Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 6/1 kur. 262-263
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Jitahidi Kumfikia Mwenzi wa Ndoa Asiye Mwamini
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Wakati Amani ya Ndoa Inapotishika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Unaweza Kupata Furaha Katika Familia Iliyogawanyika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jinsi ya Kufanikiwa Katika Ndoa ya Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 6/1 kur. 262-263

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

● Mwenzi asiyeamini akijitenga na anayeamini, je! huo si msingi wa kuvunja ndoa kulingana na 1 Wakorintho 7:15, ambapo Paulo asema: “. . . hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani”?

Sivyo, mtume hazungumzi habari ya talaka hapa, bali anafariji Mkristo kwamba yeye, awe mwanamke au mwanamume, hapaswi kujiona amepoteza upendeleo ikiwa asiyeamini ameondoka kwa makusudi bila kujali jitihada za mwamini kukaa naye kwa amani.

Paulo alikuwa ndiyo kwanza amalize kutia moyo mwenzi anayeamini asiondoke ikiwa asiyeamini “anakubali kukaa naye.” Kwa sababu gani? “Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.”​—1 Kor. 7:12-14.

Kwa hiyo, ulizo laweza kutokea vyepesi juu ya hali ambayo mwamini angeingia, mwenzi asiyeamini akiondoka ingawa mwamini amefanya jitihada za kumzuia. Je! sasa atajiona amekataliwa na Mungu au kuona kwamba watoto si watakatifu kwa sababu asiyeamini amejitenga kwa nguvu?

Sivyo, kwa maana mtume ajibu hivi: “Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.” Kwa kuwa mwamini amejitahidi awezavyo wasitengane, si lazima amfuate asiyeamini akijaribu kutimiza wajibu wake kwa huyo. Kama asiyeamini angebaki nyumbani na kuwa na nia ya kukaa kwa amani na anayeamini, anayeamini angekuwa na wajibu wa kutimiza madaraka ya ndoa. Lakini mtume alijua kujitenga kwa nguvu kwa asiyeamini kunafanya isiwezekane anayeamini afanye hivyo.

Sasa Mkristo anakuwa na amani ya kumtumikia Yehova, ingawa mtengano kwa kawaida utamletea maono mapya moyoni na kumbadili kimwili. Tena, kujaribu kulazimisha asiyeamini apatane naye kungeelekea kuongeza ugomvi. Pengine asiyeamini atataka kurudi baadaye. Hilo lingekuwa jambo la kutamanika, kuwa na mradi wa kuishi pamoja kwa amani na kutumaini kwamba asiyeamini atakuwa mwamini pia. Hiyo ingepatana na maagizo yaliyotolewa mapema katika mistari 10 na 11, kwamba wakitengana, yawapasa ‘wasioe wala kuolewa, au wapatane.’

Wakati huo wa kutengana, hiyo isingezuia mke, ikiwa ni mwamini, asitafute msaada wa kisheria ili ajitafutie riziki pamoja na watoto wake, akiona yafaa na ni lazima kufanya hivyo. Maandiko, hata sheria ya nchi mara nyingi, humpa baba na mume daraka la kutafutia jamaa yake riziki.

Yesu hakusema ni sawa mwamini aoe au aolewe tena mwenzi asiyeamini akijitenga naye na kupata talaka kisheria. Naye mtume Paulo haruki mpaka wa yaliyosemwa na Yesu kwa kutoa kinachoitwa na wakuu Wakatoliki “pendeleo la Kipaulo.” Paulo anatoa sababu zenye nguvu akipendelea ndoa idumu, si ivunjwe. Ni wazi kwamba kifo huvunja kifungo cha ndoa. Lakini wenzi wote wawili wakiwa hai, “uasherati” peke yake (Kigiriki, por·neiʹa) ndio unaompa mwenzi mwaminifu msingi wa talaka ya kweli na uhuru wa kuoa au kuolewa tena.​—Mt. 5:32; 19:9; 1 Kor. 7:39.

Hivyo, tofauti na vile watafsiri fulani wanavyoyatafsiri maneno yanayofuata ya Paulo, katika mstari wa 16, maneno hayo hayatii mwamini moyo achukue kuondoka kwa asiyeamini kama nafasi ya kujitenga kabisa na asiyeamini. Hapo asema hivi: “Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?” Maulizo hayo hayakukusudiwa kuonyesha, kama wengine wanavyodai, kwamba mwamini anajihatirisha sana akijaribu kuhifadhi ndoa kwa tumaini la kusaidia asiyeamini apate wokovu, wala hayakukusudiwa kuonyesha kwamba ingekuwa hekima zaidi kumpa asiyeamini talaka hali ziruhusupo, kwa sababu ya kuondoka kwake. Bali, Paulo akazia faida za kukaa na asiyeamini.

Basi, katika mstari wa 16 anarudia kueleza shauri lake kwa walio katika nira moja na wasioamini, akionyesha kwamba mwenzi akikaa na mwamini kwa kupenda, huenda akawa mwamini na kupata wokovu. Lo! hiyo ni sababu kubwa na ya upendo namna gani ya kutoachana! Na hiyo inapatana na barua na maana ya sehemu nyingine zote za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, kutia na onyo la upole ambalo Petro aliwapa wake Wakristo kwamba waume zao wasioamini “wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno.”​—1 Pet. 3:1-6.

Ili uhakikishe kabisa kwamba huo ndio ufahamu sahihi wa shauri la mtume, fikiria baraka ya Mungu ambayo waamini wengi kati ya mashahidi Wakristo wa Yehova wamepata kwa kuendelea kukaa na wenzi wasioamini. Naam, viko visa vichache ambapo mwamini alivumilia kutengana kwa muda, na baadaye aliyekuwa haamini akawa mwabudu mwenzake wa Yehova na sasa wanatembea pamoja katika njia ya uzima wa milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki