Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 3/15 kur. 123-124
  • Tutalisha Jirani Zetu—Au Tuwaache Wafe Njaa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tutalisha Jirani Zetu—Au Tuwaache Wafe Njaa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JIBU NI NINI?
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Upungufu wa Chakula Uliopo Duniani Leo?
    Habari Zaidi
  • Njaa Ina Maana Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 3/15 kur. 123-124

Tutalisha Jirani Zetu​—Au Tuwaache Wafe Njaa?

KUPITIA kwa habari za ulimwengu, tunajua kwamba watu wanazidi kuwa wenye njaa. Bila shaka, njaa si jambo jipya. Lakini kadiri ya ugumu wa leo ni jambo jipya. Kama vile makala katika New York Times inavyosema:

“Njaa kuu iliyo hapa na pale imeandikwa hata katika Biblia. Jambo lililo jipya ni kutokuwako kwa upungufu wa chakula katika sehemu na nyakati fulani tu: ni hatari yenye kutisha mamia ya mamilioni katika sehemu kubwa za dunia.”

Makadirio yanaonyesha kwamba karibu watu milioni 500​—wengi wao wakiwa watoto​—⁠sasa wanakaribia kufa njaa. Kwa hakika unabii wa Biblia, “kutakuwa na njaa . . . mahali mahali,” unatimia.​—Mt. 24:7.

Ni nani kati yetu anayeweza kuona picha za watu wenye njaa asitake kuwasaidia? Lakini tunaweza kufanya nini?

Si vigumu kusaidia jirani wa mahali tunapoishi wenye shida ya muda, kama vile msiba fulani unapotokea. Mara nyingi kunapokuwa hivyo watu wanafanya mambo ya fadhili na ukarimu. Walakini, hali iko tofauti ulimwengu wote unapohusika. Kwa sababu gani?

Kwanza, ziko hali nyingi zaidi leo zisizoonekana. Ingeelekea kuwa kwamba dunia haizai chakula cha kutosha kuenea sehemu zote. Lakini huo si ugumu wenyewe. Mavuno ya nafaka yanayovunwa sasa yangeweza kulisha vya kutosha kila mtu aliye hai​—kama yangegawanywa sawasawa na kama nafaka ingeliwa moja kwa moja au mkate au mazao ya namna hiyo.

Lakini sivyo ilivyo. Mengi ya mavuno ya ulimwengu yanatumiwa na mataifa yaliyo tajiri zaidi kulisha wanyama na kutokeza nyama, maziwa na mayai. Inaweza kuchukua kufikia kilogramu tatu na nusu za nafaka kutokeza nusu kilogramu ya nyama. Hiyo ni sababu moja ya yaitwayo mataifa “yenye maendeleo” yenye theluthi moja ya idadi ya watu wa dunia kula nafaka nyingi zaidi kuliko mataifa mengine yaliyo maskini zaidi, yenye theluthi mbili za idadi ya watu wa dunia yakiwekwa pamoja. Ndivyo ilivyo na kwa mafuta na mbolea, ambavyo ni vitu vikubwa vya kusaidia kuleta mazao katika ukulima wa kisasa.

Lakini je! mataifa “yenye maendeleo” hayalishi sehemu kubwa ya ulimwengu? Naam, nchi kama United States, Canada, Australia na Argentina zinasafirisha nje mamilioni na mamilioni ya kilogramu za nafaka kila mwaka. Ugumu ni kwamba mataifa yaliyo maskini zaidi yanaona ni vigumu zaidi kulipa. Kupungua kwa thamani ya pesa kwenye kwenda mbio mbio kunawafanya wasiweze kununua chakula, mafuta na mbolea. Na idadi ya watu wao inazidi kuongezeka. Kila mwaka kunakuwa na vinywa milioni 80 zaidi vya kulisha​—vingi vikiwa katika nchi zenye njaa tayari.

JIBU NI NINI?

Ufumbuzi ni nini? Madai yenye kupingana yanatolewa. Viongozi wa mataifa “yenye maendeleo” wanasema kwamba mataifa yaliyo maskini zaidi lazima yatie jitihada za kupunguza ongezeko la idadi ya watu. Lakini katika nchi hizo watoto wengi wanakufa wakiwa wa umri mdogo. Kwa hiyo kwa kweli wazazi wanataka jamaa kubwa, wakitumaini kwamba watoto wengine wataendelea kuwa hai wawatunze watakapokuwa wazee. Mataifa yaliyo maskini zaidi yanaambia mataifa “yenye maendeleo” hivi: ‘Sababu gani ninyi mwanunua vitu vyetu vya kutengenezea vifaa kwa bei ndogo kisha mwatuuzia mnavyotengeneza kwa bei za juu? Sababu gani msiishi na kula kwa kiasi zaidi ili mazao mengi ya nchi zenu yaweze kufaidi wanadamu wengi zaidi?’

Kwa mfano wewe unaweza kufanya nini usaidie, ukikabiliwa na hali hiyo? Kwa wazi, ukila kidogo zaidi hiyo tu haitawapa watu wa nchi nyingine chakula. Je! unaweza kutegemea serikali za kitaifa au matengenezo mengine uhakikishe kwamba jitihada zo zote unazofanya kusaidia chakula kiwe kingi zaidi zitaletea wenye njaa ulimwenguni faraja?

Linalosikitisha ni kwamba, yako mengi ya kufisha watu moyo. Wao wanaona kwamba hali zinazidi kuwa mbaya, ijapokuwa pesa zinatolewa kwa wingi kusaidia. Wako watu wengi zaidi wenye njaa sasa kuliko zamani. Serikali zenye kupokea msaada zinautumia kununua vifaa vya kijeshi vyenye gharama kubwa badala ya kununua chakula. Ufisadi, biashara za magendo na kuharibiwa kwa vitu ovyo kunapunguza sana vyakula vinavyopelekwa kusaidia wenye shida.

Makala moja katika gazeti BioScience inasema hivi:

“Serikali yenye hekima na uwezo wa kutosha inaweka akiba ya mazao yanayopatikana wakati wa miaka yenye mazao mengi ikifikiria miaka isiyo na mazao itakayokuja. Hilo si wazo jipya. Biblia inatueleza kwamba Yusufu alimfundisha Farao kanuni hiyo katika Misri zaidi ya miaka 2,000 iliyopita. Na hali ni wazi kabisa kwamba serikali zilizo nyingi za ulimwengu leo hazina kanuni hiyo. Ama zinakosa hekima au uwezo wa kutosha, au vyote viwili.”

Ushuhuda unaonyesha kwamba mataifa “yenye maendeleo” mara nyingi hayataki chakula kiongezeke sana. Kwa sababu gani? Kwa sababu kikiongezeka bei zitashuka na faida wanazopata zitapungua. Mazao yanazuiwa yasiwe mengi sana ili bei ziendelee kuwa juu ulimwenguni. Hata chakula kinatumiwa kupata faida ya kisiasa.

Kwa upande mmoja tunawasikia mara nyingi viongozi wa ulimwengu wakisema kwamba wanachukua wanadamu wote kama ndugu nao wazungumza juu ya “udugu wa mwanadamu.” Lakini maeneo makubwa ya wanadamu yanapokuwa na shida, mara nyingi faida za kitaifa na kibiashara zinatanguliwa mbele ya mahitaji ya wanadamu wenzao.

Zamani za kale, mtume aliyeongozwa na Mungu aliandika hivi: “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? . . . tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.” (1 Yohana 3:17, 18) Vile ilivyo kwa wanadamu ndivyo ilivyo kwa mataifa. Ingawa yanajidai kuwa ya kidini, mataifa ya ulimwengu yanaonyesha kwamba yanakosa upendo wa Mungu.

Kwa wazi kinachohitajiwa ni taratibu mpya kabisa kwa ajili ya wanadamu, taratibu itakayoondoa utukuzo wa taifa wa kichoyo na mashindano ya kibiashara yasiyo na huruma, badala yake kuwe na taratibu zenye kutendea watu wote sawasawa na kuongeza ushirikiano, ukarimu usio wa kinafiki na upendo kwa jirani. Kitabu kilichotabiri upungufu wa leo wa chakula, Biblia, kilitabiri pia juu ya kuja kwa taratibu mpya hiyo. Kinaonyesha kwamba ufalme wa Mungu kupitia kwa Mwanawe karibuni utaanza kusimamia mambo yote ya dunia na kuiondolea dunia taratibu zote zinazoletea wanadamu taabu sasa.​—Mt. 6:9, 10; Dan. 2:44.

Mmoja mmoja hatuwezi kubadili hali za sasa. Lakini hiyo haitoi sababu ya kuwa wenye baridi tusisaidie wengine wenye taabu. Je! tunatumia nafasi tulizo nazo kusaidia wengine? Mithali 22:9 inatuhakikishia hivi: “Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; maana huwapa maskini chakula chake.”

Leo mashahidi wa Yehova wanajitahidi kuhakikisha upendo wao kwa Mungu kwa kusaidia ndugu zao wenye shida katika nchi zote, bila kubagua taifa, mbari, rangi wala hali ya kijamii. Na, la maana zaidi ni kwamba, wanajaribu kusaidia watu wote kila mahali wawe na tumaini la taratibu mpya inayokuja, isiyokuwa na njaa, ambayo Neno la Mungu linaahidi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki