Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 5/1 kur. 8-9
  • Kielezi cha Talanta

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kielezi cha Talanta
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Somo Kuhusu Bidii​—Talanta
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Jifunze Kutokana na Mfano wa Talanta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kufanya Hesabu Juu ya Matumizi ya Hazina za Kristo
    Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
  • Matokeo Mazito ya Kuwaza Kubaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 5/1 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Kielezi cha Talanta

YESU aendeleza mazungumzo pamoja na mitume wake katika Mlima wa Mizeituni kwa kuwaambia kielezi kingine, cha pili katika mfululizo wa vitatu. Siku chache baadaye, alipokuwa Yeriko, alisimulia kielezi cha mina kuonyesha kwamba Ufalme ulikuwa ungali mbali katika wakati ujao. Ingawa kielezi ambacho asimulia sasa kina sehemu kadhaa zenye kufanana, chaeleza katika utimizo wacho utendaji mbalimbali wakati wa kuwapo kwa Kristo katika mamlaka ya Ufalme. Chatoa kielezi kwamba ni lazima wanafunzi wake wafanye kazi wakiwa wangali duniani ili kuongezea “mali zake.”

Yesu aanza hivi: “Kwa maana hiyo [yaani, hali zenye kuhusiana na Ufalme] ni kama wakati mtu, akiwa karibu kusafiri ng’ambo, aliita watumwa wake na kuwakabidhi mali zake.” Yesu ndiye mtu ambaye, kabla ya kusafiri ng’ambo mbinguni, akabidhi watumwa wake—wanafunzi walio katika mstari wa kupata Ufalme wa kimbingu—mali zake. Mali hizi si mali za kimwili bali huwakilisha shamba lililolimwa ambamo yeye amejenga uwezekano wa kutokeza wanafunzi zaidi.

Yesu akabidhi mali zake kwa watumwa wake muda mfupi kabla ya kupaa mbinguni. Jinsi gani? Kwa kuwaagiza waendelee kufanya kazi katika shamba lililositawishwa kwa kuhubiri ujumbe wa Ufalme kwenye sehemu za mbali kabisa za dunia. Ni kama vile Yesu asema: “Alimpa mmoja talanta tano, mwingine mbili, mwingine bado akampa moja, kila mmoja kulingana na uwezo wake mwenyewe, naye akaenda ng’ambo.”

“Baada ya muda mrefu,” Yesu aendelea kusema, “bwana-mkubwa wa watumwa hao alikuja akafanya hesabu nao.” Haikuwa mpaka karne ya 20, yapata miaka 1,900 baadaye, kwamba Kristo akarudi kufanya hesabu, kwa hiyo, kwa kweli, ilikuwa “baada ya muda mrefu.” Ndipo Yesu aeleza hivi:

Hivyo hizo talanta nane—mali za Kristo—zagawanywa kulingana na kadiri za uwezo, au kadiri za uwezekano wa kiroho, za watumwa. Watumwa hao wasimamia jamii za watumwa. Katika karne ya kwanza, jamii iliyopokea talanta tano kwa wazi ilitia ndani mitume. Yesu aendelea kusimulia kwamba watumwa wote wawili waliopokea talanta tano na mbili walizirudufisha kwa kuhubiri kwao Ufalme na kufanya wanafunzi. Hata hivyo, mtumwa aliyepokea ile talanta moja aliificha katika ardhi.

“Mmoja aliyekuwa amepokea talanta tano akaja mbele na kuleta talanta tano za ziada, akisema, ‘Bwana-mkubwa, wewe ulinikabidhi talanta tano; ona, nilipata talanta tano zaidi.’ Bwana-mkubwa wake akamwambia, ‘Vema, mtumwa mwema na mwaminifu! Wewe ulikuwa mwaminifu juu ya vitu vichache. Mimi nitakuweka juu ya vitu vingi. Ingia ndani ya shangwe ya bwana-mkubwa wako.’” Vivyo hivyo mtumwa aliyepokea talanta mbili alirudufisha talanta zake, na alipokea pongezi na thawabu ile ile.

Ingawa hivyo, hawa watumwa waaminifu huingiaje ndani ya shangwe ya Bwana-mkubwa wao? Basi, shangwe ya Bwana-mkubwa wao, Yesu Kristo, ilikuwa ile ya kupokea umiliki wa Ufalme alipoenda ng’ambo kwa Baba yake mbinguni. Kwa habari ya watumwa waaminifu katika nyakati za ki-siku-hizi, wao wana shangwe kubwa katika kuamanishwa madaraka zaidi ya Ufalme, na wanapokuwa wakimaliza mwendo wao wa kidunia, watakuwa na shangwe ya upeo ya kufufuliwa kwenye Ufalme wa kimbingu. Lakini namna gani juu ya mtumwa wa tatu?

“Bwana-mkubwa, nilikujua wewe kuwa mtu mwenye kutoza sana,” mtumwa huyu alalamika. “Kwa hiyo mimi niliogopa nikaenda na kuficha talanta yako katika ardhi. Hii hapa chukua kilicho chako.” Mtumwa huyo alikataa kimakusudi kufanya kazi katika shamba lililositawishwa kwa kuhubiri na kufanya wanafunzi. Kwa hiyo bwana-mkubwa amwita “mwovu na goigoi” na kutamka hukumu: “Mpokonyeni talanta . . . na mmtupe mtumwa asiyefaa kitu nje ndani ya giza la nje. Huko ndiko kutakuwako kilio chake na kusaga meno yake.” Wale wa jamii hii ya mtumwa mwovu, kwa kutupwa nje, hunyimwa shangwe yoyote ya kiroho.

Hii hutokeza somo zito kwa wote ambao hudai kuwa wafuasi wa Kristo. Ni lazima wafanye kazi ili kuongezea mali za Bwana-mkubwa wao wa kimbingu kwa kuwa na ushiriki kamili katika kazi ya kuhubiri ikiwa wataona shangwe ya kupongezwa na kuthawabishwa naye na ikiwa wataepuka kutupwa ndani ya giza lililo nje na uharibifu wa hatimaye. Je! wewe u mwenye bidii ya uendelevu kutumia uwezo wako mbalimbali katika habari hii? Mathayo 25:14-30, NW.

◆ Kielezi hiki kifuatacho chafundisha somo gani?

◆ Watumwa ni nani, na mali wanazoamanishwa ni nini?

◆ Ni wakati gani bwana-mkubwa aja kumaliza hesabu, naye apata nini?

◆ Ni shangwe gani ambamo mtumwa mwaminifu anaingia, na mtumwa mwovu apatwa na nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki