‘Hakustahili Kuvivua Viatu vya Masihi’
● Kwa habari ya Masihi, Yohana Mbatizaji alisema: “Yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua [kuvivua, NW] viatu vyake.” (Mt. 3:11) Katika karne ya kwanza W.K., ilikuwa kawaida ya watu kuvua viatu (ndara) vyao walipokuwa wakiingia nyumbani halafu walikuwa wakivivaa tena wakati wa kuondoka. Kazi ya kuvulisha mtu viatu vyake ilionwa kama kazi ndogo sana, iliyopaswa kufanywa na mtumwa mwenye cheo cha chini zaidi. Kwa hiyo, wakati Yohana aliposema maneno yake, alionyesha unyenyekevu mwingi, akajionyesha hakustahili hata kuwa mtumwa wa Masihi.