Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 9/15 kur. 424-427
  • Uhai Wako Ni Wenye Thamani Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uhai Wako Ni Wenye Thamani Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUCHUKUA ‘KIKOMBE CHA WOKOVU MKUU’
  • KUMLIPA YEHOVA NADHIRI
  • MAUTI YA WAAMINIFU “INA THAMANI”
  • DHABIHU YA SHUKRANI
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yehova Ni Mkuu Katika Upendo Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Upendo Mshikamanifu wa Yehova Unamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Zaburi—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 9/15 kur. 424-427

Uhai Wako Ni Wenye Thamani Gani?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1. Watu kwa ujumla wanauonaje uhai?

KWA watu walio wengi uhai ni hazina. Bila huo, hakuna cho chote. Kwa wengine, uhai si wa maana sana. Wao wana nia ya kujitia katika hatari kubwa wapate sifa au raha ya muda. Hata hivyo wengi wa watu hawa wanaoelekea kutothamini uhai sana wanajaribu kujipatia raha yote au sifa yote wawezayo kwa wakati mfupi. Wanaonyesha wazi kwa mwendo wao kwamba kwa kweli wao wangependa kuwa na maisha marefu kama wangeona wanaweza kuishi chini ya hali zinazofaa. Lakini kwa sababu ya hali mbaya zilizopo hawaoni uwezekano wo wote kwamba maisha yanaweza kuwa marefu na yenye furaha.

2. Yehova anauonaje uhai?

2 Muumba anachukuaje uhai ambao amewapa wanadamu? Yeye anauona kama wenye thamani kubwa zaidi, hazina. Yeye ndiye mwenye uhai wote naye anaujua ulivyo na unavyoweza kuwa. Kwa hiyo anatoa nafasi ya kupata uzima wa milele kwa wanadamu kupitia kwa Mwanawe Yesu Kristo, naye hataki mtu ye yote apoteze zawadi hii iliyo nzuri sana​—Yohana 6:51.

3. Mungu sasa anatolea wanadamu nafasi gani?

3 Uhai wako ni wenye thamani gani kwako wewe? Je! unataka kuuendeleza? Yeye anatoa uhakikisho wa kuokoa wale wanaoufuata mpango wake wa kupatia uzima wasije wakatoweka kabisa. Ndiyo, huenda wakafa sasa kwa sababu ya ugonjwa au mambo mengine, lakini wao wanaweza kuwa na hakika kabisa watafufuliwa wawe katika dunia hii tena wakati wa utawala wa Yesu Kristo unaokuja wa miaka elfu. (Yohana 5:28, 29) Mungu atakomboa na kuhifadhi wengi, mamilioni ya watu, waingie katika hiyo “nchi mpya,” kwa maana inakaribia sana.​—2 Pet. 3:13; Ufu. 20:4, 6; 7:9-17.

4. Je! Mungu anatuhakikishia kwamba kila mtu kati ya watu wake ataishi aokoke uharibifu wa taratibu hii ya mambo?

4 Haiwezi kusemwa kwamba kila mtu kati ya wale wanaomtumikia Mungu ana uhakikisho kabisa kwamba atalindwa awe hai mpaka wakati wa uharibifu wa taratibu hii ya mambo na kuuokoka, ambao lazima uje kabla ya utawala wenye amani wa Kristo wa miaka elfu. (2 Pet. 3:10-13; Ufu. 19:19-21; 20:1-4) Lakini Mungu anatuhakikishia katika Neno lake lililoandikwa (naye Mungu hawezi kusema uongo) kwamba watu wake, watalindwa na kukombolewa kama jamii waingie katika hiyo “nchi mpya” yenye haki. (Tito 1:2) Yeye anataka WAISHI, si wafe, wafurahie uzima kamili milele.​—Eze. 18:23, 32.

KUCHUKUA ‘KIKOMBE CHA WOKOVU MKUU’

5, 6. Mwandikaji wa Zaburi 116 alipatwa na jambo gani, naye alisema nini alipokombolewa asife?

5 Mungu mwenye upendo huo kwa watu wake alimwongoza mmojawapo wa watunga zaburi wake aandike juu ya maono yake. (Kwa kweli, mtunga zaburi huyo alielekea kuandika habari zake mwenyewe akiwakilisha taifa lote la Israeli.) Alipatwa na hali ambamo maisha yake yalikaribia kutoweka kabisa akiwa mikononi mwa adui za Mungu na watu Wake. Halafu Mungu akamkomboa na kifo. Mtume Paulo aliyataja maneno ya mtunga zaburi yaliyo katika Zaburi 116:10 akayatumia maneno hayo kwake mwenyewe na Wakristo wenzake. (2 Kor. 4:13) Kwa kushukuru mtunga zaburi alisema hivi, kwa furaha nyingi:

6 “Nitamupa [Yehova] nini kwa ukarimu wake wote alionitendea? Nitapokea kikombe cha wokovu, na kuitia jina la [Yehova]. Nitalipa [Yehova] naziri zangu, ndiyo, mbele ya watu wake wote.”​—Zab. 116:12-14, Swahili Congo Bible.

7. Maneno ya mtunga zaburi juu ya ukombozi yanatumikaje duniani sasa?

7 Zaburi hii nzuri, Zaburi 116, inatumika nyakati za kisasa kwa mabaki ya wanafunzi waliotiwa mafuta wa Kristo kutoka mwaka wa 1919 na kuendelea, baada ya kutoka katika magumu na hatari za Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Lakini wakati ujao wao na “mkutano mkubwa” pia wa “kondoo wengine” wa Kristo watapata ukombozi mkubwa katika ‘dhiki kubwa.’ Kwa hiyo, wakati watakapokombolewa na hatari Mungu akiondoa waovu duniani katika ‘dhiki kubwa,’ wao watakuwa na amani. (Mit. 21:18) Ndipo waaminifu watakapoweza kuhifadhiwa wakati wote wa miaka elfu ya ufalme wa Mungu wa Kimasihi, watakaoishi milele katika dunia itakayosafishwa wakiwa ndio waaminifu wa “mkutano mkubwa” unaotajwa katika Ufunuo 7:9-17.

8. ‘Kikombe cha wokovu mkuu’ ni nini, na wale watakaokipokea wataliitiaje jina Yehova?

8 Mtunga zaburi alizungumza juu ya “kikombe.” Kikombe kinakuwa na kitu cha kunywa au hata cha kumimina kama ‘sadaka ya kinywaji’ kwa Yehova, kama ilivyokuwa ikifanywa siku za mtunga zaburi. (Hes. 28:7; Flp. 2:17) Yehova anawatolea watu wake ‘kikombe cha wokovu mkuu’ kwa kuwahifadhi wapite ‘dhiki kubwa.’ (Ufu. 7:14) Wakati wa miaka elfu ya utawala wa Masihi wa duniani pote wao watakunywa ‘wokovu mkuu’ watakaopewa, wafurahie maisha “katika nchi za walio hai.” (‘Zab. 116:9) Watakapokuwa wakifanya hivyo, wataliitia jina la Yehova kupitia kwa Masihi awabariki na kuwaongoza katika jitihada zao zote.

KUMLIPA YEHOVA NADHIRI

9. Nadhiri ambazo ni lazima watakaokombolewa walimpe Yehova ni nini?

9 ‘Nadhiri’ ambazo lazima watakaokombolewe wamlipe Yehova ni nini? Wakati walipokuwa wanakaribia sana kufa wakiwa mikononi mwa adui za Mungu, je! waliweka nadhiri zo zote, ahadi nzito zo zote kwa Mungu wakitaka wakombolewe na Mungu? Ikiwa ndivyo, basi watamlipa Yehova ‘nadhiri’ hizo kwa sababu alitenda kupatana na nadhiri zao akawahifadhi. Watafanya walivyosema watafanya kwa kuweka nadhiri “mbele ya watu wake wote,” kwa njia hiyo walisifu jina lake mbele ya watu wote.

10. Ni kwa njia gani mtunga zaburi alikuwa “mwana wa mjakazi [wa Yehova],” naye Yehova ‘alifunguaje vifungo vyake’?

10 Akiendelea kushukuru kwa sababu ya kuhifadhiwa na Yehova, mtunga zaburi anatia mkazo juu ya thamani ambayo Yehova anaweka juu ya maisha za wale wanaoishi kulingana na kanuni zake za haki: “Ina thamani machoni pa [Yehova] mauti ya wacha Mungu wake. Ee [Yehova], hakika mimi ni mtumishi wako, mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako, umevifungua vifungo vyangu.” (Zab. 116:15, 16) Akiwa na shukrani mtunga zaburi alijua kwamba Yehova alikuwa amemhesabu kuwa mwaminifu kwa kumhifadhi. Alikuwa amekuwa katika hatari ya kuogofya, lakini Yehova akafungua vifungo ambavyo kwavyo alielekea kufungwa mpaka kufa. Alijiita “mwana wa mjakazi [wa Yehova],” jambo ambalo lilionyesha kwamba alikuwa mmoja wa watu wa Yehova. Alifahamu kwamba Yehova alimhesabu kuwa mmoja wa watumishi Wake waaminifu.

MAUTI YA WAAMINIFU “INA THAMANI”

11. Taja njia ambayo mauti ya waaminifu wake ina thamani machoni pa Yehova.

11 Mauti ya waaminifu wake “ina thamini machoni pa [Yehova]” kadiri gani? Kama vile mtunga zaburi alivyokuwa, wao ni watumwa wenye thamini sana kwa Yehova. Fadhili za upendo za Mungu kwa mtumishi wake zilimvuta ahifadhi uhai wake. Uhai wa mtu ni wenye thamani sana machoni pa Yehova hasa ikiwa anautumia kwa njia inayofaa, akiwa mwabudu Wake wa kweli. Yehova anahesabu mauti ya jamii yote ya waaminifu wake kuwa yenye thamani mno hata asiache itukie. Bila shaka, waaminifu watatoa shukrani na asante kwa sababu ya jambo hili, kwa sababu uhai ni wenye thamani sana kwao. Yehova ana sifa nzuri sana kwa kuwa anapendezwa sana sana na maisha za watumishi wake. Yeye anaona kifo chao kama hasara kubwa mno isiyolipika, na kwa hiyo haachi kifo hicho kitokee.​—Rum. 8:35-39.

12. Zaidi ya kupenda kwa Yehova watumishi wake, ni kwa sababu gani nyingine mauti ya watumishi wake ina thamani?

12 Si kwamba tu upendo mkuu wa Yehova unaonyeshwa wazi hapa, bali pia heshima yake kwa hukumu inayofaa na haki katika ulimwengu wote inaonyeshwa, kwa ajili ya faida ya viumbe vyake vyote. Akiacha adui washinde watu wake waaminifu na kuwafutilia wote mbali watoke usoni pa dunia hiyo ingekuwa kufuta kabisa enzi yake kuu ya ulimwengu wote, utawala wake juu ya mbingu na dunia. Yeye ndiye Muumba wa dunia naye aliiumba kwa ajili ya wale walio waaminifu kwake. (Isa. 45:18) Ikiwa hawezi kuhifadhi kikundi chake cha waaminifu duniani hata wakiwa chini ya shambulio kali la adui wanyonge wenye kumpinga Mungu, ingekuwa kana kwamba adui zake ndio wenye nguvu kuliko yeye na ndio wenye haki ya kusema ni nani watakaoishi duniani milele. Yeye hataruhusu utawala wake wa dunia, kwa kweli, enzi kuu yake yote ya ulimwengu wote na vile vile jina lake lishutumiwe (liaibishwe), lishindwe na jambo kama hilo.

13. Yehova akiruhusu jamii yote ya waaminifu wake ifutiliwe mbali kutoka usoni pa dunia, hii ingehusuje utawala wa ufalme wa Kimasihi wa miaka elfu?

13 Zaidi ya hayo, kama Yehova angeruhusu jamii yake yote ya waaminifu iondolewe kabisa duniani, kusingebaki mtu ye yote katika nyua za hekalu lake kuu la kiroho, ambazo ziko duniani. Kusingekuwa na msingi wa “nchi mpya” au jamii yenye haki ya kibinadamu ya kukaa chini ya “mbingu mpya.” (Ufu. 21:1) Basi, ni kwa njia gani utawala wa miaka elfu wa Masihi ungeweza kuanza, bila raia za kidunia? Sivyo! Kifo cha kikundi chote cha waaminifu wa Mungu duniani kingekuwa chenye thamani mno, chenye hasara mno, kwa Yehova. Kwa sababu ya Yeye kujiheshimu mwenyewe, ni chenye hasara mno hata asikiruhusu.

DHABIHU YA SHUKRANI

14-16. Waokokaji wa ‘dhiki kubwa’ wataonaje na watatendaje?

14 Kwa sababu ya Yehova kuokoa “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” waishi duniani, kwa sababu ya kuendeleza kusudi lake na ahadi zake ili dunia iwe mahali ambapo haki inakaa, waokokaji wa “dhiki” wanatoa sifa na shukrani za moyo. Yehova anawataka waishi na kufurahia maisha. Wao, pamoja na mabaki ya Waisraeli wa kiroho, watasema kama alivyosema mtunga zaburi:

15 “Nitakutolea zabihu ya kushukuru, na kuita jina la [Yehova]. Nitalipa naziri zangu kwa [Yehova], ndiyo, mbele ya watu waka wote; katika viwanja [“nyua,” UV] vya nyumba ya [Yehova], katikati yako, Ee Yerusalemu. Musifu [Yehova].”​—Zab. 116:17-19, Swahili Congo Bible.

16 Waokokaji wa ‘dhiki kubwa,’ mabaki yaliyotiwa mafuta na “mkutano mkubwa,” watatoa dhabihu za shukrani na sifa kwa Yehova kwa sababu ya kukombolewa kwao, wakiwa na roho ile ile ambayo Nuhu na jamaa yake walikuwa nayo wakitoa dhabihu kubwa ya shukrani walipokwisha kuokolewa kupita gharika ya dunia yote. (Mwa. 8:20, 21) Ndipo “mkutano mkubwa” ulio duniani watakapofurahi zaidi kuona mamilioni mamilioni ya watu wakifufuliwa duniani wawe na nafasi ya kupata zawadi yenye kutamaanika ya uzima pia.​—Ufu. 20:11-15.

17, 18. (a) Yehova anakusudia nini kwa wanadamu? (b) Ni kwa njia gani usemi “Haleluyah” unafaa kwa watu wa Mungu?

17 Je! wewe unathaminije uhai wako mwenyewe? Je! unafikiri unastahili kuishi katika dunia yenye amani iliyorembeshwa ukiwa na afya nzuri kabisa na bila kuogopa kifo wakati wo wote? Nyakati nyingine, maisha yanaweza kuwa magumu sasa, lakini Yehova, anayejua namna maisha yanavyoweza kuwa mazuri chini ya hali nzuri, anakusudia kuleta hali hizi. Yeye anakutaka wewe na wengine wote wachukue nafasi anayoitoa kupitia kwa Neno lake Biblia.

18 Tukiwa tunajua mambo ambayo Yehova anakusudia kwa ajili yetu, tunaweza kupata kumjua yeye na kumpenda na kuwa raia zake waaminifu, tukiwa na matumaini yenye furaha zaidi. Yeye ndiye chanzo cha pekee cha uzima, uzima kweli kweli unaoweza kufurahiwa kama ambavyo yeye aliumba wanadamu waufurahie. Kwa sababu hii tunaweza kuukubali msemo wa mtunga zaburi, “Musifu [Yehova]!” kama unaofaa kabisa. Msemo huo, kwa Kiebrania, ni “Haleluyah!” nao unaonekana mara nyingi katika Maandiko ya Kiebrania. Ukiwa katika namna ya Kigiriki unapatikana karibu na sehemu ya mwisho ya kitabu cha mwisho cha Biblia, Ufunuo. (Ufu. 19:1-6) Wale wanaotangaza jina la Mungu ni mashahidi wa utukufu, fadhili za upendo na ukuu wa Yehova.

19. Wote wanaopenda uzima wanaweza kufanya nini sasa ili wawe na matumaini ya uzima usio na mwisho?

19 Leo Wakristo wanatoa sifa hii kupitia kwa Kuhani wao Mkuu, Yesu Kristo, katika hekalu la kiroho la Yehova. Hili si jengo la kidunia. Walakini, wanakutana wajifunze Biblia na kuabudu katika majengo wanayoyaita “Majumba ya Ufalme.” Wanaongoza pia mafunzo ya nyumbani ya Biblia yasiyo na malipo kwa watu wanaopendezwa. Wote wale wanaopenda uzima wanaweza kujiunga nao sasa kuchunguza Neno la Mungu, wajifunze mengi zaidi juu ya kusudi lake na ahadi zake, nao wanaweza kujiunga nao katika ibada ya kweli. Watafurahia kuwa na matumaini mazuri sana ya kuokoka na kupata uzima milele!

​—Kutoka Kitabu God’s Kingdom of a Thousand Years Has Approached.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki