katika makala zilizotangulia kwamba wale watumwa waaminifu wawili wanawafananisha ndugu waaminifu waliozaliwa kwa roho wa Bwana Yesu Kristo katika utimizo. Basi, mtumwa mwovu angefananisha wale waliozaliwa kwa roho vile vile, Wakristo waliotiwa mafuta, lakini wanaoshindwa hasa kuziangalia “mali” walizokabidhiwa “watumwa” na Bwana wao.

10. Je! makanisa ya Kristendomu yamelima shamba la ulimwengu kwa ajili ya Bwana wanayejidai kumfuata?

10 Washiriki wenye kugawanyika katika madhehebu wa makanisa ya Kristendomu wamejidai kwa uongo kuwamo katika utumishi wa Bwana. Lakini hawakuonyesha kupendezwa ko kote na “mali” za Bwana wakati Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, ambamo walikuwa wameshiriki, ilipokwisha, nayo nafasi ya kuzihubiri habari njema za Ufalme ulimwenguni pote ilikuwako. Badala yake, walifanya nini? Waliunga mkono Ushirika wa Mataifa, uwakili ulioundwa na wanadamu ambao Federal Council of the Churches of Christ in America iliuita “wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani.” Sasa wanaelekeza fikira za watu na tegemezo kwenye Umoja wa Mataifa kama tumaini la ulimwengu kwa amani. Walionyesha hawakuwa wamekabidhiwa “mali” za Bwana, kwa maana hawakulima shamba la ulimwengu na kutokeza wafuasi wa kweli wa ufalme uliosimamishwa wa Kimasihi.​—Isa. 9:6, 7.

11, 12. Ni nani anayelingana hasa na mfano wa mtumwa mwovu aliye mlegevu, na kwa njia gani?

11 Walakini, ilikuwamo jamii iliyojitenga kwa ulegevu kati ya wale waliozaliwa kwa roho walioshirikiana na jamii ya “mtumwa mwaminifu.” Kufikia 1931, wakati jina “mashahidi wa Yehova” lilipochaguliwa na mabaki ambao hasa walikuwa wakiifanya kazi ya kuutangaza ufalme wa Mungu uliosimamishwa, hawa wenye maoni mabaya walikuwa wamekwisha jifanyizia vikundi mbalimbali vyenye majina mbali-mbali. Wao hawakuutangaza Ufalme kwa ujasiri wala kulitetea jina la Mungu Mwenye Nguvu Zote, Yehova. Zaidi ya hayo, kwa kweli wao walipinga kufanya kazi hii. Hawakupatwa na mateso ya kuogofya waliyopatwa nayo mashahidi wa Yehova katika kambi za mateso, na pia mateso katika sehemu nyingine za dunia. Wanalingana na mfano huu!

12 Jamii hii isiyoaminika haina uhakikisho wo wote wa kwamba wameongeza “mali” za Bwana kwa kuueneza ujumbe wa Ufalme. Hawakuzipata baraka za mpanuko mkubwa sana. Bali katika miaka ya 1968-1972, watu 680,871 walibatizwa, wakajiunga na mashahidi wa Yehova kuutangaza Ufalme kwa wengine. Ushuhuda upo wa kuonyesha wanaobarikiwa na Yehova Mungu. Walio waaminifu hawaamini, kama yule “mtumwa” mwovu alivyodai, kwamba Yesu Kristo anavuna isivyo haki ambapo yeye mwenyewe, alipokuwa duniani mwenyewe, hakupanda.

KUTAKA HESABU

13, 14. Mtumwa asiyeaminika alipokea adhabu gani kutoka kwa bwana wake?

13 Iangalie adhabu aliyoipokea “mtumwa” mwovu na mlegevu kutoka kwa bwana wake kwa sababu ya kuwaza kwake kubaya, kuogopa kwake na uvivu, na jitihada yake ya kutetea mwendo mbaya. Bwana wake alisema hivi: “Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi. Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa. Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.”​—Mt. 25:28-30.

14 Kwa wazi bwana alitaka hesabu kwa watumwa wake wakati wa usiku. Badala ya kuingia katika furaha ya bwana wake, mtumwa mwovu alitupwa nje. Mali za bwana alizokabidhiwa, asizozithamini, ziliondolewa kwake na kupewa kwa mtumwa aliyekuwa amepata faida ya talanta tano, ambapo thamani hizi za fedha zingeongezwa.

15. Ni nini matokeo kwa jamii ya “mtumwa” mwovu, watiwa mafuta wanaokuwa wasioaminika na wale wanaojidai kuwa watumwa?

15 Katika utimizo, twaweza kuona kwamba “watumwa” wote wa Kristo waliotiwa mafuta wanapewa onyo. Wale wa jamii ya “mtumwa” mwovu hawaingii katika furaha ya Bwana wao aliyetawazwa, kwa kuwekwa katika utumishi wake wa kifalme zaidi hapa duniani kama wajumbe wa Ufalme uliokwisha simamishwa. Huyu mtumwa mlegevu hafurahii mgawo zaidi kuongezea wafuasi wa Ufalme. Wakati giza lenye kufisha la “dhiki kubwa” litakapowajilia wanadamu waliomo katika jamii hii watalia na kusaga meno yao pamoja na wanafiki wa kidini mpaka watakapotoweka.​—Mt. 24:21.

16. Ni bidii gani inayoamshwa katika jamii ya “mtumwa” mwaminifu isiyo nayo jamii ya “Mtumwa” mwovu aliye mlegevu?

16 “Watumwa” waaminifu wanacho kile ambacho “mtumwa” mwovu na mlegevu hanacho. Kabidhi ya “mali” yenye thamani nyingi za Mfalme anayetawala na nafasi yao ya kuongezea “mali” hizi inaamsha ndani yao bidii na uaminifu kwa ufalme wake. Wanauamini ustahili wa Bwana wa kimbinguni wa kupokea ongezeko kwa kufanya wanafunzi. Wanaonyesha kusudi la upendo, la ushujaa kwa kufanya wanafunzi kati ya watu wa mataifa yote, si taifa la Kiyahudi tu ambamo Kristo alifanya kazi alipokuwa duniani.

HATARI KWA WOTE WANAOSITAWISHA NIA MBAYA

17. Ni ulinganifu gani unaoweza kuonwa juu ya “mkutano mkubwa” kama onyo kwao pia?

17 Hata wale wa “mkutano mkubwa,” walio na tumaini la kuishi duniani wakiwa wenye afya na uzima chini ya serikali ya Ufalme, wanayo nia ile ile kama “watumwa” waliotiwa mafuta wa Bwana Yesu Kristo, wanaoshirikiana nao. Wanaonyesha fadhili za upendo, shukrani, ushujaa na bidii kwa neno na tendo wanapokuwa wasaidizi wa jamii nyaminifu iliyotiwa mafuta. Wanajua kwamba kuwaza kubaya, kujitenga, kuwa wakali na kutoa udhuru wajitetee kutawatia katika hali inayolingana na ile ya “mtumwa” mwovu aliye mlegevu. Hali hii ingewazuia wasiokoke duniani kupita “dhiki kubwa.” Zaidi ya hayo, wo wote kati yao wanaokufa kama wasioaminika hawatafufuliwa waishi katika paradiso itakayoletwa duniani na utawala wa Ufalme.​—Ufu. 7:9-17; Sef. 2:3.

18. Matokeo yatakuwa nini kwa mtu anayeendelea kuwa na kuwaza kubaya juu ya mambo ya Yehova?

18 Hivyo twaweza kuona hatari ya kuwa na maoni mabaya juu ya mambo ya Bwana. Katika huu wakati wa hukumu hataruhusu wo wote walio wavivu au wenye kulaumu-laumu waendelee kushirikiana na watu wake waaminifu. Hali yao itakuwa kama ile aliyoiona mwandikaji wa Mithali​—iliyoharibika, yenye kuzaa magugu, hata watapoteza nafasi yao ya kazi katika makundi ya Bwana, ‘umaskini wao ukija kama mnyang’anyi na uhitaji wao kama mtu mwenye silaha,’ kwa ghafula. Wenye furaha ni wote wenye kuwaza ifaavyo, kwa imani na uaminifu kwa amri za Yehova kupitia kwa Kristo leo!

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki