Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 12/1 kur. 531-532
  • Ni Kwa Kadiri Gani Fadhili Zapaswa Zionyeshwe?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Kwa Kadiri Gani Fadhili Zapaswa Zionyeshwe?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Habari Zinazolingana
  • Kujitahidi Kuonyesha Fadhili Katika Ulimwengu Wenye Uadui
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Pendeza Yehova kwa Kuonyesha Fadhili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Lazima Watu wa Mungu Wapende Fadhili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Fadhili​—Sifa Inayoonyeshwa kwa Maneno na Matendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 12/1 kur. 531-532

Ni Kwa Kadiri Gani Fadhili Zapaswa Zionyeshwe?

FADHILI ni sifa tunayofurahia kuona wengine wakiwa nayo. Ndivyo inavyokuwa hasa wakati sisi tunapoonyeshwa fadhili hizo. Na hata tufanyapo kosa twatumaini kuonyeshwa fadhili.

Yehova Mungu anahesabu sifa ya fadhili kuwa ya maana sana. Mara nyingi Biblia inasema, “Fadhili zake ni za milele.” (Zab. 136) Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, alimjua zaidi ya mtu mwingine ye yote. Yesu alishauri wanafunzi wake wamwige Mungu, ambaye ‘ni mwema hata kwa wasiomshukuru, na waovu.’​—Luka 6:35.

Basi, Mungu alifanya vizuri sana kuwekea wale wanaotaka kuwa na upendeleo wake takwa kubwa la kuwa wenye fadhili. Yeye anamwambia yafuatayo mtu anayedai kwamba anamtumikia: “Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na [Yehova] anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema [fadhili, tafsiri ya New World], na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!”​—Mik. 6:8.

Tunaposhughulika na watu, huenda hali zenye kuudhi zikatokea na kutuzuia tusionyeshe fadhili. Ndivyo ilivyo hasa tunapokabiliwa na adui zetu. Lakini Yesu alisema yafuatayo juu ya jambo hilo: “Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi; ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni.”​—Mt. 5:44, 45.

Labda wajibu ulio mgumu zaidi kwa Mkristo ni kupenda adui na kuwatendea kwa fadhili. Tena, licha ya kuwa wajibu, lazima fadhili hizo zionyeshwe kwa moyo wa kupenda. “Adui yako akiwa na njaa, mlishe,” na, “usifurahi, adui yako aangukapo; wala moyo wako usishangilie ajikwaapo”​—hizo ni kanuni ambazo Mkristo lazima atimize kwa moyo wa kupenda.​—Rum. 12:20; Mit. 24:17.

Hiyo haina maana ya kwamba Mkristo hawezi kukaripia mwenzake, kumwonyesha kosa au ubaya wa matendo yake. Anaweza hata ‘kukaripia mtu kwa ukali,’ kumsadikisha na kumwepusha na matokeo ya kuendelea katika njia mbaya.​—Tito 1:13, tafsiri ya New World.

Tunao mfano wa Yesu Kristo. Yeye alieleza adui zake mambo waziwazi. Lakini hakuwatenda kwa uadui wala hakujaribu kujilipia kisasi walipomwambia mambo ya kumshambulia. Alipokuwa duniani hakuhukumu watu mmoja mmoja, wala hakuwalaani. Alitaja hukumu za Baba yake tu.​—Yohana 5:30.

Kwa mfano, alipokuwa akiongea na adui zake wakubwa kupita wote, yaani, waandishi na Mafarisayo, alifunua wazi ubaya wao, kwa maana Mungu alimweleza wazi nia yao ya moyoni. Aliwaonya juu ya hukumu ya Mungu iliyotajwa katika Maandiko. Badala ya kusema, Mimi ni Mwana wa Mungu nami nitahakikisha mmetumbukizwa Jehanum,’ aliwauliza ulizo la kuwaonya: “Mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?” (Mt. 23:33) Wangeweza kufanya hivyo mmoja mmoja kwa kuacha mwendo wao wenye msiba.

Wakati Yesu alipotendwa uadui mbaya kupita wote na Wayahudi na askari Warumi, akatendwa vibaya kuliko mtumwa, “hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya.” (1 Pet. 2:23; Mt. 27:27-31) Mkristo wa kwanza kufia imani, mwanafunzi Stefano, alifuata kielelezo hicho alipokuwa akiuawa na Wayahudi kwa mawe, akasali hivi: “Bwana, usiwahesabie dhambi hii.”​—Matendo 7:60.

Yawapasa wanaodai kuwa Wakristo wajiangalie wasionyeshe fadhili chache kuliko fadhili na ukarimu unaoonyeshwa nyakati nyingine na watu wasio watumishi wa Mungu. Katika ulimwengu kuna watu wanaotenda fadhili kwa sababu Mungu aliumba mwanadamu akiwa na sifa hiyo. Lakini kutokamilika kumefifisha sifa hiyo. Kwa hiyo lazima Mkristo ajitahidi asipungukiwe na sifa hiyo ya lazima.

Fikiria jinsi wengi waliodai kumtumikia Mungu walivyoaibishwa na watu wa kisiwa cha Melita siku za mitume. Watu hao wa Melita, kutia na mkuu wa kisiwa hicho, walimpokea mtume Paulo na wenzake waliovunjikiwa merikebu pamoja, wakiwa watu karibu 276, wakawafanyia “fadhili zisizokuwa za kawaida.” Waliwatunza miezi mitatu. Naye Luka, aliyekuwa katika kundi hilo lililovunjikiwa merikebu, atuambia kwamba merikebu nyingine ilipopatikana, wanakisiwa hao wenye fadhili “wakatuheshimu kwa heshima nyingi; basi tulipoabiri wakatupakilia vitu vile tulivyokuwa na haja navyo.”​—Matendo 28:1, 2, 10, 11; 27:37.

Lo! jinsi fadhili za watu hao zilivyowalaani watu wa miji ya Israeli waliomsikia Mwana wa Mungu akinena kwa masikio yao wenyewe na kuona miujiza yake, lakini wakamtenda vibaya sana na kumdharau!

Vivyo hivyo, leo tunaona na kusoma habari za fadhili za ajabu sana zilizoonyeshwa na wanadamu, ambazo zinakuwa nyingi sana zikilinganishwa na fadhili zinazoonyeshwa na wengine wanaodai kuwa watumishi wa Mungu walio wakf. Bila shaka Mungu anaziona fadhili hizo za wanadamu, ikiwa kweli wanazionyesha kwa moyo, naye atawapa nafasi ya kujifunza habari zaidi juu yake mwenyewe na sifa zake bora. Mashahidi wa Yehova watasaidia watu hao kwa fadhili, ambao mioyo yao inafunguliwa na Mungu watake kumjua.

Je! kuna wakati wo wote unaofaa kutenda watu kwa njia isiyo ya fadhili? Je! kuna faida za kutotendea watu fadhili? Hapana. Huenda mtu akauliza, ‘Lakini namna gani unaposhughulika na watu wanaoacha kanuni za Mungu zenye haki, au watu wanaoonyesha roho ya ushupavu, uasi, ya kutotubu? Je! inatupasa tuonyeshe watu hao fadhili?’

Wanaofanya kosa watasaidiwa zaidi na fadhili, si uadui, ambao ni namna ya ukatili. Kwa sababu gani ye yote kati ya sisi tunaotaka tuonyeshwe fadhili nyakati zote amhukumu mwanadamu mwenzake akisema hastahili fadhili wala heshima? Watu wana mambo mengi yanayowalemea, kwa hiyo haitupasi kuwaongezea mzigo kwa kuwatenda kwa njia isiyo ya fadhili.

Na hata ikiwa mtu ni mshupavu, anavunja sheria ya Mungu bila kutubu, je! ye yote kati yetu anaweza kusema kwamba mtu huyo hatatubu hata siku moja? Mungu peke yake ndiye anayeweza kuamua kama ametenda dhambi asiyoweza kusamehewa. (Mt. 12:32) Tena, uadui unaelekea kuzuia zaidi watenda makosa wasitubu.​—Rum. 2:4.

Hata wakati kundi liliposumbuliwa na migawanyiko iliyoletwa na waasi, mtume Paulo hakufanya ukatili, bali aliandika hivi: “Basi, mimi Paulo mwenyewe nawasihi kwa upole na utaratibu [fadhili, tafsiri ya New World] wa Kristo.” (2 Kor. 10:1) Neno la Kigiriki lililotafsiriwa hapa kuwa “utaratibu” linamaanisha kiasi, upole, akili. Linakwenda pamoja na uanana. Tunafurahi sana tunapokuwa karibu na mtu mwenye kututendea kwa uzuri na akili. Tunafuata mashauri yake kwa wepesi zaidi.

Basi, ili kumwiga Mungu acheni wote wanaojitahidi kuwa mashahidi waaminifu wa Yehova wajitahidi kusitawisha tunda hili la roho ya Mungu linalotuletea furaha na kufanya iwe vyepesi wanaotaka kumtumikia Mungu wafanye hivyo.​—Gal. 5:22.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki