Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/10 kur. 5-6
  • Jitahidi Kumfikia Mwenzi wa Ndoa Asiye Mwamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jitahidi Kumfikia Mwenzi wa Ndoa Asiye Mwamini
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Unaweza Kupata Furaha Katika Familia Iliyogawanyika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kweli Huleta, “Si Amani, Bali Upanga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Msijifunge Nira Pamoja na Wasioamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 11/10 kur. 5-6

Jitahidi Kumfikia Mwenzi wa Ndoa Asiye Mwamini

1. Mbali na Wakristo walio katika familia zilizogawanyika kidini, ni nani wengine wanaotamani kumsaidia mwenzi asiye mwamini aikubali kweli?

1 Je, kuna wahubiri fulani katika kutaniko lenu ambao wana mume au mke asiye mwamini? Ikiwa ndiyo, ni wazi kwamba wahubiri hao wanatamani sana mwenzi wao wa ndoa ajiunge nao katika ibada ya kweli. Hata hivyo, si wao tu wanaotamani iwe hivyo. Kama Mungu, kutaniko zima linatamani kwamba “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Tunaweza kuwafikiaje wenzi wasio waamini wa wahubiri wa kutaniko letu?

2. Kuwa na ufahamu kutatusaidiaje kumsaidia mwenzi asiye mwamini?

2 Kwanza, tunapaswa kuelewa maoni ya mwenzi asiye mwamini. Wenzi wengi wa ndoa wasio waamini wanapenda familia zao na hujaribu kuwa mwenzi na mzazi mzuri. Huenda ni wanyoofu katika imani yao ingawa inatofautiana na yetu. Huenda wasijue mengi kuhusu Mashahidi wa Yehova ila yale tu ambayo wameambiwa na rafiki zao wasiotujua vizuri au wanaotuchukia. Baadhi yao wanaudhika kwa sababu wakati ambao mwenzi wao alitumia hapo awali pamoja na familia, sasa anautumia kwa ajili ya ibada. Ufahamu utatusaidia kumtendea kwa fadhili na heshima mtu asiye mwamini na kuepuka kuwa na wasiwasi mwingi tunapokuwa naye.—Met. 16:20-23.

3. Ni njia gani inayoweza kuwa bora zaidi ya kumsaidia mwenzi asiye mwamini aikubali kweli?

3 Pendezwa Nao Kibinafsi: Njia bora ya kumsaidia mwenzi wa ndoa asiye mwamini aikubali kweli, hasa mwanzoni, ni kupitia mwenendo wetu, bali si mazungumzo ya Biblia. (1 Pet. 3:1, 2) Jambo muhimu ni kupendezwa nao kibinafsi. Akina dada kutanikoni wanaweza kupendezwa na mke asiye mwamini, nao akina ndugu wapendezwe na mume asiye mwamini. Jinsi gani?

4. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunapendezwa na mtu kibinafsi?

4 Iwapo hujapata kukutana na mume au mke huyo, unaweza kufanya hivyo baada ya kuzungumza na mwenzi wake ambaye ni Mkristo. Usivunjike moyo ikiwa mwanzoni mwenzi huyo asiye mwamini si mwenye urafiki. Kuwa wenye urafiki na kupendezwa naye kibinafsi kunaweza kumchochea aanze kupendezwa na Mashahidi wa Yehova. (Rom. 12:20) Wakristo fulani wakomavu humwalika mwenzi asiye mwamini pamoja na familia yake kwa chakula cha jioni, ili wapate kumjua vizuri na kuondolea mbali chuki yoyote ambayo huenda akawa nayo. Wao huzungumzia mambo anayopenda badala ya kufanya mazungumzo yahusu mambo ya kiroho tu. Baadaye, mtu huyo asiye mwamini akiwa hana wasiwasi tena kuhusu Mashahidi, mazungumzo ya Kimaandiko yanawezekana. Au anaweza kukubali mwaliko wa kuhudhuria mikutano yetu ili kujua mambo ambayo mke wake anajifunza, hasa kwa kuwa tayari anawafahamu watu kadhaa kutanikoni. Hata ikiwa hayuko tayari kujifunza kweli, anaweza kupongezwa kwa kumtegemeza mwenzi wake aliye mwamini.

5. Wazee wanaweza kumfikiaje mtu asiye mwamini?

5 Wazee hasa wanapaswa kuwafikia wenzi ambao si waamini na kuwa tayari kuwatolea ushahidi. Huenda mtu asiye mwamini ambaye hajakubali ujumbe wa Biblia akasikiliza mazungumzo ya Biblia anapotiwa moyo kupitia Maandiko akiwa hospitalini au anapokabili matatizo makubwa ya afya. Familia iliyogawanyika kidini ikipata msiba, kama vile kufiwa na mtu wa familia, wazee wanaweza kumwalika yule asiye mwamini wanapoifariji familia.

6. Kwa nini tuwafikie wenzi wa ndoa wasio waamini?

6 Wazia shangwe ambayo Mkristo katika kutaniko letu atakuwa nayo ikiwa mwenzi wake ataikubali kweli! Tukio hilo lenye kufurahisha litamletea Yehova, malaika, na wote kutanikoni shangwe kubwa. (Luka 15:7, 10) Hata hivyo, ikiwa mtu huyo asiye mwamini haitikii mwanzoni, bado tunaweza kufurahi kwamba jitihada zetu zinamfurahisha Yehova ambaye “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”—2 Pet. 3:9.

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Njia bora ya kumsaidia mwenzi wa ndoa asiye mwamini aikubali kweli, hasa mwanzoni, ni kupitia mwenendo wetu, bali si mazungumzo ya Biblia

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki