Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 1/1 kur. 17-21
  • Ubatizo—Ni Mwanzo Tu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ubatizo—Ni Mwanzo Tu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UHUSIANO WENYE THAMANI NA YEHOVA
  • KUJENGA JUU YA MSINGI IMARA
  • Kufanye Kumtumikia Mungu Milele Kuwe Lengo Lako
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ubatizo​—Takwa kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 1/1 kur. 17-21

Ubatizo​—⁠Ni Mwanzo Tu

Inapendekezwa maandiko yaliyoonyeshwa bila maneno yake yasomwe na yaonyeshwe yanatumikaje kadiri wakati uruhusuvyo katika funzo la kundi la makala hii

1. (a) Yesu aliuonaje ubatizo wake? (Yohana 6:38) (b) Huenda wengine wa “mkutano mkubwa” wakaonaie ubatizo leo?

UBATIZO wa Yesu ulikuwa mwanzo tu wa huduma yake. Hakuuona kama ndio mwisho wa jambo fulani, bali, kama wenye kumwingiza katika jambo lililopaswa kuendelezwa na kukuzwa. Namna gani wewe? Je! umebatizwa kuonyesha kwamba umejiweka wakf kufanya mapenzi ya Mungu, hivyo ukajitambulisha mbele ya wengine kwamba u mmoja wa Mashahidi wa Yehova? Pengine umebatizwa karibuni, miezi michache iliyopita au mwaka uliopita hivi, kama wengi ambao sasa ni Mashahidi wa Yehova. Waonaje juu ya jambo hilo? Je! labda unafikiri sasa umechukua hatua iliyo kubwa na unaweza kujiambia hivi: ‘Sasa mambo yamekwisha. Kila mtu ajua kwamba mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, mmoja wa “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wa Yesu, nami nikifa sasa naweza kuwa na hakika nitafufuliwa mapema katika ufalme wa Mungu.’​—⁠Yohana 10:16; Ufu. 7:9; Ebr. 10:5-9.

2. (a) Ni mfano gani unaoweza kutusaidia tufikirie vizuri habari ya ubatizo? (b) Watu wengi leo huwa na nia gani juu ya ndoa?

2 Je! ni hekima na yafaa kufuata nia hiyo? Kabla hatujaendelea kuangalia habari za Yesu, na tuangalie mfano, wa ndoa. Uwe umeoa au kuolewa au uwe bado, wajua kwamba wengi huona arusi yenyewe kama tukio kubwa, na wakati na fikira nyingi hutumiwa kuitayarisha. Halafu tukio hilo na shangwe zinazofuatana nalo ziishapo, wenye kuoana wanajiambia: ‘Sasa hatua hiyo imekwisha. Yatakayofuata yatajiangalia yenyewe.’

3, 4. (a) Kwa habari ya ndoa. vijana wengi wameshindwa kujua nini? (Mt. 19:4-6) (b) Sasa tutachunguza ulinganifu gani?

3 Mara nyingi mno vijana hushindwa kujua kwamba kuoa au kuolewa ni kuingia katika uhusiano unaopaswa kuendelea kusitawishwa na kulindwa. Kuweka nadhiri za ndoa na kuziandikisha ulikuwa mwanzo ‘ tu. Kwa sababu ya kudanganyika na kutoona mambo ya mbele ya ndoa wengi hawawi tayari kwa magumu yasiyotazimiwa, licha ya vishawishi, vinavyoweza kutokea baada ya kumalizika kwa ile raha ya msisimko unaopatikana kwanza. Mmoja wao au wote wawili huenda wakaanza kutazama mahali penginepo wakitafuta njia ya kuepuka ghadhabu yao kali na nyege zao, wakitaka kutosheleza tamaa za moyo wao, kwa sababu ya kujisikia wamekata tamaa na kufadhaika. Kwa hiyo, hatua iliyochukuliwa na kumalizwa sasa inakomeshwa na wanatafuta mwungano mpya. Je! hiyo si moja ya sababu kubwa zinazofanya ndoa zivunjike leo, na kuleta huzuni nyingi na uchungu?

4 Sasa na tuone jinsi mfano huo unavyoweza kulingana na mambo ya ubatizo wa Yesu, na vilevile ubatizo wako mwenyewe.

UHUSIANO WENYE THAMANI NA YEHOVA

5. Wakati wa ubatizo wake, Yesu alikuwa na ujuzi na ufahamu gani mzuri?

5 Kwanza, Yesu alionaje ubatizo wake? Masimulizi ya Injili hayaelezi sana yaliyokuwa akilini mwake kabla hajakwenda “Yordani kwa Yohana [Mbatizaji], ili abatizwe.” (Mt. 3:13) Lakini, fikiria maisha yake ya kwanza. Kutokana na lililotukia akiwa na umri wa miaka kumi na miwili tu, twajua alikuwa na ufahamu mwingi sana wa Maandiko ya Kiebrania. Luka aandika kwamba “yule mtoto Yesu” alikuwa hekaluni muda mwingi wa siku tatu, “ameketi katikati ya waalimu,” na kwamba “wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.” Kumbuka, pia, aliyomwambia mama yake: “Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?” (Luka 2:43-49) Kwa wazi alikuwa anajua alizaliwa kwa mwujiza. Inaelekea pia alifahamu maana ya maneno ambayo malaika Gabrieli alikuwa amemwambia mama yake, Mariamu, alipokuwa akitangaza angechukua mimba kwa uwezo wa roho takatifu, na kwamba mwanawe angepewa ufalme na Mungu. Je! si pia angeelekea kujua maana ya maneno ambayo Simeoni alimwambia Mariamu kwa kuongozwa na Mungu, kwamba “nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako,” akitabiri majonzi ya Mariamu wakati angeona mwanawe juu ya mti wa mateso?​—⁠Luka 1:30-33; 2:34, 35.

6. (a) Kwa kujitoa abatizwe, Yesu alionyesha alikuwa akitambua sana nini? (b) Nia ya Yesu ilikuwa nini, na msingi wa nia hiyo ulikuwa nini? (Yohana 4:34)

6 Kutokana na hayo yote tunaweza kukata maneno kwamba, hasa Yesu alipokuwa akikaribia umri wa miaka 30, alikuwa akitambua sana mambo yaliyokuwa mbele yake. Alijua kwamba ubatizo wake ulikuwa mwanzo tu. Je! ulikuwa mwanzo wa huduma yake tu na thawabu ya wakati ujao akiwa mwaminifu? Sivyo. Liko jambo lililoambatana na mambo hayo, ambalo sasa lilikuwa likizidi sana. Jambo hilo lenye kuzidi na lenye maana na thamani zaidi lilikuwa uhusiano wake na Baba yake wa kimbinguni, na sasa ulikuwa ukizidi kuwa na maana, maana ya kiroho. Hii inaonyeshwa katika Zaburi 40:6-10, ambayo Yesu bila shaka alitambua ilikuwa ikimtaja yeye mwenyewe kwa njia ya unabii, ikieleza juu ya kutolewa dhabihu kwa mwili wake mkamilifu wa kibinadamu ukiwa bora kupita dhabihu zote za wanyama zilizotolewa chini ya Torati iliyopewa kupitia kwa Musa. Mtajo wa Paulo wa fungu hilo la maneno katika Waebrania 10:5-9 wahakikisha huo ndio ufahamu sahihi. Walakini, nia ya Yesu ilikuwa nini, na msingi pia wa nia hiyo ulikuwa nini, ijapokuwa angeteswa na kuuawa ndipo atoe dhabihu hiyo? Angalia jibu linalotolewa katika Zaburi 40:8: “Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; naam, sheria yako imo moyoni mwangu.”

7. (a) Sikuzote Yesu aliendelea kuwa na uhusiano gani na Baba yake, na ni nini kilichomwongoza afanye hivyo? (b) Baada ya ubatizo wake, Yesu aliendelezaje uhusiano huo na kuutia nguvu? (Ebr. 5:7-9)

7 Hilo linaeleza kwa ufasaha nia ya Yesu na vilevile kuthamini kwake kwingi na kichocheo cha moyoni kilichomwongoza aendelee kuwa na uhusiano wa kutii na kujipa sikuzote kwa Baba yake wa kimbinguni! Yesu alipendezwa sikuzote na kufanya mapenzi ya Baba yake, hasa alipojua wakati wake ulikuwa umefika wa kuanza kufuata mwendo wa kutoa dhabihu. Ubatizo wake ulikuwa hatua ya kwanza tu. Baada ya hapo angeendeleza na kutia nguvu uhusiano huo kwa kutafuta sikuzote kumpendeza na kumheshimu Baba yake, hata kutokee nini. Kama. alivyomwambia Baba yake alipokuwa karibu kupatwa na jaribu la mwisho lenye maumivu makuu: “Baba, uniokoe katika saa hii . . . Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii. Baba, ulitukuze jina lako.”​—⁠Yohana 12:27, 28.

8. (a) Wewe uliona furaha gani ulipofanya maendeleo ukafikia hatua ya wakf? (b) Kama Yesu, unaweza kufahamu nini unapotaabika? (Marko 10:28-30)

8 Hata hivyo, namna gani juu yako? Je! mfano ule wa ndoa unakuhusu na kukusaidia kwa vyo vyote? Bila shaka, mtu akilinganisha maisha yako ya kwanza na ya Yesu kabla hajafika umri wa miaka 30 hayawezi kulingana. Walakini, je! haiwezi kusemwa ulifurahi sana ulipojua kweli inayoonyesha Yehova ni Mungu wa namna gani, “Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli”? (Kut. 34:6) Je! wewe, kama Yesu, hukufurahi sana ulipojua kusudi la Yehova, na vilevile ulipoona jinsi unavyoweza kuingia katika kusudi hilo? Ukapata kujua kwamba kwa kuchukua hatua ya wakf unaweza kuhesabiwa kati ya wale ambao Paulo aliandika hivi juu yao: “Naye [Yehova] alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.” (Kol. 1:13) Kama Yesu, bila shaka uliona kwamba kutambuliwa kama mtumishi wa Yehova aliye wakf kungetia ndani kutaabika. Yaelekea ulipatwa na majaribu na upinzani fulani kabla hujabatizwa, lakini ulithamini ubora wa mambo uliyojifunza na ukakaza nia ushikamane nayo.

9. (a) Ulinganifu wa uhusiano wa ndoa unaingiaje? (b) Wakati wa ubatizo, uliingia katika uhusiano gani wenye upendeleo, na yakupasa uuoneje? (Mik. 4:5) (c) Sasa ni ulizo gani kubwa linalokukabili?

9 Hapa ndipo ulinganifu wa uhusiano wa ndoa unapoingia. Je! wewe ulikuwa ukiona hapa karibu tu au ulikuwa ukiona mbele ulipojiweka wakf na kubatizwa? Je! ulijisikia kwamba umefanya yote’yaliyotakiwa? Au ulikuwa unajua umeingia katika uhusiano wa kipekee, si na kiumbe mwenzako, bali na Yeye Aliye Juu Zaidi ya vyote katika ulimwengu wote, lakini ambaye ungeweza kusema naye kwa usiri na ambaye ungeweza kumsihi kama Baba yako? Je! ulifahamu kwamba ulikuwa umeanza jambo lisilo la kuchukuliwa vivi hivi tu, bali ambalo lingeweza kusitawishwa na lazima lisitawishwe na kulindwa, ama sivyo litapungua na kuwa katika hatari ya kuharibika na pengine likome? Je! uliamua kwamba chini ya hali zote ungetaka kusema, kama Yesu: “Baba, ulitukuze jina lako”? Kwa hiyo ulizo kubwa unalopaswa kujiuliza ni hili: Jambo hili lenye thamani nyingi sana, uhusiano huu ambao nimeingia pamoja na Baba yangu wa kimbinguni, wawezaje kutiwa nguvu na kuzidishwa?

KUJENGA JUU YA MSINGI IMARA

10. (a) Kwa sababu gani yakupasa uwe na funzo la kipekee la Biblia lenye bidii? (b) Wawezaje kufanya hivyo? (2 Tim. 3:14, 16, 17)

10 Jambo la maana zaidi ni jinsi unavyofanya fumo lako la kipekee la Biblia, na kujua jinsi ya kutumia unayojifunza katika maisha yako ya kila siku. Sikuzote Yesu alipendezwa na kufanya mapenzi ya Mungu, kwa sababu aliweza kusema: “Sheria yako imo moyoni mwangu.” (Zab. 40:8) Alikuwa amejifunza Neno la Mungu na aliweza kulitumia. Wewe pia waweza kuwa ivyo hivyo, kama Zaburi 1:1-3 inavyotaja: “Heri mtu yule . . . [ambaye] sheria ya [Yehova] ndiyo impendezayo, na sheria yake huitafakari mchana na usiku.” Halafu inaeleza jinsi mtu huyo atakavyokuwa kama mti ambao sikuzote una matunda na haunyauki kamwe, “na kila alitendalo litafanikiwa.” Hiyo maana yake si kusoma Biblia kijuujuu tu. Inahitaji kuendelea kuchunguza sana yote yaliyomo katika Neno la Mungu, na vilevile chakula cha kiroho na mashauri yanayotolewa na “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” halafu kuona yanahusuje kila upande wa maisha yako.​—⁠Mt. 24:45-47.

11. (a) Kusudi la kutwaa maarifa sahihi ni nini? (Flp. 1:9-11) (b) Lazima tufanyize kifungo cha namna gani na Yehova, na kwa njia gani?

11 Usifanye kosa la kudhani kwamba funzo ni kutwaa maarifa ya kichwani tu juu ya mambo ya msingi ya kweli. Maarifa sahihi ni ya lazima kabisa, lakini kusudi lake si uweze kukumbuka kwa kichwa mambo mengi sana na tarakimu nyingi. Bali, kusudi ni uweze kujawa na ‘hekima yote na ufahamu wa kiroho; uenende kama ulivyo wajibu wako kwa Yehova, ukimpendeza kabisa; ukizaa matunda kwa kila kazi njema, upate kuwa na saburi ya kila namna na uvumilivu pamoja na furaha.’ (Kol. 1:9-11) Kama vile katika ndoa, hiyo yamaanisha kukua katika ufahamu na ushikamanifu, kufanyiza kifungo kisichoweza kuvunjwa kamwe. Kuna wakati ambao Wakristo Waebrania walipata kuwa “wavivu wa kusikia.” Hawakuwa na funzo la kipekee wala hawakutumia mambo waliyojifunza na walihitaji maziwa kama vitoto vichanga. Kwa hiyo angalia yale Paulo aliyowaandikia: “Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.” Maarifa ya kichwani siyo peke yake yanayookoa, bali ile ile roho ya kweli, “kuipenda ile kweli.”​—⁠Ebr. 5:11-14; 2 The. 2:10; 1 Kor. 8:1.

12. (a) Ni ukosefu gani unaoharibu uhusiano wa kibinadamu mara nyingi? (b) Ni sifa gani hasa inayotakiwa ili kutengeneza uhusiano mwema? (Luka 14:11)

12 Halafu, iko sala. Hapa tena mfano wa ndoa utatusaidia. Je! kukosa maongezi siyo ishara ya kwanza ya mtengano kati ya mume na mke? Huenda sababu yenyewe isiwe wazi. Huenda kukawa ni kutoelewana tu, au huenda ikawa mmoja ana hali ya kuona haya na hasemi sana. Walakini, wakiendelea bila kuzungumza, uhusiano wao utaharibika. Unaweza kutengenezwa wakijisikia wanajitahidi kuanza tena mazungumzo. Hilo si jambo jepesi. Wote wawili wanahitaji zaidi sifa moja kuliko zile nyingine, na hiyo ndiyo unyenyekevu.

13. Baadaye, ni tatizo gani laweza kukua kuhusu sala? (1 Pet. 4:7)

13 Hiyo inatumikaje katika njia ya kiroho? Pengine ulipokuwa ukielekea kujiweka wakf na kubatizwa hakukuwa na matatizo makubwa. Kuthamini kweli na kumpenda Mpaji wa kweli ndiyo mambo yaliyokuongoza uchukue hatua hizo za kwanza, na katika sala ulimwambia Yehova unamshukuru sana na kwamba unataka kujipa kwake kabisa kwa nafsi vote. Ulikuwa ukianza kufuata njia mpya ya maisha. Walakini, kwa sababu ya kutokamilika na sababu nyingine, upya huo unaweza kwisha, kama uwezavyo kwisha katika ndoa. Huenda wakati ukatokea ambao utaona kidogo kidogo au vingine, kwamba inakuwa vigumu kwako kusali au unaona kama desturi tu. Utafanyaje?

14. Sala zako zikizuiwa, waweza kufanya nini? (Yak. 5:14, 15)

14 Usitoe udhuru wala kujaribu kujitetea. Hicho ni kinyume cha unyenyekevu. Bali, jitahidi kwa uaminifu na unyofu kuonyesha wazi sababu yenyewe. Je! dhamiri yako inasumbukia jambo fulani? Linaweza kuzuia sala zako kwa vyepesi. Je! pengine umekuwa mzembe kidogo, ukaacha mikazo ya. maisha ya kila siku ichukue mwingi mno wa wakati wako na fikira zako? Je! ni udhaifu unaorudirudi uliotia mizizi sana kuliko ulivyodhani? Huenda ukafikia hatua ya kujiambia: Mimi sitaweza kamwe kumaliza nililoanza. Ikiwa ugumu umekuwa mkubwa sana hata waona huwezi kumwendea Yehova katika sala, njia ya pekee ni kumwendea mmoja wa watumishi wa Yehova na kuomba msaada wake, na ni vizuri zaidi awe mwangalizi au mtu mwingine aliyekomaa. Hiyo itahitaji uwe na unyenyekevu lakini huenda tatizo lisiwe kubwa kama. ulivyodhani, na jitihada yako haitakuwa ya bure. Hata katika maisha ya jamaa, nyakati nyingine ndugu au dada mzee atasaidia kijana anyoshe mambo na baba au mama. Ndivyo inavyoweza kuwa katika jamaa ya Mungu.

15. Sala zinazotoka moyoni kuelekezwa kwa Yehova zina faida gani? (Mt. 6:6)

15 Sala ni ya maana sana​—⁠si ile ya desturi tu, bali sala inayoonyesha unathamini sana mambo yote mema ambayo Yehova ametufanyia sisi, na wengine pia. Naam, tunataka kuonyesha tunafikiria wengine kwa upendo, na kuomba Mungu awasaidie watatue matatizo yao na atusaidie sisi pia na matatizo yetu wenyewe. Hiyo itatulinda tusiwe wenye kujifikiria wenyewe tu, kinyume cha unyenyekevu.

16. (a) Mtunga zaburi anatusaidiaje tukumbuke ubatizo ni mwanzo tu? (b) Yesu alituwekeaje mfano mwema?

16 Liko jambo jingine la maana ili tumalize kujenga juu ya msingi imara, kutusaidia tukumbuke ubatizo wetu ulikuwa mwanzo tu. Hilo, pia, linatajwa katika Zaburi 40, mistari 9 na 10: “Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa. Sikuzuia midomo yangu; Ee [Yehova], unajua . . . Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako. Sikuficha fadhili zako wala kweli yako katika kusanyiko kubwa.” Ndivyo alivyofanya Yesu, na alikaza nia amalize aliloanza alipobatizwa. (Yohana 4:34) Maneno haya ya mtunga zaburi kwanza yanaonyesha alimpenda sana Yehova na sifa zake njema na pia alitaka sana kuona jina jema la Yehova likishuhudiwa kabisa. Yanaonyesha pia kwamba alikuwa na upendo wa kweli wa kijirani, kutaka kwa unyofu wengine wajue mambo hayo, hasa wenye sikio la kusikia ambao wangeitikia na kusaidia kujenga “kusanyiko kubwa.” Kwa kufuata maneno hayo, Yesu alituwekea mfano mwema.​—⁠Mt. 9:36-38; Yohana 17:6, 18-21.

17. Twawezaje kuonyesha tunahangaikia watu? (Luka 10:2, 5, 6)

17 Jambo moja lastahili kuangaliwa. Wakati Yesu alipokuwa akienda hapa na pale hakuwa na nakala ya Maandiko ya Kiebrania mkononi, hata hivyo alipofundisha sikuzote alitaja vile Maandiko hayo yalivyosema. Kwetu wenyewe, ni rahisi kwenda hapa na pale tukiwa na Biblia. Kwa hiyo ni jambo lenye faida kujifunza jinsi ya kutumia Biblia yenyewe wakati tunapotolea watu ushuhuda. Yatupasa tuhangaikie watu, na kuonyesha tunawahangaikia kwa kuwarudia waonyeshapo wanapendezwa, tukijitahidi kuanza mafunzo ya Biblia katika nyumba zao,

18. Ni kwa njia gani waliobatizwa wanavyoweza kupanua utendaji wao? (1 Kor. 16:9)

18 Huenda pia ukawa na nafasi za kupanua utendaji wako, kama mhubiri wa kundi, kama mtangazaji msaidizi wa habari njema au wa wakati wote, au kama misionari au mshiriki wa jamaa ya Betheli. Bila shaka, si kila pendeleo la utumishi. lililo wazi kwa kila mtu, lakini mtu akiwa na hamu nyingi na akipanga mambo vizuri, akionyesha hamu yake katika sala, kwa kawaida anafunguliwa njia ya kushiriki zaidi kufanya mapenzi ya Yehova.

19. Kama mtu aliyebatizwa, yakupasa uendelee kuthamini nini moyoni mwako? (2 Kor. 4:6, 7)

19 Usidhani kamwe mtu fulani anajaribu kukukaza. Lakini yakupasa uendelee kuthamini moyoni mwako mambo yote yanayofananishwa na ubatizo wako. Kama mtumishi aliye wakf wa Yehova una hali yenye pendeleo zaidi sana. Yakupasa ujisikie kwamba jamaa ya mbinguni na duniani ya Yehova inapendezwa sana nawe, kwa hiyo yakupasa uchochewe utake kusonga mbele katika utumishi wako kwa Yehova. Usisahau. Ubatizo wako ulikuwa mwanzo tu. ​—⁠Kutoka The Watchtower, Aug. 15, 1976.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki