Biblia Zaidi na Vitabu vya Kusaidia Kujifunza Biblia
● Biblia inapatikana sasa yote au sehemu yake, katika lugha 1,526, kulingana na mashirika ya United Bible Societies. Ilitokea katika lugha 26 zaidi kwa mara ya kwanza mwaka jana. Kitabu kinachosaidia kujifunza Biblia Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele, kilichochapwa na Watchtower Bible and Tract Society na kutolewa mwaka wa 1968 (kwa Kiingereza na 1969 kwa Kiswahili), sasa kimechapwa kufikia nakala milioni 74 katika lugha 91. Kitabu kingine kama hicho cha kusaidia kujifunza Biblia ni Amani ya Kweli na Usalama wa Kweli—Kutoka Chanzo Gani? (1973 kwa Kiingereza na 1974 Kiswahili), kiko sasa katika lugha 14; zaidi ya nakala milioni 16 vimechapwa.