Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w75 10/15 kur. 475-478
  • Ni Mambo Gani Unayotaka Zaidi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Mambo Gani Unayotaka Zaidi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • WATU MMOJA MMOJA WAHUSIKA MATAIFA ‘YATIKISWAPO’
  • HEKALU KUU LA KIROHO LA MUNGU
  • UTUKUFU MKUU ZAIDI WALETWA KWENYE NYUMBA YA MUNGU
  • “Vitu Vinavyotamaniwa” Vinaijaza Nyumba ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Nyumba ya Yehova Yainuliwa Juu
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
  • Acheni Wote Wamtukuze Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
w75 10/15 kur. 475-478

Ni Mambo Gani Unayotaka Zaidi?

Makala hii ni ya kutumia kwa mafunzo ya kitabu ya kundi

1, 2. Ni vitu gani vyenye thamani zaidi kwetu?

UNAPOFIKIRIA mambo ambayo ungetaka zaidi, je! wewe unafikiria pesa kwanza? utajiri? mamlaka? Au kwanza unafikiria rafiki wema na waaminifu, kujipatia mwenyewe amani na usalama pamoja na jamaa yako?

2 Unapofikiria maulizo haya, huenda pesa zikaelekea kuvutia sana kwa sababu zinaweza kununua vitu vingi vya kupendeza. Lakini inaelekea sana kwamba unafikiria amani, usalama na furaha kama mambo yaliyo ya maana zaidi. Pesa haziwezi kununua vitu hivi kwa wingi. Na je! mambo haya mema hayaelekei sana kupatikana kwa kushirikiana na rafiki waaminifu wanaokupenda na kujaribu wawezavyo kukufaidi?

3, 4. Mungu aliporudisha watu wake Yerusalemu baada ya kuwa uhamishoni Babeli, alionyeshaje kwamba hekalu lenye mapambo na lenye kuvutia kwa sababu ya fahari yake halikuwa ndilo jambo lenye kutamanika kwake?

3 Mungu anahesabu watu wema na wanyofu kuwa bora kuliko mali za kimwili, sawa na wewe unavyowahesabu kuwa bora. Kwa kweli wanafurahisha moyo wake, na wanafurahisha wengine. (Mit. 23:15; 27:11; Hos. 6:6) Wakati mmoja Mungu alikuwa na hekalu lake mwenyewe lenye kuonekana na lenye fahari katika Yerusalemu, lakini kwa sababu ya kuabudiwa na watu kwa mdomo tu si kwa moyo akaruhusu hekalu hilo liharibiwe. (Isa. 29:13, 14) Baadaye, aliporudisha Wayahudi Yerusalemu kutoka uhamishoni Babeli, Mungu angaliweza kuagiza hekalu lenye mapambo zaidi lijengwe. Ili kukazia uhakika huu kwao, akawaambia wajenzi hivi: “Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu.” (Hag. 2:8) Lakini hekalu lenye kuvutia kwa sababu ya fahari yake tu lisingetukuza jina lake duniani. Ni nini kingefanya hivyo?

4 Kitu chenye kutoka kwa mataifa kilikuwa chenye thamani zaidi kwake kuliko dhahabu na fedha. Alitangaza hivi: “Nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa vya mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu.”​—Hag. 2:7.

WATU MMOJA MMOJA WAHUSIKA MATAIFA ‘YATIKISWAPO’

5. Yehova atatikisa mataifa kadiri gani, na hivyo namna gani juu ya uvumilivu wao wa dini wakati wa sasa?

5 Kutikiswa kwa mataifa walipopashwa habari kwamba Yehova Mungu Mwenye Nguvu zote alichukua enzi yake kuu ya ulimwengu wote wakati wa mwaka wenye vita wa 1914 kulifanya watangazaji wa Ufalme wakasirikiwe sana. Mataifa ya kisiasa ya dunia yataonyesha ukatili wao wote kwa mara ya mwisho, naye Yehova atayatikisa mataifa yote kweli kweli mpaka yavunjike-vunjike na kuharibika yaondolewe milele. Kwa hiyo, mabalozi wa Ufalme kwa sasa wanavumiliwa na mataifa kwa muda tu. Ye yote asidanganywe na jambo hilo.

6. Je! mataifa ya kisiasa yametimiza unabii wa Hagai 2:7?

6 Basi, ni kwa njia gani ‘vitu vinavyotamaniwa vya mataifa yote vinavyokuja’ kabla ya mataifa yote kuonyesha hasira kuu na baada ya hapo kuondolewa kwa nguvu nyingi? Basi, mambo ya hakika ya historia yanaonyesha nini juu ya kutimizwa kwa unabii huu mpaka sasa? Hayaonyeshi kwamba mataifa yote ya kisiasa yamekuja katika hekalu la kweli la Yehova la ibada na kuleta vitu vinavyotamaniwa vya mataifa yao kama zawadi za kujitolea.

7. Watu wengine mmoja mmoja wanaonaje leo wakati ambapo Mungu ‘anatikisa’ mataifa?

7 Hata hivyo, namna gani juu ya raia mmoja mmoja katika mataifa yote? Basi, mpaka sasa makumi ya maelfu ya watu wameitikia kuhubiriwa kwa Ufalme kwa njia tofauti na ile ya serikali zao za kisiasa na matengenezo ya kidini yaliyojitia siasani. Wamepata kuona kwamba wakati wao ujao hautakuwa wenye furaha, wenye amani na ufanisi wakikaa chini ya serikali hizo za kisiasa zilizofanywa na wanadamu. Wamepata kuona kwamba tumaini la pekee la kuokolewa na uharibifu utakaoyapata mataifa ya kisiasa ya taratibu hii ya mambo ni ufalme wa Kimasihi wa Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. Wanaona sana kwamba Shetani Ibilisi ndiye “mungu wa taratibu hii ya mambo,” nao hawataki kumwabudu mungu huyo wa uongo kwa kuyaabudu mataifa ya kisiasa. (2 Kor. 4:4) Wanajua kwamba enzi yote kwa haki ni ya Mungu Aliye Juu Zaidi ya wote. Kwa hiyo, wao wamejiweka wakf kabisa kumwabudu Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova katika nyumba yake ya kweli ya ibada. Wameshirikiana na mabalozi wake.

HEKALU KUU LA KIROHO LA MUNGU

8. Tunaona utimizo wenye kusisimua wa unabii gani leo?

8 Tunapoona mawakili hao wa kisasa wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova pamoja na ibada yake, tunaona utimizo wenye kusisimua wa unabii ule unaotajwa mara nyingi wa Isaya 2:2-4: “Itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya [Yehova] utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi. Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa [Yehova], nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake, . . . nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”

9. Isaya 2:2-4 pamoja na Waebrania 9:24 inaonyesha hekalu ambako Mungu anakusanya “mataifa mengi” ni nini?

9 Katika Yerusalemu wa kale hekalu la Yehova lilikuwa juu ya Mlima Sayuni. Ndipo palipokuwa mahali pakuu pa ibada. Hekalu hilo liliharibiwa na Wababeli mwaka wa 607 B.C.E., nalo hekalu la pili, lililojengwa baada ya Wayahudi kurudishwa Yerusalemu kutoka uhamishoni Babeli na kujengwa upya na kupanuliwa na Herode, liliharibiwa na majeshi ya Kirumi mwaka wa 70 C.E. Kwa hiyo, hekalu hili linalotajwa na Isaya kama likiwako katika siku za mwisho, ambako watu watakusanyika, si hekalu lenye kuonekana lililojengwa kwa mikono ya wanadamu, bali ndilo lile ambalo mwandikaji wa kitabu cha Biblia kinachoitwa “Kwa Waebrania” alisema hivi juu yake: “Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu.”​—Ebr. 9:24.

10. Sababu kubwa ya ‘kuugua’ kwa watu hawa wanaotajwa katika Isaya 2:2-4 wanaokuja kwenye hekalu la Yehova la ibada safi ni nini?

10 Hili ndilo hasa unabii wa Hagai ulitaja​—hekalu kuu la kiroho, ambamo Mtakatifu Zaidi ya wote Yehova Mungu aketi kama Mwamuzi, katika mbingu zenyewe. (Ebr. 12:22, 23) Kristo akiwa ndiye Kuhani Mkuu na Mfalme ni wakili mkuu wa Mungu wa ‘kutikisia’ mataifa. (Zaburi 110) Yeye anakusanya watu “wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika” watoke, hasa katika Jumuiya ya Wakristo (Kristendomu), ambayo inajidai kutumikia Mungu na Kristo. (Eze. 9:4) Sababu kubwa ya “kuugua” kwa watu hawa si kwamba hali za ulimwengu zinawataabisha sana, bali upotovu wanaoona ukizoewa kati ya wanaoitwa Wakristo ndiyo sababu​—suto ambalo watu hawa wanaleta juu ya jina zuri la Yehova Mungu Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote, na ambalo linaletwa juu ya Mwanawe, mfalme na kuhani wake mkuu. Wanajihakikisha kuwa wapenda haki kweli kweli.

11-14. Maandiko katika Ufunuo 7:9-17 yanatambuaje wale wanaokusanyika kwenye nyumba ya Yehova?

11 Katika sehemu ya mwisho ya siku za mwisho hakuna shaka kwamba watu hawa waliomo katika nyua za kidunia za hekalu la kiroho la Yehova wanatambuliwa. Wametoka katika hali zote​—kutoka makabila yote, mataifa na hali za maisha. Wamesafisha maisha zao nao wanabadili nyutu zao kulingana na kielelezo kilichowekwa katika Maandiko. (Efe. 4:22-24) Tumaini la Biblia walilo nalo ni la kupata uzima wa milele duniani. Wanasimuliwa vizuri katika kitabu cha unabii cha Ufunuo. Kwa habari ya wakati ambapo ‘kutikiswa’ kwa mataifa na Mungu kunakaribia mwisho, njozi ya Ufunuo kwanza inaonyesha kukusanywa kwa mwisho kwa hao watakaofufuliwa wakawe wafalme na makuhani wa kimbinguni pamoja na Yesu Kristo, kama ilivyoandikwa na mtume Yohana:

12 “Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha . . . wakilia kwa sauti kuu wakisema, Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.”

13 Yohana aliuliza watu hawa ni nani, naye mzee aliyeulizwa akajibu hivi:

14 “Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, [wakati ambapo taratibu hii ya mambo itatikiswa kabisa ivunjike vipande vipande], nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo. Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake . . . Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, . . . kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”​—Ufu. 7:9-17.

UTUKUFU MKUU ZAIDI WALETWA KWENYE NYUMBA YA MUNGU

15. Kwa sababu gani hawa wanaoingia katika nyumba ya Yehova wanatamanika kwa Mungu, na je! wanatamanika kwetu?

15 Basi, watu hawa wanatamanika kweli kweli na Mungu. Na je! wewe huthamini watu wanaojisafisha, kimwili na kwa adili? Je! wale wasiotaka vita, ‘wasiojifunza vita tena kamwe,’ lakini wanaojaribu kutafuta amani na faida bora za jirani zao, hawaelekei kutamanika zaidi kwako kuliko wale wasiozuia tamaa zao au wasiojiweza? Na je!, kwa kweli watu hawa si wenye thamani zaidi kuliko dhahabu na fedha? Kama watu wote wangekuwa hivi, uchoyo, sababu kubwa ya uvunjaji wa sheria, udanganyifu, unyang’anyi wa kutumia cheo, wizi na vita, ingeondolewa. Hata kusingekuwa kuogopa njaa kuu na uchafu wa hewa, maji na chakula, kwa maana kila mtu angependezwa na jirani yake kama anavyopendezwa na yeye mwenyewe.​—Luka 10:27.

16. Yehova ‘amejazaje nyumba yake na utukufu’ na ‘kuwapa amani katika mahali hapa’?

16 Kwa hiyo Mungu ‘amewapa amani katika mahali hapa kama alivyosema kupitia kwa nabii wake Hagai, yaani, katika nyua za kidunia za hekalu lake kuu la kiroho, ambamo “mkutano mkubwa,” ‘vitu vinavyotamaniwa vya mataifa yote,’ vimekusanyika. (Hag. 2:9) Watu hawa wanaomjia Muumba kwa moyo wa kupenda, na wanaopatanisha maisha zao na kanuni zake na kumtukuza, ndio “vitu vinavyotamaniwa” vya mataifa machoni pake. Kupitia kwao Yehova ameletea jina lake na hekalu lake hili la kiroho utukufu mkuu zaidi kama vile alivyosema angefanya, kuliko alivyouleta kwa lile la kidunia.

17. Wale ambao wamekuja kwenye nyumba ya Yehova kwa ajili ya ibada wamepata nini?

17 Vile vile, wale ambao wamekusanyika kwa umoja wamtumikie Yehova katika hekalu lake kuu la kiroho, na ambao wameanza kubadili maisha zao, wanatimiziwa mambo aliyosema Yesu: “Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili, ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.” (Marko 10:29, 30) Kwa kufuata amri za Yehova, wamejifanya “vitu vinavyotamaniwa,” nao wanatoshelezewa tamaa zao za moyoni.​—Zab. 145:16.

​—Kutoka Kitabu Paradise Restored to Mankind​—⁠by Theocracy.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki